• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
    • eVibali |
Shinyanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Shinyanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Yetu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
      • Afya
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Shinyanga
    • Wilaya ya Kahama
    • Wilaya ya Kishapu
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu
    • Halmashauri ya Mji wa Kahama
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu
    • Halmashauri ya Wilaya ya Msalala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
    • Bandari Kavu
  • Huduma
    • Kutoa Ushauri wa Kitaalam
    • Kutafsiri Sheria na Sera
    • Kuratibu Shughuli za Wadau
    • Ulinzi na Usalama
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Tafiti
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha

KAHAMA YALINDA MIFUGO KWA KAMPENI KUBWA YA CHANJO NA UTAMBUZI

Posted on: October 9th, 2025

Katika kuhakikisha afya na ustawi wa mifugo, Halmashauri ya Manispaa ya Kahama kupitia Divisheni ya Kilimo, Mifugo na Ushirika, imezindua kampeni kabambe ya utoaji wa chanjo na utambuzi wa mifugo, hatua inayolenga kuinua kipato cha mfugaji na kuimarisha usalama wa chakula nchini.

Kampeni hiyo, iliyoanza rasmi tarehe 19 Agosti 2024, ni sehemu ya utekelezaji wa mkakati wa Kitaifa wa utoaji wa huduma muhimu kwa mifugo, na itatekelezwa kwa kipindi cha miaka mitano mfululizo hadi mwaka 2030.

Tayari, maelfu ya mifugo imepatiwa huduma muhimu huku wataalamu wa mifugo wakijipanga kuwafikia wafugaji wote nyumba kwa nyumba.

Miongoni mwa huduma zinazotolewa ni chanjo tatu muhimu ambazo ni Chanjo ya homa ya mapafu kwa ng’ombe ambapo mfugaji huchangia Shilingi 500 kwa kila ng’ombe; Chanjo ya sotoka kwa mbuzi na kondoo kwa kuchangia Shilingi 300 kwa mnyama na Chanjo ya kuku na bata mzinga inayotolewa bure kwa ajili ya kudhibiti milipuko ya magonjwa ya ndege.

Mpaka sasa, mafanikio makubwa yameripotiwa ambapo Ng’ombe 37,694, Mbuzi 4,215, Kondoo 513, Kuku 169,098 Bata mzinga 376 wamekwisha chanjwa.

Kwa ujumla, Kampeni hii si tu kwamba inalenga kupunguza vifo vya mifugo vinavyosababishwa na magonjwa, bali pia inalenga kuongeza tija kwa wafugaji, kuhakikisha mifugo ina afya bora na kuinua pato la familia kupitia uzalishaji ulioimarika.

Kwa Manispaa ya Kahama, huu ni mwanzo mpya wa mageuzi katika sekta ya mifugo na ni mfano halisi wa namna Serikali inavyoleta huduma karibu na wananchi kwa vitendo.

Mbali na chanjo, zoezi la utambuzi wa mifugo kwa kutumia hereni maalum linaendelea ambapo ng’ombe na punda huvalishwa hereni kubwa, huku mbuzi na kondoo wakivalishwa hereni ndogo. Utaratibu huu unasaidia kurahisisha ufuatiliaji wa afya, wizi wa mifugo, na kuweka kumbukumbu sahihi za mifugo katika maeneo yote ya Manispaa.

Kwa mujibu wa mtaalamu wa mifugo kutoka Manispaa hiyo Pendo Matulanya amesema ratiba maalum imewekwa ili kuwafikia wafugaji wote bila kuwaacha nyuma.

Lengo ni kuhakikisha kila mnyama anapatiwa huduma stahiki bila kujali yupo kijijini au pembezoni mwa mji.

Matangazo

  • No records found
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • RC MHITA AWAHAMASISHA WAFANYABIASHARA NA WAWEKEZAJI KUCHANGAMKIA FURSA ZA KIUCHUMI MKOANI SHINYANGA

    November 13, 2025
  • RC MHITA AKUTANA NA MSANII BANDO MC, APONGEZA JUHUDI ZA KUSAIDIA VIJANA SHINYANGA

    November 11, 2025
  • RC MHITA APONGEZA UONGOZI MPYA WA KANISA LA WASABATO NGBF MKOANI SHINYANGA.

    November 07, 2025
  • WANAFUNZI 29,193 KUFANYA MTIHANI WA UPIMAJI KIDATO CHA PILI SHINYANGA.

    November 07, 2025
  • Angalia zote

Video

RC MHITA AWAHAMASISHA WAFANYABIASHARA NA WAWEKEZAJI KUCHANGAMKIA FURSA ZA KIUCHUMI MKOANI SHINYANGA
Video Nyinginezo

Viunganishi vya Haraka

  • Historia
  • Dira na Dhima
  • Hotuba Mbalimbali
  • Video Mbalimbali
  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Picha za Matukio
  • Miongozo na kanuni

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Mfumo wa kutuma, kupokea na kufuatilia malalamiko, mapendekezo, maulizo na pongezi
  • Ofisi ya Rais Menejimenti ya utumishi wa Umma
  • Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    OFISI YA MKUU WA MKOA, MKOA WA SHINYANGA, 04 MTAA WA BOMA

    Anuani: P.O.Box 320, 37180,SHINYANGA, TANZANIA

    Simu: +255 28 2762222

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras@shinyanga.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2018. Mkoa wa Shinyanga. Haki zote zimehifadhiwa