• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
    • eVibali |
Shinyanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Shinyanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Yetu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
      • Afya
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Shinyanga
    • Wilaya ya Kahama
    • Wilaya ya Kishapu
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu
    • Halmashauri ya Mji wa Kahama
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu
    • Halmashauri ya Wilaya ya Msalala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
    • Bandari Kavu
  • Huduma
    • Kutoa Ushauri wa Kitaalam
    • Kutafsiri Sheria na Sera
    • Kuratibu Shughuli za Wadau
    • Ulinzi na Usalama
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Tafiti
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha

TAKUKURU SHINYANGA YAWEKA MIKAKATI YA KUPAMBANA NA RUSHWA KUELEKEA UCHAGUZI MKUU YAWAPA MAFUNZO WANAHABARI

Posted on: September 25th, 2025

Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) Mkoa wa Shinyanga imeanza kuchukua hatua thabiti kuelekea Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 29, 2025 kwa kuwakutanisha waandishi wa habari na kuwapatia mafunzo maalum ya kupinga vitendo vya rushwa katika kipindi hiki nyeti.

Mafunzo hayo yamefanyika Septemba 25, 2025 katika Ukumbi wa Ofisi ya TAKUKURU Mkoa wa Shinyanga, yakilenga kuwawezesha wanahabari kuelewa kwa kina Sheria ya Kuzuia Rushwa, Sheria ya Gharama za Uchaguzi, na namna bora ya kushiriki katika mapambano dhidi ya rushwa kwa kutumia kalamu na vipaza sauti vyao.

Akifungua rasmi mafunzo hayo, Kaimu Mkuu wa TAKUKURU Mkoa wa Shinyanga, Bi. Mwamba Masanja, amesisitiza kuwa vyombo vya habari ni nguzo muhimu ya uwajibikaji katika jamii, na hivyo vina nafasi ya kipekee katika kuelimisha umma kuhusu madhara ya rushwa, hasa wakati huu wa uchaguzi.

"Ni wajibu wenu kuhakikisha elimu hii haibaki humu ukumbini, bali inafika kwa wananchi kupitia vipindi, makala, na mijadala mnayoandaa. Wananchi wakielimika watatambua kuwa kutumia haki yao ya kupiga kura ni hatua ya kuikataa rushwa na kuchagua viongozi wanaofaa,” amesema Bi. Masanja.

Kwa upande wake, Mkuu wa Dawati la Elimu kwa Umma TAKUKURU Shinyanga, Bw. Mohammed Doo, amewataka wanahabari kuendelea kuwa mabalozi wa uadilifu, kwa kuhakikisha taarifa wanazochapisha au kutangaza hazichochei au kufumbia macho vitendo vya rushwa, bali zinakuwa sehemu ya ujenzi wa taifa.

“Vyombo vya habari vinaweza kuhamasisha uwajibikaji, kwa kuwafikia wananchi kwa lugha rahisi kuhusu madhara ya rushwa na umuhimu wa kuchagua viongozi bora kwa maslahi ya maendeleo ya taifa letu,” amesema Doo.

Mafunzo hayo yaliambatana na kaulimbiu isemayo:

“Kuzuia Rushwa ni Jukumu Lako na Langu – Tutimize Wajibu Wetu.”

Wanahabari waliohudhuria wamepongeza hatua hiyo ya TAKUKURU, wakiahidi kuwa mabalozi wa mapambano dhidi ya rushwa, hasa katika kipindi hiki cha uchaguzi.


Matangazo

  • No records found
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • RC MHITA ARIDHISHWA NA UTOAJI HUDUMA HOSPITALI YA RUFAA YA MKOA WA SHINYANGA.

    September 28, 2025
  • WATENDAJI AMCOS WATAKIWA KUWA WABUNIFU ILI KUONGEZA UZALISHAJI NA THAMANI YA MAZAO YA KIBIASHARA.

    September 27, 2025
  • RC MHITA AITEMBELEA SHULE YA WASICHANA SHINYANGA, ATOA WITO WA KUWEKEZA KATIKA MAADILI NA ELIMU BORA KWA MTOTO WA KIKE.

    September 27, 2025
  • HALMASHAURI SHINYANGA ZATAKIWA KUTENGA BAJETI KUENDELEZA UTOAJI WA HUDUMA ZA MADAWATI YA USTAWI WA JAMII KATIKA STENDI ZA MABASI

    September 27, 2025
  • Angalia zote

Video

RC MHITA AAGIZA MKANDARASI KUKATWA MILIONI 2 KILA SIKU KWA KUCHELEWESHA BARABARA KAHAMA
Video Nyinginezo

Viunganishi vya Haraka

  • Historia
  • Dira na Dhima
  • Hotuba Mbalimbali
  • Video Mbalimbali
  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Picha za Matukio
  • Miongozo na kanuni

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Mfumo wa kutuma, kupokea na kufuatilia malalamiko, mapendekezo, maulizo na pongezi
  • Ofisi ya Rais Menejimenti ya utumishi wa Umma
  • Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    OFISI YA MKUU WA MKOA, MKOA WA SHINYANGA, 04 MTAA WA BOMA

    Anuani: P.O.Box 37180,SHINYANGA, TANZANIA

    Simu: +255 28 2762222

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras@shinyanga.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2018. Mkoa wa Shinyanga. Haki zote zimehifadhiwa