• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
    • eVibali |
Shinyanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Shinyanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Yetu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
      • Afya
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Shinyanga
    • Wilaya ya Kahama
    • Wilaya ya Kishapu
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu
    • Halmashauri ya Mji wa Kahama
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu
    • Halmashauri ya Wilaya ya Msalala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
    • Bandari Kavu
  • Huduma
    • Kutoa Ushauri wa Kitaalam
    • Kutafsiri Sheria na Sera
    • Kuratibu Shughuli za Wadau
    • Ulinzi na Usalama
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Tafiti
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha

Ambaye hajaona kazi ya Magufuli kwa miaka minne achunguzwe akili- Askofu Sangu

Posted on: November 14th, 2019

Askofu wa jimbo Katoliki Shinyanga Mhashamu Liberatus Sangu ameyasema hayo leo tarehe 14 Novemba, 2019 kwenye misa ya shukrani ya Jubilee ya miaka 25 ya upadri iliyofanyika katika kanisa kuu la Mama mwenye Huruma, Parokia ya Ngokolo, Manispaa ya Shinyanga.

Akitoa salamu za shukrani kwa Mgeni rasmi Waziri wa Habari, Sanaa, Utamaduni na Michezo, Mhe. Harrison Mwakyembe pamoja na wote walioshiriki kuadhimisha Jubilee hiyo, Sangu amesema kuwa, Serikali la awamu ya tano imefanya mambo makubwa ambayo kwa mtu mwenye akili timamu anapaswa kupongeza.

"Mtu ambaye hajaona Rais Magufuli amefanya nini kwa kipindi cha miaka minne achuguzwe akili, kama ana akili timamu basi ana wivu" amesema Askofu Sangu.

Naye Mwenyekiti wa Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania Mhashamu Askofu Mkuu Gervas Nyaisonga ametumia nafasi hiyo kuwakumbusha wanataaluma mbalimbali na wapiga kura kuhakikisha uchaguzi wa Serikali za Mitaa unafanyika kwa amani na utulivu, kwa ajili ya ustawi wa Taifa.

Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Mhe. Zainab Telack, akimkaribisha Mgeni rasmi amewashukuru viongozi wa dini kwa kuendelea kuombea amani ya Nchi na kuwaomba waendelee na kazi hiyo kubwa.

"Shinyanga kuna amani, kwani mmekuwa mkifanya kazi kubwa kuombea amani ya Taifa letu ndiyo sababu tupo hapa tunasherekea kwa amani na utulivu, naomba  endeleeni kuombea amani ili tufanye kazi kwa amani na tupate chakula cha kutosha" Amesisitiza Mhe. Telack.

Aidha, Telack amewahimiza wananchi kujitokeza kwa wingi kwenye uchaguzi wa Serikali za Mitaa tarehe 24 Novemba, 2019 ili wawachague viongozi wanaowafaa.

Misa hiyo imehudhuriwa pia na viongozi mbalimbali wa Serikali akiwemo Mama Anna Makinda, Spika wa Bunge Mstaafu, Mhe. Nape Nnauye Mbunge wa Jimbo la Mtama - Lindi, Mkuu wa Wilaya ya Dodoma Mhe. Patrobas Katambi pamoja na Viongozi waandamizi wa Mkoa na Wilaya ya Shinyanga.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUOMBA NAFASI YA UJUMBE WA BODI YA HOSPITALI YA MKOA January 03, 2020
  • Matokeo ya Mtihani wa Kidato cha nne 2019 January 09, 2020
  • Matokeo ya upimaji wa Kitaifa Kidato cha pili 2019 January 09, 2020
  • Mwenge wa Uhuru kuwasili Mkoani Shinyanga May 07, 2019
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • SIKU 100

    June 27, 2021
  • SIKU MIA 100 ZA RAIS SAMIA

    June 27, 2021
  • DKT. SENGATI AHAIDI KUPAMBANA NA CHANGAMOTO YA UMASIKINI SHINYANGA

    June 05, 2021
  • Katibu Tawala Mkoa wa Shinyanga aapishwa

    June 02, 2021
  • Angalia zote

Video

MIFUKO BANDIA ZAIDI YA ELFU 20 YAKAMATWA SHINYANGA
Video Nyinginezo

Viunganishi vya Haraka

  • Historia
  • Dira na Dhima
  • Hotuba Mbalimbali
  • Video Mbalimbali
  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Picha za Matukio
  • Miongozo na kanuni

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Mfumo wa kutuma, kupokea na kufuatilia malalamiko, mapendekezo, maulizo na pongezi
  • Ofisi ya Rais Menejimenti ya utumishi wa Umma
  • Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Boma Street, Mwanza Road

    Anuani: P.O.Box 320, Shinyanga

    Simu: +255 28 2762222

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras@shinyanga.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2018. Mkoa wa Shinyanga. Haki zote zimehifadhiwa