• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
    • eVibali |
Shinyanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Shinyanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Yetu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
      • Afya
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Shinyanga
    • Wilaya ya Kahama
    • Wilaya ya Kishapu
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu
    • Halmashauri ya Mji wa Kahama
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu
    • Halmashauri ya Wilaya ya Msalala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
    • Bandari Kavu
  • Huduma
    • Kutoa Ushauri wa Kitaalam
    • Kutafsiri Sheria na Sera
    • Kuratibu Shughuli za Wadau
    • Ulinzi na Usalama
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Tafiti
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha

Kampeni ya "SHINYANGA MPYA MTI KWANZA" yazinduliwa

Posted on: September 25th, 2017

Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Mhe. Zainab Telack amezindua kampeni maalumu ya kupanda miti iliyopewa kauli mbiu ya "Shinyanga Mpya, Mti kwanza" yenye lengo la kuhakikisha Mkoa wa Shinyanga unakuwa na miti ili kuhifadhi mazingira na kurudisha hali ya Mkoa inayotishia kuwa jangwa.

Mhe. Telack amesema kuwa Mkoa wa Shinyanga ni kati ya maeneo yanayotajwa kuwa na jangwa, hivyo hali hiyo inayotaka kunyemelea na kuwa jangwa imesababishwa na wanashinyanga wenyewe.

"Jangwa linalotaka kunyemelea Mkoa wa Shinyanga tumelitengeneza sisi wenyewe, sasa tumeamua na kudhamiria, kwamba kwa mikono ileile ambayo ilitaka kuifanya Shinyanga iwe jangwa, sasa tuitumie kuhakikisha kwamba Shinyanga haiwi jangwa" 

"Sasa tumedhamiria kuona kwamba Shinyanga inakuwa ya kijani, na inakuwa ya kijani kwa sisi kutumia nguvu zetu, kwa sisi kutumia umoja tulionao kuhakikisha tunapanda miti hii na kuisimamia kwa umoja wetu"amesema Mhe. Telack.

Ameagiza kila mmoja awe mlinzi wa mti kwa kila taasisi, kila nyumba kila mfanya biashara atapewa mti wa kutunza na atakayeshindwa atapelekwa mahakamani. Amesema ili kusimamia lazima kuwe na kutaratibu wa kuitunza kwa kuanza na Manispaa na hatimaye Mkoa mzima.

Kuhusu mifugo inayotembea ovyo na kuharibu miti, amesema kuanzia leo mfugo yoyote utakaokamatwa unazagaa ovyo faini ni shilingi elfu 50 kwa kila mfugo.

Kampeni hiyo iliyohudhuriwa na makundi mbalimbali ya wananchi wa Manispaa ya Shinyanga imeelezwa kuwa itakuwa endelevu kwani kila Taasisi, mwananchi, wafanyabiashara itapewa jukumu la kutunza miti iliyo kwenye maeneo yao.

Awali, Mkuu wa Wilaya ya Shinyanga Mhe. Josephine Matiro amesema Kampeni hiyo ina lengo la kuhakikisha katika kila shughuli itakayofanyika lazima ianze kwa kupanda miti. 

Amesema barabara zote ndani na nje ya Manispaa zitapandwa miti katika pande zote, aidha, kila mwananchi apande mti katika eneo lake. Amewahimiza wananchi kuwa watunzaji wa miti hiyo.

Mhe. Matiro amesema kuna utarativu mzuri uliowekwa ili kuhakikisha miti hiyo inatunzwa hususani kuiwekea fito na kufunga chupa kwa ajili ya kunyunyizia maji ili kudhibiti mifugo haribifu pamoja na kuweka watu maalum ambao watahakikisha miti inakuwa katika barabara zisizokuwa makazi ya watu.


Matangazo

  • No records found
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • WANUFAIKA WA MIKOPO YA 10% LIPENI KWA WAKATI ILI PIA VIKOPESHWE NA VIKUNDI VINGINE - RC MACHA

    February 13, 2025
  • CP. HAMDUNI AKUTANA NA KAMATI YA MICHEZO YA JWTZ

    February 13, 2025
  • WANANCHI, LIPENI KODI YA ARDHI KWA WAKATI MUEPUKE RIBA - LEO KOMBA

    February 12, 2025
  • WAJUMBE WA BODI, TUMIENI TAALUMA ZENU KUISAIDIA HOSPITALI KUKAMILISHA MIRADI YA UJENZI- RAS CP. HAMDUNI.

    February 11, 2025
  • Angalia zote

Video

MIFUKO BANDIA ZAIDI YA ELFU 20 YAKAMATWA SHINYANGA
Video Nyinginezo

Viunganishi vya Haraka

  • Historia
  • Dira na Dhima
  • Hotuba Mbalimbali
  • Video Mbalimbali
  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Picha za Matukio
  • Miongozo na kanuni

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Mfumo wa kutuma, kupokea na kufuatilia malalamiko, mapendekezo, maulizo na pongezi
  • Ofisi ya Rais Menejimenti ya utumishi wa Umma
  • Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Boma Street, Mwanza Road

    Anuani: P.O.Box 320, Shinyanga

    Simu: +255 28 2762222

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras@shinyanga.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2018. Mkoa wa Shinyanga. Haki zote zimehifadhiwa