• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
    • eVibali |
Shinyanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Shinyanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Yetu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
      • Afya
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Shinyanga
    • Wilaya ya Kahama
    • Wilaya ya Kishapu
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu
    • Halmashauri ya Mji wa Kahama
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu
    • Halmashauri ya Wilaya ya Msalala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
    • Bandari Kavu
  • Huduma
    • Kutoa Ushauri wa Kitaalam
    • Kutafsiri Sheria na Sera
    • Kuratibu Shughuli za Wadau
    • Ulinzi na Usalama
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Tafiti
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha

DKT. KHATIBU AITAKA OFISI YA TAIFA YA MASHTAKA MKOA WA SHINYANGA KUBORESHA SEKTA KWA KUTOA HAKI KWA WAKATI

Posted on: March 16th, 2024

Na. Shinyanga RS.

NAIBU Katibu Mkuu Wizara ya Katiba na Sheria Dkt. Khatibu Kazungu ameitaka Ofisi ya Taifa ya Mashtaka Mkoa wa Shinyanga kuboresha Sekta kwa kutoa haki kwa wakati, kulinda amani na usalama kwa maendeleo ya Taifa hili, huku akisisitiza kuboreshwa kwa mnyororo wa utoaji wa haki jinai sanjari na kufanya kazi kwa kuzingatia maadili na weledi.

Dkt. Kazungu ameyasema haya leo tarehe 16/3/2024 wakati wa Hafla ya Uzinduzi wa Jengo hili lililopo Manispaa ya Shinyanga halfa ambayo imehudhuriwa na viongozi mbalimbali wakiwemo wa Serikali na Dini, ambapo pamoja na maelekezo haya Dkt. Kazungu pia amesema uzinduzi wa jengo hili unawakilisha majengo mengine (5) yaliyokamilika likiwemo la Ilala, Mkoa wa Pwani, Manyara, Katavi na Mkoa wa Rukwa. 

"Niwatake Ofisi ya Taifa ya Mashtaka Mkoa wa Shinyanga kuboresha Sekta hii kwa kutoa haki kwa wakati, kulinda amani na usalama kwa maendeleo ya Taifa hili sanjari na kuboresha mnyororo wa utoaji wa Haki Jinai huku mkizingatia maadili ya kazi zenu na weledi katila kuwatumikia wananchi wetu," amesema Dkt. Kazungu.

Kwa upande wake Ndg. Sylvester Mwakitali ambaye ni Mkurugenzi wa Mashtaka amesema kuwa, muundo wa Ofisi ya Taifa ya Mashtaka unaelekezq kuwepo kwa Ofisi za Mashtaka katika Mikoa yote na Wilaya zote. Hadi sasa zipo Ofisi katika Mikoa yote ya Kiserikali pamoja na mikoa minne ya Kimashtaka hivyo kufanya kuwa na jumla ya Ofisi 30 nq zote zinafanya kazi.

Akitoa salamu za Serikali Mhe. Joseph Mkude - DC KIshapu kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Mhe. Anamringi Macha, amemshukuru sana Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kutoa fedha zaidi ya Bil. 2 kujenga jengo hili la Ofisi ambapo kukamilika kwake kunakwenda kusogeza na kuboresha huduma kwa jamii pamoja na kuimarisha mnyororo mzima wa utoaji haki jinai.

Ofisi ya Taifa ya Mashtaka ni Taasisi iliundwa mwaka 2018 kufuatia mabadiliko ya Muundo wa Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali, ambapo iliyokuwa Divisheni ya Mashtaka chini ya Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali na kuwa huru na Mamlaka kamili.


HABARI PICHA

Dkt. Khatibu Kazungu akielezea jambo wakati wa hafla

Mhe. Joseph Mkude, Mkuu wa Wilaya ya Kishapu ambaye alimuwakilisha Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Mhe. Anamringi Macha

Matangazo

  • No records found
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • WANUFAIKA WA MIKOPO YA 10% LIPENI KWA WAKATI ILI PIA VIKOPESHWE NA VIKUNDI VINGINE - RC MACHA

    February 13, 2025
  • CP. HAMDUNI AKUTANA NA KAMATI YA MICHEZO YA JWTZ

    February 13, 2025
  • WANANCHI, LIPENI KODI YA ARDHI KWA WAKATI MUEPUKE RIBA - LEO KOMBA

    February 12, 2025
  • WAJUMBE WA BODI, TUMIENI TAALUMA ZENU KUISAIDIA HOSPITALI KUKAMILISHA MIRADI YA UJENZI- RAS CP. HAMDUNI.

    February 11, 2025
  • Angalia zote

Video

MIFUKO BANDIA ZAIDI YA ELFU 20 YAKAMATWA SHINYANGA
Video Nyinginezo

Viunganishi vya Haraka

  • Historia
  • Dira na Dhima
  • Hotuba Mbalimbali
  • Video Mbalimbali
  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Picha za Matukio
  • Miongozo na kanuni

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Mfumo wa kutuma, kupokea na kufuatilia malalamiko, mapendekezo, maulizo na pongezi
  • Ofisi ya Rais Menejimenti ya utumishi wa Umma
  • Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Boma Street, Mwanza Road

    Anuani: P.O.Box 320, Shinyanga

    Simu: +255 28 2762222

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras@shinyanga.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2018. Mkoa wa Shinyanga. Haki zote zimehifadhiwa