• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
    • eVibali |
Shinyanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Shinyanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Yetu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
      • Afya
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Shinyanga
    • Wilaya ya Kahama
    • Wilaya ya Kishapu
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu
    • Halmashauri ya Mji wa Kahama
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu
    • Halmashauri ya Wilaya ya Msalala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
    • Bandari Kavu
  • Huduma
    • Kutoa Ushauri wa Kitaalam
    • Kutafsiri Sheria na Sera
    • Kuratibu Shughuli za Wadau
    • Ulinzi na Usalama
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Tafiti
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha

BIL. 4.27 KUIMARISHA MAWASILIANO MKOANI SHINYANGA - MHE. NAPE

Posted on: July 19th, 2024

Na. Paul Kasembo, SHY RS.

WAZIRI wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari Mhe. Nape Moses Nnauye (Mb) amesema kuwa Serikali kupitia Mguko wa Mawasiliano kwa wote imegharamia zaidi ya shilingi Bilioni 4 ambao zitatumika kuimarisha mawasiliano mkoani Shinyanga kwa kujenga minara 30 katika Kata 29 vyenye jumla ya vijiji 83 ambapo takribani wakazi 421, 259 watanufaika huku akisisitiza matumizi sahihi na yenye faida na siyo vinginevyo.

Mhe. Nape ameyasema haya tarehe 19 Julai, 2024 wakati wa wasilisho la Taasisi mbalimbali lililofanyika mbele ya Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Mhe. Anamringi Macha katika ukumbi wa mikutano uliopo ofisi ya Mkuu wa mkoa na kuhudhuriwa na viongozi mbalimbali wa Serikali, Taasisi, kampuni za simu na wadau wa mawasiliano mkoani shinyanga.

"Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Mhe. Anamringi Macha, Serikali imedhamiria kuhakikisha kuwa kila mwananchi anafikiwa na mawasiliano ya simu, ambapo kwa mkoa huu wa shinyanga Mfuko wa Mawasiliano kwa wote ikiwakilisha Serikali inayapatia makampuni ya simu kujenga minara 30 katika Kata 29 ambapo ndani yake kuna vijiji 83 na hivyo kuwanufaisha wakazi 421, 259 wa Mkoa wa Shinyanga, hili ni jambo kubwa sana na lenye kumpongeza Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuimarisha mawasiliano kwa Wanashinyanga," amesema Mhe. Nape.

Kwa upande wake RC Macha amempongeza sana Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuendelea kuimarisha mawasiliano kwa wanashinyanga na Tanzania kwa ujumla jambo ambalo linaimarisha ulinzi, kuongeza uchumi wetu.

Akiwa Shinyanga Mhe. Nape amezindua mnara wa Kampuni ya Halotel uliojengwa katika Kata ya Busangwa ambapo Serikali imetoa fedha zake za ruzuku shilingi Mil. 145 ambapo wakazi zaidi ya 12,100 kutoka vijiji vya Mwanima, Mwajipungira, Pambe na Busangwa vyote vya Wilaya ya Kishapu watanufaika.

Kisha amemalizia kwa kukagua na kupongeza ujenzi mzuri na bora wa mnara wa Kampuni ya Honora uliopo Kata ya Bukomela, Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu wenye uwezo wa 2G, 3G, 4G na 5G ambao utawanufaisha wakazi wa vijiji vitano (5) ikiwa ni zaidi ya lengo la awali la vijiji viwili (2) na kuwafikia wakazi zaidi ya 20 elfu.


HABARI PICHA

Mhe. Nape Nnauye, Waziri wa Habari

Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Mhe. Anamringi Macha

Mkurugenzi Mtendaji Mfuko wa Mawasiliano kwa wite Bi. Justina Mashiba

Mnara wa Honora Kata ya Bukomelo - Halmashauri ya Ushetu

Mnara wa Hatolel uliojengwa Kata ya Busangwa Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu

Picha ikionesha baadhi ya wananchi waliojitokeza wakati wa hafla ya ufunguzi wa mnara wa Honora - Ushetu

Matangazo

  • No records found
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • KIKAO CHA MAPITIO YA ROBO MWAKA KWA KIPINDI CHA OKT - DES 2024 CHA (PJT MMMAM) CHAFANYIKA MKOANI SHINYANGA.

    February 28, 2025
  • RCC SHINYANGA YARIDHIA MAPENDEKEZO NANE (8) YA MATUMIZI BORA YA ARDHI.

    February 27, 2025
  • KUKAMILISHWA KWA MIRADI YA BARABARA KUTAPUNGUZA KERO KWA WANANCHI – RC MACHA

    February 26, 2025
  • WALIMU, TOENI ELIMU INAYOENDANA NA MABADILIKO YA TEKNOLOJIA -RC MACHA

    February 24, 2025
  • Angalia zote

Video

MIFUKO BANDIA ZAIDI YA ELFU 20 YAKAMATWA SHINYANGA
Video Nyinginezo

Viunganishi vya Haraka

  • Historia
  • Dira na Dhima
  • Hotuba Mbalimbali
  • Video Mbalimbali
  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Picha za Matukio
  • Miongozo na kanuni

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Mfumo wa kutuma, kupokea na kufuatilia malalamiko, mapendekezo, maulizo na pongezi
  • Ofisi ya Rais Menejimenti ya utumishi wa Umma
  • Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Boma Street, Mwanza Road

    Anuani: P.O.Box 320, Shinyanga

    Simu: +255 28 2762222

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras@shinyanga.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2018. Mkoa wa Shinyanga. Haki zote zimehifadhiwa