• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
    • eVibali |
Shinyanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Shinyanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Yetu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
      • Afya
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Shinyanga
    • Wilaya ya Kahama
    • Wilaya ya Kishapu
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu
    • Halmashauri ya Mji wa Kahama
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu
    • Halmashauri ya Wilaya ya Msalala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
    • Bandari Kavu
  • Huduma
    • Kutoa Ushauri wa Kitaalam
    • Kutafsiri Sheria na Sera
    • Kuratibu Shughuli za Wadau
    • Ulinzi na Usalama
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Tafiti
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha

AFISA UTAMADUNI MKUU AHITIMISHA SIKU YA NNE YA TAMASHA LA UTAMADUNI UKUNE, APONGEZA JUHUDI ZA KUHIFADHI MILA NA DESTURI ZA KISUKUMA.

Posted on: August 23rd, 2025

Afisa Utamaduni Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, Janeth Elias Mompome, amehitimisha kwa heshima kubwa siku ya nne ya Tamasha la Nne la Utamaduni lililofanyika katika Himaya ya UKUNE, kijiji cha Iboja, Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu, akisisitiza umuhimu wa kuenzi na kudumisha mila na desturi nzuri za Kisukuma.

Tamasha hilo ambalo limekuwa jukwaa la kipekee la kuonesha utajiri wa tamaduni za kabila la Wasukuma, limebeba ujumbe mahsusi wa kutekeleza agizo la Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, alilolitoa mwaka 2022 akiwa jijini Mwanza, akihimiza kila mkoa kuandaa matamasha ya utamaduni ili kurithisha urithi huu kwa vizazi vya sasa na vijavyo.

Katika tamasha hilo lililofanyika Agosti 22,2025 Halmashauri ya Ushetu,  Bi. Janeth alipata nafasi ya kutembelea mashindano ya vikundi mbalimbali vya sanaa ya utamaduni, ambavyo vilionesha vipaji vya kipekee katika ngoma, mavazi, nyimbo na maigizo ya kitamaduni.

Akimpongeza Chifu Mkuu Hangaya kwa kuendelea kulisimamia tamasha hilo kwa mafanikio, Afisa huyo wa Utamaduni alieleza kuwa utamaduni ni uti wa mgongo wa jamii yoyote na unastahili kulindwa kwa gharama yoyote ile.

Katika kilele cha siku hiyo, washindi wa mashindano ya sanaa walitangazwa na Bi. Janeth alikabidhi zawadi kwa vikundi vitatu bora vilivyoibuka kidedea, akisisitiza kuwa Serikali itaendelea kuunga mkono juhudi za kuhifadhi urithi wa kitamaduni.

Tamasha hilo limeendelea kuwa alama ya mshikamano, urithi na utambulisho wa jamii ya Kisukuma ndani ya Mkoa wa Shinyanga na Tanzania kwa ujumla.

Matangazo

  • No records found
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • AFISA UTAMADUNI MKUU AHITIMISHA SIKU YA NNE YA TAMASHA LA UTAMADUNI UKUNE, APONGEZA JUHUDI ZA KUHIFADHI MILA NA DESTURI ZA KISUKUMA.

    August 23, 2025
  • WAZIRI LUKUVI ATEMBELEA MGODI WA NYANDOLWA, AFIKISHA MAELEKEZO YA RAIS SAMIA

    August 22, 2025
  • MSANII MBOSSO AMTEMBELEA MKUU WA MKOA WA SHINYANGA OFISINI KWAKE.

    August 22, 2025
  • RC MHITA ATAKA KASI KUONGEZWA KWA UTOAJI VITAMBULISHO VYA WAFANYA BIASHARA,ARUHUSU SOKO LA IBINZAMATA KUTUMIKA KAMA GULIO.

    August 22, 2025
  • Angalia zote

Video

RC MHITA ALIVYOTOA KIBALI CHA KUTUMIKA KWA SOKO LA IBINZAMATA KUWA GULIO.... ASISITIZA ...
Video Nyinginezo

Viunganishi vya Haraka

  • Historia
  • Dira na Dhima
  • Hotuba Mbalimbali
  • Video Mbalimbali
  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Picha za Matukio
  • Miongozo na kanuni

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Mfumo wa kutuma, kupokea na kufuatilia malalamiko, mapendekezo, maulizo na pongezi
  • Ofisi ya Rais Menejimenti ya utumishi wa Umma
  • Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Boma Street, Mwanza Road

    Anuani: P.O.Box 320, Shinyanga

    Simu: +255 28 2762222

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras@shinyanga.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2018. Mkoa wa Shinyanga. Haki zote zimehifadhiwa