• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
    • eVibali |
Shinyanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Shinyanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Yetu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
      • Afya
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Shinyanga
    • Wilaya ya Kahama
    • Wilaya ya Kishapu
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu
    • Halmashauri ya Mji wa Kahama
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu
    • Halmashauri ya Wilaya ya Msalala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
    • Bandari Kavu
  • Huduma
    • Kutoa Ushauri wa Kitaalam
    • Kutafsiri Sheria na Sera
    • Kuratibu Shughuli za Wadau
    • Ulinzi na Usalama
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Tafiti
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha

KUKAMILISHWA KWA MIRADI YA BARABARA KUTAPUNGUZA KERO KWA WANANCHI – RC MACHA

Posted on: February 26th, 2025

Na. Paul Kasembo, SHY RS.

MKUU wa Mkoa wa Shinyanga Mhe. Anamringi Macha amesema kuwa kazi kubwa imefanywa na Serikali ili kuimarisha miundombinu ya barabara kwa Mkoa wa Shinyanga na nchi nzima kwani barabara nyingi zimefunguliwa na miradi mbalimbali ya miundombinu inaendelea kutekelezwa ambayo itakuwa na manufaa makubwa na hivyo kupunguza kero kwa wananchi.

RC Macha ameyasema haya leo Februari 26, 2025 akiwa kwenye kikao cha Bodi ya Barabara kilichofanyika kwenye Ukumbi wa Mikutano Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga ambapo pamoja na yote amewataka Wakala ya Barabara Tanzania (TANROAD) na Wakala ya Barabara Vijijini (TARURA) mkoani Shinyanga kuhakikisha kingo za barabara zinazojengwa kwa kiwango cha lami zinakamilishwa kwa ubora unaotakiwa.

“Serikali inayoongozwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan inaendelea kufanya kazi kubwa ili kuimarisha miundombinu ya barabara hapa mkoani Shinyanga na Nchi nzima kwa ujumla kwani mpaka sasa barabara nyingi zimefunguliwa maeneo mbalimbali, lakini pia miradi mbalimbali ya barabara inatekelezwa na itakuwa na manufaa makubwa sana kwa wananchi,” amesema RC Macha.

Akitolea mfano wa miundombinu inayotekelezwa mkoani Shinyanga, RC Macha amesema ujenzi wa barabara ya Kahama – Kakola pamoja na ujenzi wa madaraja Halmashauri ya Ushetu unaogharimu zaidi ya Tzs. Bilioni 18 ni vielelezo vikubwa vya utekelezaji wa Ilani ya Chama Cha Mapinduzi na miardi hii inategemewa kupunguza na kutatua kero za wananchi kuhusu miundombinu.

Aidha RC Macha amebainisha kuwa ujenzi wa barabara ya Ndala – Mwawaza inayoelekea Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Shinyanga yenye kilometa 4 inategemewa kupunguza kero kwa wananchi ambao wamekuwa wakihangaika kwa muda mrefu kutokana na ubovu wa barabara.

Kwa nyakati tofauti Kaimu Meneja wa TANROADS Mha. Joel Mwambungu na Kaimu Meneja wa TARURA Mha. Avith Theodory  wamekiri kupokea ushauri, maelekezo na mapendekezo ya Bodi na kwamba wanakwenda kuyafanyia kazi kwa hataka na kwa weledi zaidi ili Serikali iweze kufikia lengo la kuwaboreshea miundombinu wananchi.

Matangazo

  • No records found
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • KIKAO CHA MAPITIO YA ROBO MWAKA KWA KIPINDI CHA OKT - DES 2024 CHA (PJT MMMAM) CHAFANYIKA MKOANI SHINYANGA.

    February 28, 2025
  • RCC SHINYANGA YARIDHIA MAPENDEKEZO NANE (8) YA MATUMIZI BORA YA ARDHI.

    February 27, 2025
  • KUKAMILISHWA KWA MIRADI YA BARABARA KUTAPUNGUZA KERO KWA WANANCHI – RC MACHA

    February 26, 2025
  • WALIMU, TOENI ELIMU INAYOENDANA NA MABADILIKO YA TEKNOLOJIA -RC MACHA

    February 24, 2025
  • Angalia zote

Video

MIFUKO BANDIA ZAIDI YA ELFU 20 YAKAMATWA SHINYANGA
Video Nyinginezo

Viunganishi vya Haraka

  • Historia
  • Dira na Dhima
  • Hotuba Mbalimbali
  • Video Mbalimbali
  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Picha za Matukio
  • Miongozo na kanuni

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Mfumo wa kutuma, kupokea na kufuatilia malalamiko, mapendekezo, maulizo na pongezi
  • Ofisi ya Rais Menejimenti ya utumishi wa Umma
  • Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Boma Street, Mwanza Road

    Anuani: P.O.Box 320, Shinyanga

    Simu: +255 28 2762222

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras@shinyanga.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2018. Mkoa wa Shinyanga. Haki zote zimehifadhiwa