• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
    • eVibali |
Shinyanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Shinyanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Yetu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
      • Afya
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Shinyanga
    • Wilaya ya Kahama
    • Wilaya ya Kishapu
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu
    • Halmashauri ya Mji wa Kahama
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu
    • Halmashauri ya Wilaya ya Msalala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
    • Bandari Kavu
  • Huduma
    • Kutoa Ushauri wa Kitaalam
    • Kutafsiri Sheria na Sera
    • Kuratibu Shughuli za Wadau
    • Ulinzi na Usalama
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Tafiti
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha

KUANZIA SASA BWAWA LA MALENGE LISAJILIWE KWA JINA LA SHIJA - MHE. BASHE

Posted on: September 15th, 2024

ISAGEHE - KAHAMA.

WAZIRI wa Kilimo Mhe. Hussein Bashe ameiagiza Tume ya Umwagiliaji (NIRC) kuhakikisha mradi wa bwawa la umwagiliaji lililopo kijiji cha Malenge, Kata ya Isagehe wilayani Kahama lenye ukubwa wa mita za ujazo 600,000 na thamani ya Bil. 2.5 linajengwa unasajiliwa kwa jina la SHIJA  badala ya jina la awali la MALENGE.

Bashe ameyasema haya katika ziara yake wilayaninKahama ambapo pamoja na mambo mengine lakini pia amekagua mradi huu unaojengwa kwa ushirikiano kati ya Serikali na ufadhili wa Mgodi wa Barrick huku akimshukuru sana mzee Shija Lukinga ambaye awali alikuwa mmiliki wa eneo hilo na baadae kulitoa bure ili kupisha utekelezwaji wa mradi huu ambao unatajwa kuwa na tija zaidi kwa wakulima na wanamchi wa maeneo haya.

"Hii ni taswira na kipaji cha kipekee kabisa alichonacho mzee Shija cha kujitoa na kujitolea eneo lake ili kujengwa bwawa ambalo litawanufaisha wakulima takribani 427 na kuanzia sasa mradi huu usajiliwe kwa jina la SHIJA badala ya MALENGE kama ilivyokuwa ikisomeka awali," amesema Mhe. Bashe.

Aidha ameagiza kusakafiwa kwa mifereji yenye urefu wa kilometa 12 na kujenga  hekta 400 za tuta zilizobakia na kwamba wataalam wa ndani watumike katika kazi hizi za ujenzi wa bwawa, ghala na kinu.

Kando na hayo pia Bashe amemuomba Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Mhe. Anamringi Macha kufanya kikao vha ujirani mwema na Mkuu wa Mkoa wa Tabora ili Bonde la Manonga liweze kulindwa kwa ajili ya miundombinu ya uzalishaji wa chakula badala ya kujenga nyumba za makazi.

Kukamilika kwa usanifu uliolekezwa na Mhe. Bashe utawawezesha wakuli takribani 427 kunufaika na kilimo cha uhakika ambapo sasa wataweza kuvuna hadi mara tatu kwa mwaka.

Matangazo

  • No records found
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • KIKAO CHA MAPITIO YA ROBO MWAKA KWA KIPINDI CHA OKT - DES 2024 CHA (PJT MMMAM) CHAFANYIKA MKOANI SHINYANGA.

    February 28, 2025
  • RCC SHINYANGA YARIDHIA MAPENDEKEZO NANE (8) YA MATUMIZI BORA YA ARDHI.

    February 27, 2025
  • KUKAMILISHWA KWA MIRADI YA BARABARA KUTAPUNGUZA KERO KWA WANANCHI – RC MACHA

    February 26, 2025
  • WALIMU, TOENI ELIMU INAYOENDANA NA MABADILIKO YA TEKNOLOJIA -RC MACHA

    February 24, 2025
  • Angalia zote

Video

MIFUKO BANDIA ZAIDI YA ELFU 20 YAKAMATWA SHINYANGA
Video Nyinginezo

Viunganishi vya Haraka

  • Historia
  • Dira na Dhima
  • Hotuba Mbalimbali
  • Video Mbalimbali
  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Picha za Matukio
  • Miongozo na kanuni

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Mfumo wa kutuma, kupokea na kufuatilia malalamiko, mapendekezo, maulizo na pongezi
  • Ofisi ya Rais Menejimenti ya utumishi wa Umma
  • Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Boma Street, Mwanza Road

    Anuani: P.O.Box 320, Shinyanga

    Simu: +255 28 2762222

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras@shinyanga.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2018. Mkoa wa Shinyanga. Haki zote zimehifadhiwa