• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
    • eVibali |
Shinyanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Shinyanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Yetu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
      • Afya
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Shinyanga
    • Wilaya ya Kahama
    • Wilaya ya Kishapu
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu
    • Halmashauri ya Mji wa Kahama
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu
    • Halmashauri ya Wilaya ya Msalala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
    • Bandari Kavu
  • Huduma
    • Kutoa Ushauri wa Kitaalam
    • Kutafsiri Sheria na Sera
    • Kuratibu Shughuli za Wadau
    • Ulinzi na Usalama
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Tafiti
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha

Angalia matukio katika picha, Umoja wa Wake wa Viongozi walivyokabidhi madarasa katika shule ya msingi Buhangija

Posted on: November 11th, 2019


Mama Tunu Pinda Mke wa Waziri Mkuu Mstaafu Mhe. Mizengo Pinda, ambaye ni Mwenyekiti wa Umoja wa wake wa Viongozi nchini akitoa neno katika hafla fupi kwenye ukumbi wa shule ya msingi Buhangija, ambapo ameelezea historia na shughuli zinazofanywa na  katika kusaidia jamii na kusema kuwa wameguswa sana na watoto wenye ulemavu lengo lililowafanya kuamua kujenga madarasa hayo

Mama Kighoma Malima ambaye ni Katibu wa Umoja wa Wake wa Viongozi, akiwatambulisha wakina mama waliopo katika Umoja huo kwenye ukumbi wa shule ya msingi Buhangija

Mkuu wa shule ya msingi Buhangija Bw. Selemani Kipanya akitoa taarifa ya shule hiyo na kuwashukuru akina mama kwa msaada walioutoa

Katibu Tawala Mkoa wa Shinyanga Bw. Albert Msovela (kulia), akitoa maelezo kwa akina mama Wake wa Viongozi kuhusu ujenzi wa matundu ya vyoo kanika eneo la ujenzi wa vyoo hivyo ambapo amewahakikishia vitakamilika baada ya muda mfupi

Mkuu wa Wilaya ya Shinyanga Mhe. Jasinta Mboneko, (katikati) na Mama Malima (wa tatu kutoka kulia), wakicheza na kufurahi na watoto wa shule ya msingi Buhangija kabla ya kukabidhi madarasa kwa Waziri Ndalichako, jana tarehe 10/11/2019

Akina mama Wake wa Viongozi, Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, Mkuu wa Wilaya ya Shinyanga, pamoja na watoto wa shule ya msingi Buhangija katika picha ya pamoja hapo jana baada ya kukabidhiwa madarasa manne yaliyojengwa na akina mama hao

Mama Mary Majaliwa Mke wa Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa akitoa neno baada ya kumkabidhi madarasa Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Mhe. Joyce Ndalichako hapo jana tarehe 10/11/2019 katika shule ya msingi Buhangija



Baadhi ya wanafunzi wa shule ya msingi Buhangija, wakicheza kwa furaha mbele ya madarasa yaliyojengwa na umoja wa wake wa Viongozi na kukabidhiwa kwa Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia hapo jana tarehe 10/11/2019


Kutoka kushoto ni Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Mhe. Prof. Joyce Ndalichako, Mama Tunu Pinda, Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Mhe. Zainab Telack, Mama Mary majaliwa na Wake wengine wa Viongozi wakiangalia moja ya chumba cha darasa kati ya vyumba vinne vilivyojengwa na Umoja wa Wake wa Viongozi jana tarehe 10/11/2019 katika shule ya msingi Buhangija


Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Mhe. Zainab Telack (kushoto) akimuongoza Mama Mary Majaliwa (katikati) na Mama Tunu Pinda (kulia) kuelekea kwenye darasa mojawapo katika shule ya msingi Buhangija


Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Mhe. Zainab Telack (mbele kushoto) akicheza kwa furaha pamoja na Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia (wa tatu kulia),Mkuu wa Wilaya ya Shinyanga (wa pili kulia) na Wake wa Viongozi, mbele ya chumba cha darasa kati ya vinne vilivyojengwa na Wake wa Viongozi shule ya msingi Buhangija


Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknoloji Mhe. Prof. Joyce Ndalichako (mwenye skafu) akikata utepe kuonesha kupokea vyumba vinne vya madarasa kutoka kwa Umoja wa Wake wa Viongozi katika shule ya msingi Buhangija 


Katibu Tawala Mkoa wa Shinyanga Bw. Albert Msovela akisoma taarifa ya ujenzi wa vyumba vya madarasa na matundu ya vyoo katika shule ya msingi Buhangija


Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknoloji Mhe. Prof. Joyce Ndalichako na mwenyeji wake Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Mhe. Zainab Telack wakipokea salamu kutoka kwa wanafunzi wa shule ya msingi buhangija baada ya kuwasili katika eneo hilo jana 


Viongozi wa Mkoa na Wilaya, Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia na Wake wa Viongozi wakiimba kwa pamoja na watoto wa shule ya msingi Buhangija (hawapo pichani)


Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Mhe. Prof. Joyce Ndalichako akivishwa skafu na Skauti baada ya kuwasili eneo la shule ya msingi Buhangija 


Mama Mary Majaliwa alipokuwa akiwasili katika eneo la shule ya msingi Buhangija hapo jana 


Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Mhe. Prof. Joyce Ndalichako akisalimiana na Katibu Tawala Mkoa Bw. Albert Msovela mara baada ya kuwasili katika shule ya msingi Buhangija


Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Mhe. Prof. Joyce Ndalichako akisalimiana na Mkuu wa Wilaya ya Shinyanga Mhe. Jasinta Mboneko mara baada ya kuwasili katika shule ya msingi Buhangija

Wake wa Viongozi wakiongozwa na Mama Mary Majaliwa pamoja na Waziri Ndalichako kutoa huduma ya chakula kwa watoto wa shule ya msingi Buhangija baada ya kukabidhi madarasa

Matangazo

  • No records found
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • NATOA WITO KWA VIJANA HAPA SHINYANGA KUREJEA NA KUTATHIMINI UPYA NJIA ZA KUJIPATIA KIPATO - RC. MACHA

    May 20, 2025
  • SERIKALI YATHIBITISHA VIFO VYA WATU SITA NA MAJERUHI 11 KATIKA AJALI YA MGODI WA MWAKITOLYO.

    May 18, 2025
  • WAZAZI NA WALEZI, NENDENI MKAWE MABALOZI SAHIHI WA KAZI ZA MHE. RAIS DKT. SAMIA SULUHU HASSAN – RC. MACHA

    May 16, 2025
  • WAZAZI NA WALEZI WEKEZENI ZAIDI KATIKA MALEZI NA MAKUZI YA WATOTO – LYAMONGI

    May 15, 2025
  • Angalia zote

Video

MIFUKO BANDIA ZAIDI YA ELFU 20 YAKAMATWA SHINYANGA
Video Nyinginezo

Viunganishi vya Haraka

  • Historia
  • Dira na Dhima
  • Hotuba Mbalimbali
  • Video Mbalimbali
  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Picha za Matukio
  • Miongozo na kanuni

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Mfumo wa kutuma, kupokea na kufuatilia malalamiko, mapendekezo, maulizo na pongezi
  • Ofisi ya Rais Menejimenti ya utumishi wa Umma
  • Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Boma Street, Mwanza Road

    Anuani: P.O.Box 320, Shinyanga

    Simu: +255 28 2762222

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras@shinyanga.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2018. Mkoa wa Shinyanga. Haki zote zimehifadhiwa