• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
    • eVibali |
Shinyanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Shinyanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Yetu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
      • Afya
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Shinyanga
    • Wilaya ya Kahama
    • Wilaya ya Kishapu
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu
    • Halmashauri ya Mji wa Kahama
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu
    • Halmashauri ya Wilaya ya Msalala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
    • Bandari Kavu
  • Huduma
    • Kutoa Ushauri wa Kitaalam
    • Kutafsiri Sheria na Sera
    • Kuratibu Shughuli za Wadau
    • Ulinzi na Usalama
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Tafiti
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha

Makazi ya Wazee kuhamishiwa TAMISEMI

Posted on: July 26th, 2017

Naibu Waziri wa Afya, Jinsia, Wazee, Wanawake na Watoto Mhe. Dkt. Hamis Kigwangala amemuagiza Katibu Mkuu wa Wizara hiyo Dkt. Sihaba Nkinga kukamilisha taratibu za kuhamisha makazi yote ya wazee nchini kuwa chini ya Ofisi ya Rais TAMISEMI ambayo kimsingi ndiyo yenye jukumu la kuendesha makazi ya wazee hao kwa sababu wako karibu kwa maana ya Mamlaka za Serikali za Mitaa. 

Mhe. Kigwangala ametoa agizo hilo hivi karibuni katika ziara yake ya siku moja Mkoani hapa ambapo ametembelea makazi ya wazee katika kambi ya Kolandoto, Manispaa ya Shinyanga.

Amesema, Wizara ya Afya itaendelea na jukumu la kutoa Sera na miongozo ya kuwahudumia Wazee hao na Mamlaka za Serikali za Mitaa yaani Halmashauri za Wilaya, Manispaa, Miji na Majiji ndiyo zenye jukumu la kuendesha makazi na vituo hivyo kwani ndiyo wako karibu na wazee.

Aidha, amemuelekeza Katibu Mkuu wa Afya awasiliane na Katibu Mkuu TAMISEMI ili kujenga vituo 10 kwenye Mikoa ambayo haina vituo vya Wazee, ikiwa ni hatua ya awali ya kila Mkoa kuwa na Makazi ya Wazee, ambapo hadi sasa kuna vituo 17 nchi nzima vyenye wazee 459.

Hata hivyo Mhe. Kigwangala amesema kuwa, kwa mujibu wa sera sehemu ya kwanza ya wazee kutunzwa ni ndani ya familia na Serikali huchukua jukumu hilo baada ya ngazi zote kushindwa kuwatunza, hivyo ametoa rai kwa wananchi wote kuhakikisha wanawatunza wazee kuanzia kwenye familia zao.

"Ni muhimu kuzingatia tamko la sera, kuwatunza ni jukumu la familia hivyo tusiwanyanyapae sababu ya umri wao, tuwashirikishe kwani ni tunu kubwa" amesisitiza Mhe. Kigwangala.

Kigwangala amewataka wananchi kukemea vitendo vya ukatili kwa wazee na kuondoa vikwazo vinavyowakosesha amani na kuwa, Serikali itaendelea kuchukua hatua kali kwa wale wote watakaobainika wanafanya vitendo vya ukatili kwa wazee.

Katika ziara hiyo, Mhe. Kigwangala ameweka jiwe la msingi ujenzi wa bweni la wazee ambalo litakuwa na uwezo wa kubeba wazee 20, amekabidhi bajaji itakayowasaidia wazee hao usafiri wa karibu pia amefungua jiko maalumu litakalotumika kupikia wazee likiwa na majiko ya gesi.


Matangazo

  • No records found
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • WANUFAIKA WA MIKOPO YA 10% LIPENI KWA WAKATI ILI PIA VIKOPESHWE NA VIKUNDI VINGINE - RC MACHA

    February 13, 2025
  • CP. HAMDUNI AKUTANA NA KAMATI YA MICHEZO YA JWTZ

    February 13, 2025
  • WANANCHI, LIPENI KODI YA ARDHI KWA WAKATI MUEPUKE RIBA - LEO KOMBA

    February 12, 2025
  • WAJUMBE WA BODI, TUMIENI TAALUMA ZENU KUISAIDIA HOSPITALI KUKAMILISHA MIRADI YA UJENZI- RAS CP. HAMDUNI.

    February 11, 2025
  • Angalia zote

Video

MIFUKO BANDIA ZAIDI YA ELFU 20 YAKAMATWA SHINYANGA
Video Nyinginezo

Viunganishi vya Haraka

  • Historia
  • Dira na Dhima
  • Hotuba Mbalimbali
  • Video Mbalimbali
  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Picha za Matukio
  • Miongozo na kanuni

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Mfumo wa kutuma, kupokea na kufuatilia malalamiko, mapendekezo, maulizo na pongezi
  • Ofisi ya Rais Menejimenti ya utumishi wa Umma
  • Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Boma Street, Mwanza Road

    Anuani: P.O.Box 320, Shinyanga

    Simu: +255 28 2762222

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras@shinyanga.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2018. Mkoa wa Shinyanga. Haki zote zimehifadhiwa