• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
    • eVibali |
Shinyanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Shinyanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Yetu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
      • Afya
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Shinyanga
    • Wilaya ya Kahama
    • Wilaya ya Kishapu
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu
    • Halmashauri ya Mji wa Kahama
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu
    • Halmashauri ya Wilaya ya Msalala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
    • Bandari Kavu
  • Huduma
    • Kutoa Ushauri wa Kitaalam
    • Kutafsiri Sheria na Sera
    • Kuratibu Shughuli za Wadau
    • Ulinzi na Usalama
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Tafiti
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha

HESHIMA YA ZAO LA PAMBA SASA KUREJEA KAMA ZAMANI - RC MACHA

Posted on: November 10th, 2024

Na. Paul Kasembo, KISHAPU.

MKUU wa Mkoa wa Shinyanga Mhe. Anamringi Macha amesema kuwa, heshima ya zao la pamba mkoani Shinyanga sasa inakwenda kurejea kama ilivyokuwa hapo zamani huku akiwasisitiza Maafisa Ugani Kilimo kuwa wabunifu zaidi, kutumia taaluma zao kuleta mapinduzi ya kweli na kwamba watapimwa utendaji kazi wao kupitia ongezeko la uzalishaji wa zao hili ambalo linatajwa kuwa zao muhimu la kibiashara ambapo kwa Shinyanga linazalishwa zaidi wilayani Kishapu.

RC Macha ameyasema haya leo tarehe 10 Novemba, 2024 katika semina elekezi kwa Maafisa Ugani Kilimo na Watendaji wa Kata wote iliyofanyika katika ukumbi wa mikutano uliopo Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu na kuhudhuriwa na viongozi mbalimbali wa Serikali na Chama akiwemo Mkuu wa Wilaya Mhe. Josph Mkude na Balozi wa Pamba nchini Ndugu Aggrey Mwanri na watalaam kutoka Bodi ya Pamba Kanda ya Ziwa.

"Nitumie nafasi kuwaeleza kuwa, heshima ya zao la pamba mkoani Shinyanga sasa inakwenda kurejea kama ilivyokuwa hapo zamani, lakini pia nanyi Maafisa Ugani Kilimo na Watendaji Kata mbadilike, muwe na uwezo wa kujiongeza, kuwa wabunifu na mtumie elimu yenu kuleta mabadiliko ya kweli na katika hili tutawapima kupitia uzalishaji wa zao hili," amesema RC Macha.

Kando na hili pia ametoa siku mbili (2) tarehe 10 - 11 Novemba, 2024 kwa wakulima wote wa zao la pamba kuhakikisha kuwa wanachoma wanang'oa na maoteo na masalia yote kabla ya kuanza msimu wa kilimo kwa mwaka huu wa 2024/2025 kqzi ambayo kwa mujibu wa sheria ya pamba na kanuni zake ilipaswa kutekelezwa kabla ya Septemba, 15..

Kwa upande wake Balozi wa Pamba ndg. Mwanri amesema kuwa, maotea na masalia katika zao pamba ni jambo ambalo halikubaliki kabisa kuachiwa liendelee, na ikitokea hivyo mkulima atazalisha pamba ambayo ni mapepe, isiyokuwa na ubora na ambayo ahikubaliki sokoni na hapo ndiyo malalamiko ya wakulima huanzia.

Ufuatiliaji, usimamizi na utekelezaji wa urejeshaji heshima ya zao la pamba mkoani Shinyanga ni sehemu ya mikakati ya RC Macha ya kuhakikisha kuwa zao hili muhimu la biashara mkoani Shinyanga maarufu kama (dhahabu nyeupe) linarejea kama zamani.

Matangazo

  • No records found
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • NATOA WITO KWA VIJANA HAPA SHINYANGA KUREJEA NA KUTATHIMINI UPYA NJIA ZA KUJIPATIA KIPATO - RC. MACHA

    May 20, 2025
  • SERIKALI YATHIBITISHA VIFO VYA WATU SITA NA MAJERUHI 11 KATIKA AJALI YA MGODI WA MWAKITOLYO.

    May 18, 2025
  • WAZAZI NA WALEZI, NENDENI MKAWE MABALOZI SAHIHI WA KAZI ZA MHE. RAIS DKT. SAMIA SULUHU HASSAN – RC. MACHA

    May 16, 2025
  • WAZAZI NA WALEZI WEKEZENI ZAIDI KATIKA MALEZI NA MAKUZI YA WATOTO – LYAMONGI

    May 15, 2025
  • Angalia zote

Video

MIFUKO BANDIA ZAIDI YA ELFU 20 YAKAMATWA SHINYANGA
Video Nyinginezo

Viunganishi vya Haraka

  • Historia
  • Dira na Dhima
  • Hotuba Mbalimbali
  • Video Mbalimbali
  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Picha za Matukio
  • Miongozo na kanuni

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Mfumo wa kutuma, kupokea na kufuatilia malalamiko, mapendekezo, maulizo na pongezi
  • Ofisi ya Rais Menejimenti ya utumishi wa Umma
  • Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Boma Street, Mwanza Road

    Anuani: P.O.Box 320, Shinyanga

    Simu: +255 28 2762222

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras@shinyanga.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2018. Mkoa wa Shinyanga. Haki zote zimehifadhiwa