• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
    • eVibali |
Shinyanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Shinyanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Yetu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
      • Afya
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Shinyanga
    • Wilaya ya Kahama
    • Wilaya ya Kishapu
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu
    • Halmashauri ya Mji wa Kahama
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu
    • Halmashauri ya Wilaya ya Msalala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
    • Bandari Kavu
  • Huduma
    • Kutoa Ushauri wa Kitaalam
    • Kutafsiri Sheria na Sera
    • Kuratibu Shughuli za Wadau
    • Ulinzi na Usalama
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Tafiti
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha

HALMASHAURI SHINYANGA ZATAKIWA KUTENGA BAJETI KUENDELEZA UTOAJI WA HUDUMA ZA MADAWATI YA USTAWI WA JAMII KATIKA STENDI ZA MABASI

Posted on: September 27th, 2025

Kaimu Katibu Tawala Mkoa wa Shinyanga ambaye pia ni Katibu Tawala Msaidizi Utawala na Rasilimali Watu, David Lyamongi amezitaka Halmashauri za Manispaa ya Shinyanga na Kahama kutenga bajeti maalumu kwa ajili ya kuendeleza utoaji wa huduma katika madawati ya ustawi wa jamii yaliyopo kwenye stendi za mabasi

Alitoa agizo hilo Septemba 26, 2025 katika kikao cha tathmini ya utoaji wa huduma kwenye madawati hayo yaliyopo stendi za mabasi za Manispaa ya Shinyanga na Kahama, kikao kilichoratibiwa na Ofisi ya Mkuu wa Mkoa kwa kushirikiana na Shirika la Railway Children Africa (RCA).

Lyamongi amesema lengo la kuimarisha madawati hayo ni kuhakikisha watoto wanaoishi na kufanya kazi mitaani pamoja na makundi mengine yenye uhitaji wanapata huduma za kitaalamu zitakazosaidia kupunguza changamoto wanazokabiliana nazo.

Aidha, amezitaka mamlaka husika kuhakikisha miradi mikubwa ya ujenzi kama vile stendi mpya za kisasa zinazojengwa Manispaa ya Shinyanga na Kahama, ujenzi wa Uwanja wa Ndege wa Ibadakuli na vituo vya Treni ya Mwendo Kasi (SGR), inatenga vyumba maalumu kwa ajili ya madawati ya ustawi wa jamii, vyumba vya jeshi la Polisi pamoja na huduma ya kwanza.

Kwa mujibu wake, hatua hiyo itasaidia kupunguza ongezeko la watoto wanaoingia na kuishi mtaani.

Kwa upande wake, Mratibu wa Shirika la RCA, Bi. Irene Wampembe, amepongeza jitihada zinazofanywa na Serikali ya Mkoa wa Shinyanga kupitia madawati ya ustawi wa jamii na kusisitiza kuwa shirika hilo litaendelea kushirikiana na Ofisi ya Mkuu wa Mkoa pamoja na halmashauri kuhakikisha huduma hizo zinafika kwa walengwa.

Hata hivyo, ameziomba halmashauri kuandaa mikakati thabiti ya uendelevu wa huduma hizo kwani mradi unaotekelezwa na Shirika la RCA unatarajiwa kufikia ukomo wake mwezi Machi 2026.

Kikao hicho kimehudhuriwa na viongozi na wataalamu kutoka Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, Halmashauri za Manispaa ya Shinyanga na Kahama, Ofisi ya Latra, Ofisi ya RPC, Uhamiaji, wawakilishi wa wenyeviti wa mitaa, watendaji wa kata, watoa huduma za malezi ya mtoto pamoja na wadau kutoka Shirika la RCA.

Matangazo

  • No records found
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • RC MHITA ARIDHISHWA NA UTOAJI HUDUMA HOSPITALI YA RUFAA YA MKOA WA SHINYANGA.

    September 28, 2025
  • WATENDAJI AMCOS WATAKIWA KUWA WABUNIFU ILI KUONGEZA UZALISHAJI NA THAMANI YA MAZAO YA KIBIASHARA.

    September 27, 2025
  • RC MHITA AITEMBELEA SHULE YA WASICHANA SHINYANGA, ATOA WITO WA KUWEKEZA KATIKA MAADILI NA ELIMU BORA KWA MTOTO WA KIKE.

    September 27, 2025
  • HALMASHAURI SHINYANGA ZATAKIWA KUTENGA BAJETI KUENDELEZA UTOAJI WA HUDUMA ZA MADAWATI YA USTAWI WA JAMII KATIKA STENDI ZA MABASI

    September 27, 2025
  • Angalia zote

Video

RC MHITA AAGIZA MKANDARASI KUKATWA MILIONI 2 KILA SIKU KWA KUCHELEWESHA BARABARA KAHAMA
Video Nyinginezo

Viunganishi vya Haraka

  • Historia
  • Dira na Dhima
  • Hotuba Mbalimbali
  • Video Mbalimbali
  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Picha za Matukio
  • Miongozo na kanuni

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Mfumo wa kutuma, kupokea na kufuatilia malalamiko, mapendekezo, maulizo na pongezi
  • Ofisi ya Rais Menejimenti ya utumishi wa Umma
  • Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    OFISI YA MKUU WA MKOA, MKOA WA SHINYANGA, 04 MTAA WA BOMA

    Anuani: P.O.Box 37180,SHINYANGA, TANZANIA

    Simu: +255 28 2762222

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras@shinyanga.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2018. Mkoa wa Shinyanga. Haki zote zimehifadhiwa