• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
    • eVibali |
Shinyanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Shinyanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Yetu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
      • Afya
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Shinyanga
    • Wilaya ya Kahama
    • Wilaya ya Kishapu
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu
    • Halmashauri ya Mji wa Kahama
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu
    • Halmashauri ya Wilaya ya Msalala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
    • Bandari Kavu
  • Huduma
    • Kutoa Ushauri wa Kitaalam
    • Kutafsiri Sheria na Sera
    • Kuratibu Shughuli za Wadau
    • Ulinzi na Usalama
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Tafiti
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha

Halmashauri zaagizwa kukamilisha ujenzi wa shule zinazoanzishwa na wananchi

Posted on: August 21st, 2019

Akizungumza na wananchi wa kijiji cha Lyamidati katika Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga mapema leo tarehe 21/08/2019, Makamu wa pili wa Rais wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar Mhe. Balozi Seif Ali Iddi, amezitaka Halmashauri nchini kuhakikisha zinakamilisha maboma yanayoanzishwa na wananchi ikiwemo shule ili kuwapunguzia umbali wanafunzi.

Mhe. Balozi akiwa kijijini hapo amekagua madarasa yaliyojengwa kwa fedha za mpango wa kuboresha Elimu (Equip – T) kwa lengo la kuwasaidia watoto wanaoanza darasa la kwanza kutotembea umbali wa kilometa 5 kufuata shule ya msingi, ambapo wananchi wa kijiji hicho wameamua kuchangia na kuongezea vyumba vinne vya madarasa na ofisi moja ili kujenga shule kamili.

Akisoma taarifa ya ujenzi wa madarasa hayo, Afisa Mtendaji wa kijiji Bw. Deus Maina, amesema kuwa gharama iliyotumika kutokana na nguvu ya wananchi, Serikali ya kijiji na mfuko wa Jimbo ni sh. 5,740,000. Aidha, fedha iliyotolewa na Equip –T ni sh. 6,600,000 pamoja na mfuko wa lipa kulingana na matokeo unaoitwa EP4R sh.12,500,000.

Katika taarifa hiyo, Afisa Mtendaji amesema fedha inayotakiwa kukamilisha ujenzi wa vyumba viwili vya madarasa pamoja na ofisi ili shule iweze kusajiliwa ni sh. Milioni 25.

Awali, Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Mhe. Zainab Telack amemtaka Mkurugenzi wa Halmashauri hiyo Bi. Hoja Mahiba kuangalia uwezekano wa kukamilisha shule hiyo kutokana na mapato ya ndani ya Halmashauri.

Matangazo

  • No records found
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • RC MHITA AZINDUA MPANGO WA KITAIFA WA UGAWAJI WA MBEGU BORA KWA WAKULIMA MSIMU WA 2025/2026

    October 23, 2025
  • SHINYANGA YAPAMBANA NA UKATILI WA KIJINSIA KWA NGUVU MPYA

    October 21, 2025
  • AFISA UTAMADUNI MKOA AKUTANA NA MAAFISA UTAMADUNI WA HALMASHAURI ZA MKOA WA SHINYANGA KUJADILI UBORESHAJI WA UKUSANYAJI MAPATO KUPITIA MAKTABA ZA VIDEO

    October 21, 2025
  • RC MHITA AKABIDHI MAGARI 5 MAPYA KWA JESHI LA ZIMAMOTO SHINYANGA, ASEMA YATASAIDIA KUOKOA MAISHA ZAIDI

    October 20, 2025
  • Angalia zote

Video

SHINYANGA IKO SALAMA, WANANCHI JITOKEZENI KUPIGA KURA KWA AMANI - RC MHITA
Video Nyinginezo

Viunganishi vya Haraka

  • Historia
  • Dira na Dhima
  • Hotuba Mbalimbali
  • Video Mbalimbali
  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Picha za Matukio
  • Miongozo na kanuni

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Mfumo wa kutuma, kupokea na kufuatilia malalamiko, mapendekezo, maulizo na pongezi
  • Ofisi ya Rais Menejimenti ya utumishi wa Umma
  • Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    OFISI YA MKUU WA MKOA, MKOA WA SHINYANGA, 04 MTAA WA BOMA

    Anuani: P.O.Box 320, 37180,SHINYANGA, TANZANIA

    Simu: +255 28 2762222

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras@shinyanga.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2018. Mkoa wa Shinyanga. Haki zote zimehifadhiwa