• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
    • eVibali |
Shinyanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Shinyanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Yetu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
      • Afya
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Shinyanga
    • Wilaya ya Kahama
    • Wilaya ya Kishapu
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu
    • Halmashauri ya Mji wa Kahama
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu
    • Halmashauri ya Wilaya ya Msalala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
    • Bandari Kavu
  • Huduma
    • Kutoa Ushauri wa Kitaalam
    • Kutafsiri Sheria na Sera
    • Kuratibu Shughuli za Wadau
    • Ulinzi na Usalama
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Tafiti
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha

Tunataka Hospitali za Umma ziwe sehemu ya Wananchi wote kutembelea - Dkt Chaula

Posted on: October 23rd, 2019

Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya, maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt Zainab Chaula amesema Hospitali za Umma zinatakiwa kuwa na mazingira mazuri ya kuwavutia wananchi kukimbilia kupata huduma.

Dkt. Chaula Ameyasema hayo mapema leo tarehe 23/10/2019 wakati wa ziara yake ya kazi Mkoani Shinyanga yenye lengo la kutembelea miradi ya maendeleo na kuzungumza na watumishi.

Dkt. Chaula amesema kuwa, iwapo hospitali za Umma zitakuwa na mazingira ya kuvutia kuanzia upande wa majengo hadi huduma hata watu wasioumwa watapenda kwenda kupata ushauri . "Hospitali zikiimarishwa katika suala zima la huduma na Afya na mambo yote, siyo lazima waje wagonjwa tu, tunataka hata watu wazima wasioumwa waje kupata huduma ya ushauri" 

Awali, akimkaribisha Dkt. Chaula, Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Mhe. Zainab Telack amemueleza kuwa, kazi kubwa imefanyika katika Serikali ya awamu ya tano hivyo kufanikisha kupunguza changamoto nyingi ikiwemo vifo vya akina mama na watoto kutokana na ongezeko la Vituo vya kutolea huduma za Afya.

" Shukrani kwa Mhe. Rais na watendaji wa Wizara ya Afya, Vituo vipo ni vizuri, wananchi wanavifurahia na vimejengwa kwa gharama nafuu kwa kutumia mafundi wetu" amesema Mhe. Telack.

Katika hatua nyingine Dkt. Chaula ameahidi kuhakikisha fedha iliyobaki kwa ajili ya kukamilisha Hospitali ya Rufaa ya Mkoa inapatikana ili ianze kutoa huduma ikiwemo kununua vifaa tiba na vitendea kazi vingine. 

Akizungumza na watumishi, katika Hospitali ya Mkoa wa Shinyanga Dkt. Chaula amewakumbusha kutekeleza majukumu yao na kuhakikisha wanawajibika kabla ya kudai haki. Amesisitiza pia wafanye kazi kwa pamoja kama timu moja lengo likiwa wananchi wanapata huduma.

Akiwa Mkoani Shinyanga, Dkt. Chaula ametembelea eneo la Mwawaza inapojengwa Hospitali mpya ya Rufaa ya Mkoa pamoja na kuzungumza na watumishi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa.



Matangazo

  • No records found
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • WANUFAIKA WA MIKOPO YA 10% LIPENI KWA WAKATI ILI PIA VIKOPESHWE NA VIKUNDI VINGINE - RC MACHA

    February 13, 2025
  • CP. HAMDUNI AKUTANA NA KAMATI YA MICHEZO YA JWTZ

    February 13, 2025
  • WANANCHI, LIPENI KODI YA ARDHI KWA WAKATI MUEPUKE RIBA - LEO KOMBA

    February 12, 2025
  • WAJUMBE WA BODI, TUMIENI TAALUMA ZENU KUISAIDIA HOSPITALI KUKAMILISHA MIRADI YA UJENZI- RAS CP. HAMDUNI.

    February 11, 2025
  • Angalia zote

Video

MIFUKO BANDIA ZAIDI YA ELFU 20 YAKAMATWA SHINYANGA
Video Nyinginezo

Viunganishi vya Haraka

  • Historia
  • Dira na Dhima
  • Hotuba Mbalimbali
  • Video Mbalimbali
  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Picha za Matukio
  • Miongozo na kanuni

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Mfumo wa kutuma, kupokea na kufuatilia malalamiko, mapendekezo, maulizo na pongezi
  • Ofisi ya Rais Menejimenti ya utumishi wa Umma
  • Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Boma Street, Mwanza Road

    Anuani: P.O.Box 320, Shinyanga

    Simu: +255 28 2762222

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras@shinyanga.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2018. Mkoa wa Shinyanga. Haki zote zimehifadhiwa