• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
    • eVibali |
Shinyanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Shinyanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Yetu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
      • Afya
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Shinyanga
    • Wilaya ya Kahama
    • Wilaya ya Kishapu
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu
    • Halmashauri ya Mji wa Kahama
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu
    • Halmashauri ya Wilaya ya Msalala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
    • Bandari Kavu
  • Huduma
    • Kutoa Ushauri wa Kitaalam
    • Kutafsiri Sheria na Sera
    • Kuratibu Shughuli za Wadau
    • Ulinzi na Usalama
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Tafiti
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha

HONGERENI SANA MANISPAA YA SHINYANGA

Posted on: May 16th, 2024

RC MACHA AIPONGEZA SHINYANGA MC KUIBUKA KIDEDEA KATI YA MANISPAA ZOTE 19 NCHINI KWA USAFI


Na. Paul Kasembo, SHY RS.

MKUU wa Mkoa wa Shinyanga Mhe. Anamringi Macha ameipongeza Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga kwa kuibuka mshindi wa kwanza katika mashindano ya Afya na Usafi wa Mazingira yaliyohusisha Manispaa 19 Nchini huku akiwataka watumishi kuongeza kasi ya kuchapa kazi katika sekta zote ili kuweza kuyaisha na kutafisiri maono ya Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ya kuwatumikia Watanzania na kuwaletea maendeleo.

Pongezi hizi zimetolewa leo tarehe 16 Mei, 2024 na RC Macha alipokutana na Watumishi wa Manispaa ya Shinyanga kwa lengo la kutambuana na kukumbusha wajibu na majukumu ya kila mtumishi katika eneo lake la kazi ambapo pamoja na maelekezo mengine lakini pia amewataka watumishi kupendana, kushirikiana, kuwa wazalendo na kuyokubali kugawanywa kwa namna yoyote.

Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Shinyanga Mhe. Julius Mtatiro (Wakili) amemshukuru sana RC Macha kwa pongezi hizo za ushindi, lakini pia amempongeza kwa kazi nzuri anazozifanya katika kuwatumikia Wanshinyanga huku akimuahidi kuwa yale yote aliyoelekeza wanakwenda kuyatekeleza kwa weledi mkubwa na kuleta tija zaidi kwa wananchi wa Manispaa ya Shinyanga

Katika mashindano hayo, Manispaa.ya Shinyanga imeshinda na kuwa ya kwanza Kitaifa kwa kupata asilimia 95 ya alama zote zilizowekwa na Wizara ya Afya ikifuatiwa na Manispaa ya Moshi ambayo imepata asilimia 87 wakati nafasi ya tatu imechukuliwa na Manispaa ya Iringa ambayo imepata asilimia 83.

RC Macha anaendelea na ziara zake katika Halmashauri zote 6 zinazounda Mkoa wa Shinyanga ambapo kesho ni zamu ya Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga ambapo kuko pamoja na mambo mengine atakagua utekelezaji wa miradi ya maendeleo na baadae atazungumza na wananchi katika mkutano wa hadhara utakaofanyika Iselamagazi.

Matangazo

  • No records found
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • WANUFAIKA WA MIKOPO YA 10% LIPENI KWA WAKATI ILI PIA VIKOPESHWE NA VIKUNDI VINGINE - RC MACHA

    February 13, 2025
  • CP. HAMDUNI AKUTANA NA KAMATI YA MICHEZO YA JWTZ

    February 13, 2025
  • WANANCHI, LIPENI KODI YA ARDHI KWA WAKATI MUEPUKE RIBA - LEO KOMBA

    February 12, 2025
  • WAJUMBE WA BODI, TUMIENI TAALUMA ZENU KUISAIDIA HOSPITALI KUKAMILISHA MIRADI YA UJENZI- RAS CP. HAMDUNI.

    February 11, 2025
  • Angalia zote

Video

MIFUKO BANDIA ZAIDI YA ELFU 20 YAKAMATWA SHINYANGA
Video Nyinginezo

Viunganishi vya Haraka

  • Historia
  • Dira na Dhima
  • Hotuba Mbalimbali
  • Video Mbalimbali
  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Picha za Matukio
  • Miongozo na kanuni

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Mfumo wa kutuma, kupokea na kufuatilia malalamiko, mapendekezo, maulizo na pongezi
  • Ofisi ya Rais Menejimenti ya utumishi wa Umma
  • Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Boma Street, Mwanza Road

    Anuani: P.O.Box 320, Shinyanga

    Simu: +255 28 2762222

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras@shinyanga.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2018. Mkoa wa Shinyanga. Haki zote zimehifadhiwa