• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
    • eVibali |
Shinyanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Shinyanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Yetu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
      • Afya
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Shinyanga
    • Wilaya ya Kahama
    • Wilaya ya Kishapu
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu
    • Halmashauri ya Mji wa Kahama
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu
    • Halmashauri ya Wilaya ya Msalala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
    • Bandari Kavu
  • Huduma
    • Kutoa Ushauri wa Kitaalam
    • Kutafsiri Sheria na Sera
    • Kuratibu Shughuli za Wadau
    • Ulinzi na Usalama
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Tafiti
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha

Katibu Tawala Mkoa awahakikishia wananchi upatikanaji wa dawa Hospitalini

Posted on: August 22nd, 2017

Katibu Tawala Mkoa wa Shinyanga Bw. Albert Msovela amewahakikishia wananchi wa Mkoa wa Shinyanga uwepo wa dawa za kutosha kwenye Hospitali na vituo vya kutolea huduma za afya Mkoani hapa.

Akizungumza katika mkutano wa hadhara Mjini Shinyanga, Bw. Msovela amesema hivi sasa, upatikanaji wa dawa katika Hospitali zote ndani ya Mkoa ni asilimia 80.

Amewahimiza wananchi kujiunga kwa wingi na mfuko wa Bima ya afya iliyoboreshwa (CHF) ili kuepuka gharama kubwa za matibabu kwani kwa mwaka mzima kaya moja yenye watu sita wanatibiwa wote kwa kulipia shilingi 10,000/= tu.

Msovela amewataka wananchi kutoa taarifa kwake au kwa Mganga Mkuu wa Mkoa iwapo watapata changamoto yoyote katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa pamoja na Vituo vya huduma za Afya kuhusu dawa au matibabu.

Kuhusu uhaba wa watumishi katika vituo vya kutolea huduma, Msovela amesema suala la upatikanaji wa watumishi linashughulikiwa na Serikali na tayari imeshaanza kutoa vibali vya ajira katika nafasi mbalimbali kwa ngazi zote hivyo wananchi wategemee kuona watumishi wakiongezeka japo si kwa kasi wanavyotarajia.

Akifunga mkutano huo wa hadhara uliokuwa na lengo la kusikiliza kero za wananchi, Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Mhe. Zainab Telack amewataka wataalamu wote kuwasilisha taarifa za utekelezaji wa maagizo aliyoyatoa zikiwa zimekamilika.

Matangazo

  • No records found
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • WANUFAIKA WA MIKOPO YA 10% LIPENI KWA WAKATI ILI PIA VIKOPESHWE NA VIKUNDI VINGINE - RC MACHA

    February 13, 2025
  • CP. HAMDUNI AKUTANA NA KAMATI YA MICHEZO YA JWTZ

    February 13, 2025
  • WANANCHI, LIPENI KODI YA ARDHI KWA WAKATI MUEPUKE RIBA - LEO KOMBA

    February 12, 2025
  • WAJUMBE WA BODI, TUMIENI TAALUMA ZENU KUISAIDIA HOSPITALI KUKAMILISHA MIRADI YA UJENZI- RAS CP. HAMDUNI.

    February 11, 2025
  • Angalia zote

Video

MIFUKO BANDIA ZAIDI YA ELFU 20 YAKAMATWA SHINYANGA
Video Nyinginezo

Viunganishi vya Haraka

  • Historia
  • Dira na Dhima
  • Hotuba Mbalimbali
  • Video Mbalimbali
  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Picha za Matukio
  • Miongozo na kanuni

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Mfumo wa kutuma, kupokea na kufuatilia malalamiko, mapendekezo, maulizo na pongezi
  • Ofisi ya Rais Menejimenti ya utumishi wa Umma
  • Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Boma Street, Mwanza Road

    Anuani: P.O.Box 320, Shinyanga

    Simu: +255 28 2762222

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras@shinyanga.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2018. Mkoa wa Shinyanga. Haki zote zimehifadhiwa