• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
    • eVibali |
Shinyanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Shinyanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Yetu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
      • Afya
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Shinyanga
    • Wilaya ya Kahama
    • Wilaya ya Kishapu
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu
    • Halmashauri ya Mji wa Kahama
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu
    • Halmashauri ya Wilaya ya Msalala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
    • Bandari Kavu
  • Huduma
    • Kutoa Ushauri wa Kitaalam
    • Kutafsiri Sheria na Sera
    • Kuratibu Shughuli za Wadau
    • Ulinzi na Usalama
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Tafiti
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha

MAKONDA AZINDUA RASMI WIKI YA MAADHIMISHO YA MIAKA 47 YA CCM

Posted on: January 28th, 2024

KATIBU wa Itikadi, Uenezi na Mafunzo CCM Taifa Ndugu Paul Makonda amezindua rasmi kitaifa wiki ya maadhimisho ya miaka 47 ya kuzaliwa kwa Chama Cha Mapinduzi akiwa katika viwanja vya Shule ya Msingi Town ambapo pia alikuwa akihitimisha ziara yake ya siku mbili ndani ya Mkoa wa Shinyanga.

Makonda amesema kuwa CCM inatimiza miaka 47 ya kuzaliwa kwake ambapo kuanzia leo tarehe 28 Januari, 2024 hadi tarehe 4 Februari, 2024 ndiyo mwisho wa wiki ya maadhimisho na tarehe 5 Februari, 2024 itakuwa kilele cha sherehe.

"Napenda kutumia fursa hii kutangaza rasmi kuwa leo hapa Manispaa ya Shinyanga hapa Mkoa wa Shinyanga, nazindua rasmi Wiki ya Maadhimisho ya Miaka 47 ya CCM yenye Kauli Mbiu Shiriki Uchaguzi kwa Uadilifu na Kazi Iendelee", alisema Makonda.

Kando na uzinduzi huu, Makonda pia amepata wasaa wa kuhutubia wananchi, kusikiliza na kutatua kero za wananchi ambapo pamoja na mamb9 mengine alisisitiza umuhimu wa watumishi wa umma kuwa waadilifu katika kuwahudumia wananchi ikiwa ni pamoja na kutumia vema lugha katika kuwajibu.

Aidha, Makonda amesema kuwa CCM haitambeba mtumishi yeyote mzembe, asiyekuwa muadilifu na asiekuwa na ambaye hatoi huduma bora kwa wananchi, CCM haitambeba mtumishi huyo, alisisitiza Makonda.

Mkutano huu unaofanyika viwanja vya Shule ya Msingi Town unahitimisha ziara ya siku mbili ya ndugu Makonda katika Mkoa wa shinyanga iliyoanza tarehe 27 hadi 28 Januari, 2024 ambapo amefika, kuhutubia, kusikiliza na kutatua kero katika Manispaa ya Kahama, Kata ya Segese iliyopo Halmashauri ya Msalala, Kata ya Kakola.

Na siku ya pili alianza na wananchi waliokuwepo Ofisi ya Mkuu wa Wilaya Kahama kisha akasimama Kata ya Kagongwa, Mwakata, Tinde na kisha hapa viwanja vya Shule ya Msingi Town Manispaa ya Shinyanga.


HABARI PICHA


Matangazo

  • No records found
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • WANUFAIKA WA MIKOPO YA 10% LIPENI KWA WAKATI ILI PIA VIKOPESHWE NA VIKUNDI VINGINE - RC MACHA

    February 13, 2025
  • CP. HAMDUNI AKUTANA NA KAMATI YA MICHEZO YA JWTZ

    February 13, 2025
  • WANANCHI, LIPENI KODI YA ARDHI KWA WAKATI MUEPUKE RIBA - LEO KOMBA

    February 12, 2025
  • WAJUMBE WA BODI, TUMIENI TAALUMA ZENU KUISAIDIA HOSPITALI KUKAMILISHA MIRADI YA UJENZI- RAS CP. HAMDUNI.

    February 11, 2025
  • Angalia zote

Video

MIFUKO BANDIA ZAIDI YA ELFU 20 YAKAMATWA SHINYANGA
Video Nyinginezo

Viunganishi vya Haraka

  • Historia
  • Dira na Dhima
  • Hotuba Mbalimbali
  • Video Mbalimbali
  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Picha za Matukio
  • Miongozo na kanuni

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Mfumo wa kutuma, kupokea na kufuatilia malalamiko, mapendekezo, maulizo na pongezi
  • Ofisi ya Rais Menejimenti ya utumishi wa Umma
  • Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Boma Street, Mwanza Road

    Anuani: P.O.Box 320, Shinyanga

    Simu: +255 28 2762222

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras@shinyanga.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2018. Mkoa wa Shinyanga. Haki zote zimehifadhiwa