• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
    • eVibali |
Shinyanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Shinyanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Yetu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
      • Afya
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Shinyanga
    • Wilaya ya Kahama
    • Wilaya ya Kishapu
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu
    • Halmashauri ya Mji wa Kahama
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu
    • Halmashauri ya Wilaya ya Msalala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
    • Bandari Kavu
  • Huduma
    • Kutoa Ushauri wa Kitaalam
    • Kutafsiri Sheria na Sera
    • Kuratibu Shughuli za Wadau
    • Ulinzi na Usalama
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Tafiti
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha

Jamii yatakiwa kuwatunza wajawazito

Posted on: January 18th, 2019

Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Mhe. Zainab Telack amewataka wananchi kuwatunza wakina mama wajawazito ili kuhakikisha wanajifungua salama katika vituo vya kutolea huduma za afya.

Mhe. Telack ametoa wito huo wakati akizindua kampeni ya “Jiongeze tuwavushe salama” yenye lengo la kuzuia vifo vitokanavyo na uzazi leo katika ukumbi wa mikutano wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa.

Telack amesema kuwa, vifo vinavyotokana na uzazi bado ni tatizo katika Mkoa wa Shinyanga hivyo kila mmoja katika jamii awajibike ili kuwaepusha akina mama na watoto.

“Tukishikana, tukafanya pamoja, tutatoka pamoja katika kuwavusha akina mama na watoto wakiwa salama” amesema Mhe. Telack.

Amesema sababu nyingi ni za mzaha na uzembe, mila potofu, uelewa mdogo wa wananchi pamoja na lishe duni.

Awali akitoa taarifa ya vifo vitokanavyo na uzazi katika Mkoa wa Shinyanga, Katibu Tawala Msaidizi Sehemu ya Afya katika Sekretarieti ya Mkoa wa Shinyanga Dkt. Rashid Mfaume, amesema kuwa, vituo 9 vya afya vipo katika hatua ya kukamilika ili vianze kutoa huduma za dharura za uzazi, ambapo Serikali ametoa jumla ya sh. bilioni 3.9.

Aidha, Dkt. Mfaume amesema kuwa, Serikali pia ametoa sh. Bilioni 3. Kwa ajili ya ujenzi wa Hospitali mbili za Wilaya ya Ushetu na Shinyanga ili kupunguza tatizo la uhaba wa vituo vya Afya.

Kampeni hiyo ya Kitaifa iliyozinduliwa na Makamu wa Rais Mhe. Samia Suluhu, tarehe 6/11/2018 Mkoani Dodoma, inazinduliwa katika Mikoa yote nchini.

Matangazo

  • No records found
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • WANUFAIKA WA MIKOPO YA 10% LIPENI KWA WAKATI ILI PIA VIKOPESHWE NA VIKUNDI VINGINE - RC MACHA

    February 13, 2025
  • CP. HAMDUNI AKUTANA NA KAMATI YA MICHEZO YA JWTZ

    February 13, 2025
  • WANANCHI, LIPENI KODI YA ARDHI KWA WAKATI MUEPUKE RIBA - LEO KOMBA

    February 12, 2025
  • WAJUMBE WA BODI, TUMIENI TAALUMA ZENU KUISAIDIA HOSPITALI KUKAMILISHA MIRADI YA UJENZI- RAS CP. HAMDUNI.

    February 11, 2025
  • Angalia zote

Video

MIFUKO BANDIA ZAIDI YA ELFU 20 YAKAMATWA SHINYANGA
Video Nyinginezo

Viunganishi vya Haraka

  • Historia
  • Dira na Dhima
  • Hotuba Mbalimbali
  • Video Mbalimbali
  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Picha za Matukio
  • Miongozo na kanuni

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Mfumo wa kutuma, kupokea na kufuatilia malalamiko, mapendekezo, maulizo na pongezi
  • Ofisi ya Rais Menejimenti ya utumishi wa Umma
  • Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Boma Street, Mwanza Road

    Anuani: P.O.Box 320, Shinyanga

    Simu: +255 28 2762222

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras@shinyanga.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2018. Mkoa wa Shinyanga. Haki zote zimehifadhiwa