• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
    • eVibali |
Shinyanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Shinyanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Yetu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
      • Afya
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Shinyanga
    • Wilaya ya Kahama
    • Wilaya ya Kishapu
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu
    • Halmashauri ya Mji wa Kahama
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu
    • Halmashauri ya Wilaya ya Msalala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
    • Bandari Kavu
  • Huduma
    • Kutoa Ushauri wa Kitaalam
    • Kutafsiri Sheria na Sera
    • Kuratibu Shughuli za Wadau
    • Ulinzi na Usalama
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Tafiti
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha

HATI SAFI ISIWALEWESHE - RC MACHA

Posted on: June 24th, 2024

Na. Paul Kasembo, KISHAPU DC.

MKUU wa Mkoa wa Shinyanga Mhe. Anamringi Macha ameitaka Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu isilewe na kujisahau baada ya kupata Hati Safi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) kwa mwaka wa fedha 2022/2023 na badala yake iwatie moyo wa kuongeza juhudi, maarifa na ufanisi katika utekelezaji wa majukumu ya kila siku ili waendelee kuipata Hati Safi kila ukaguzi unapofanyika, huku akisisitiza kuongeza umakini na kuzingatia taratibu za kihasibu na wafanye vizuri zaidi.

RC Macha ameyasema haya leo tarehe 24 Juni, 2024 wakati akichangia hoja kwenye Mkutano wa Baraza Maalum la Madiwani linalojadili maagizo ya CAG ambapo pia ametumia nafasi hii kuitaka Halmashauri kuongeza umakini na kuzingatia zaidi taratibu za kihasibu ambazo ndiyo mwishoni hutoa hatma ya kupata Hati Safi au vinginevyo.

"Pamoja na kuwapongeza kwa kupata Hati Safi ya CAG, lakini niwaombe msilewe na badala yake sasa muongeze juhudi na muongeze umakini zaidi katika utekelezaji wa majukumu yenu namzingatie taratibu zote za kihasibu ili muendelee kupata hati safi kila ukaguzi unapofanyika,"amesema RC Macha.

Kwa upande wake Katibu Tawala Mkoa wa Shinyanga Prof. Siza Tumbo amezitaka Halmashauri zote sita (6) zinazounda Mkoa wa Shinyanga kuanza kutenga fedha kutoka vyanzo vyao vya mapato ili kuweza kulipa deni la litokanalo na mkopo wa Mradi wa Upimaji Viwanja vya kuuza ambapo Halmashauri zilikopa kwa lengo la kupima na kuuza ikiwa ni sehemu ya kuongeza pato deni ambalo hivi sasa linajitokeza sana kwenye hoja za CAG.

Akiwasilisha taatifa ya Utekelezaji wa Maagizo ya CAG ambaye ni Mweka Hazina ndg. George Sumbwe kwa niaba ya Mkurugenzi wa Halmashauri ya Kishapu ndg. Emmanuel Johnson amesema kuwa katika Kishapu ilikuwa na Hoja 48 ikijumlisha na hoja za nyuma ambapo 10 zimefungwa, 36 zipo hatua mbalimbali za utekelezaji, 1 imepitwa na wakati huku 1 haijatekelezwa.

Kwa upande wake CPA Yusuph Mabwe ambaye ni Mkaguzi Mkuu wa nje wa Hesabu za Serikali Mkoa wa Shinyanga amesema kuwa maoni na mapendekezo yote yaliyotolewa na wajumbe wameyachukua na watafanyia kazi.


HABARI PICHA 


Matangazo

  • No records found
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • WANUFAIKA WA MIKOPO YA 10% LIPENI KWA WAKATI ILI PIA VIKOPESHWE NA VIKUNDI VINGINE - RC MACHA

    February 13, 2025
  • CP. HAMDUNI AKUTANA NA KAMATI YA MICHEZO YA JWTZ

    February 13, 2025
  • WANANCHI, LIPENI KODI YA ARDHI KWA WAKATI MUEPUKE RIBA - LEO KOMBA

    February 12, 2025
  • WAJUMBE WA BODI, TUMIENI TAALUMA ZENU KUISAIDIA HOSPITALI KUKAMILISHA MIRADI YA UJENZI- RAS CP. HAMDUNI.

    February 11, 2025
  • Angalia zote

Video

MIFUKO BANDIA ZAIDI YA ELFU 20 YAKAMATWA SHINYANGA
Video Nyinginezo

Viunganishi vya Haraka

  • Historia
  • Dira na Dhima
  • Hotuba Mbalimbali
  • Video Mbalimbali
  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Picha za Matukio
  • Miongozo na kanuni

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Mfumo wa kutuma, kupokea na kufuatilia malalamiko, mapendekezo, maulizo na pongezi
  • Ofisi ya Rais Menejimenti ya utumishi wa Umma
  • Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Boma Street, Mwanza Road

    Anuani: P.O.Box 320, Shinyanga

    Simu: +255 28 2762222

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras@shinyanga.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2018. Mkoa wa Shinyanga. Haki zote zimehifadhiwa