• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
    • eVibali |
Shinyanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Shinyanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Yetu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
      • Afya
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Shinyanga
    • Wilaya ya Kahama
    • Wilaya ya Kishapu
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu
    • Halmashauri ya Mji wa Kahama
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu
    • Halmashauri ya Wilaya ya Msalala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
    • Bandari Kavu
  • Huduma
    • Kutoa Ushauri wa Kitaalam
    • Kutafsiri Sheria na Sera
    • Kuratibu Shughuli za Wadau
    • Ulinzi na Usalama
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Tafiti
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha

KIKAO KAZI CHA MMMAM CHAFANYIKA SHINYANGA, KUWEKA MIKAKATI MADHUBUTI YA MALEZI NA MAKUZI BORA KWA MTOTO

Posted on: August 20th, 2025

Kikao kazi cha uratibu wa utekelezaji wa Programu ya Malezi, Makuzi na Maendeleo ya Awali ya Mtoto (MMMAM) kimefanyika mkoani Shinyanga kikihusisha wadau kutoka sekta ya afya, lishe, ustawi wa jamii, maendeleo ya jamii, elimu pamoja na shirika la ICS ambalo ni mdau kinara wa malezi ya watoto.

Kikao hicho kilichofanyika katika Ukumbi wa Mikutano wa Hospitali ya Manispaa ya Shinyanga kimejadili kwa kina njia bora za kuhakikisha mtoto wa Kitanzania anapata msingi imara wa makuzi ya kimwili, kiakili, kihisia na kijamii tangu hatua za awali za maisha yake.

Miongoni mwa maazimio yaliyofikiwa ni kuhakikisha kila sekta inayohusika inakuwa na viashiria vya utekelezaji wa MMMAM ili kusaidia upatikanaji wa taarifa sahihi kwa kila robo mwaka. Pia, imependekezwa kuwa wataalamu wa sekta husika washiriki katika vikao vya kamati za wazazi na shule kwa lengo la kutoa elimu kuhusu malezi na makuzi kwa wazazi na walezi.

Aidha, kikao hicho kimehimiza kufanyika kwa vikao vya pamoja vya kupokea na kujadili taarifa za utekelezaji wa MMMAM kutoka kila sekta kwenye ngazi ya mkoa. Ufuatiliaji wa ubora wa chakula cha watoto mashuleni pia umepewa kipaumbele, hasa kuhakikisha unga unaotumika mashuleni umetengenezwa kwa kiwango cha kurutubishwa.

Akizungumza katika kikao hicho, Afisa Ustawi wa Jamii Mkoa wa Shinyanga, Lydia Kwesigabo, amesema kuwa utekelezaji wa programu hii ni hatua muhimu kwa watoto kupata nafasi ya kukua kwa utimilifu katika nyanja zote za maisha yao. Alieleza kuwa ushahidi wa kisayansi unaonesha kuwa uwekezaji wa mapema kwa watoto huleta mafanikio ya muda mrefu katika afya, elimu na maendeleo ya jamii.

MMMAM ni moja ya mikakati inayotekelezwa kitaifa ikiwa ni sehemu ya juhudi za serikali na wadau katika kujenga kizazi chenye afya bora, maarifa na uwezo wa kuchangia maendeleo ya taifa.

Matangazo

  • No records found
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • KIKAO KAZI CHA MMMAM CHAFANYIKA SHINYANGA, KUWEKA MIKAKATI MADHUBUTI YA MALEZI NA MAKUZI BORA KWA MTOTO

    August 20, 2025
  • WAMILIKI WA VITUO VYA KULELEA WATOTO MCHANA SHINYANGA WAASWA KUSAJILI VITUO VYAO ILI KUTOA HUDUMA SALAMA KWA WATOTO

    August 20, 2025
  • RC MBONI MHITA ATETA NA MANAIBU WAZIRI KUHUSU AJALI YA MGODI WA NYANDOLWA – ATANGAZA MAENDELEO YA ZOEZI LA UOKOAJI

    August 19, 2025
  • RC MBONI MHITA APONGEZA TUME YA UTUMISHI WA MAHAKAMA KWA KUIMARISHA MAADILI NA UWAJIBIKAJI KWA WATUMISHI.

    August 19, 2025
  • Angalia zote

Video

MIFUKO BANDIA ZAIDI YA ELFU 20 YAKAMATWA SHINYANGA
Video Nyinginezo

Viunganishi vya Haraka

  • Historia
  • Dira na Dhima
  • Hotuba Mbalimbali
  • Video Mbalimbali
  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Picha za Matukio
  • Miongozo na kanuni

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Mfumo wa kutuma, kupokea na kufuatilia malalamiko, mapendekezo, maulizo na pongezi
  • Ofisi ya Rais Menejimenti ya utumishi wa Umma
  • Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Boma Street, Mwanza Road

    Anuani: P.O.Box 320, Shinyanga

    Simu: +255 28 2762222

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras@shinyanga.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2018. Mkoa wa Shinyanga. Haki zote zimehifadhiwa