• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
    • eVibali |
Shinyanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Shinyanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Yetu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
      • Afya
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Shinyanga
    • Wilaya ya Kahama
    • Wilaya ya Kishapu
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu
    • Halmashauri ya Mji wa Kahama
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu
    • Halmashauri ya Wilaya ya Msalala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
    • Bandari Kavu
  • Huduma
    • Kutoa Ushauri wa Kitaalam
    • Kutafsiri Sheria na Sera
    • Kuratibu Shughuli za Wadau
    • Ulinzi na Usalama
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Tafiti
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha

MFUMO WA AICBL WALETWA KUONGEZA UMAHIRI KWA WANAFUNZI- HANGO

Posted on: October 1st, 2025

Afisa Elimu wa Mkoa wa Shinyanga, Samson Allute Hango ambaye alikuwa mgeni rasmi katika uzinduzi wa mfumo wa Ujifunzaji wa Umahiri kwa Njia ya Sauti (AICBL), amesema Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inaendelea kuhitaji walimu wabunifu wanaobuni mbinu na zana zitakazowasaidia wanafunzi kuelewa kwa urahisi.

Amesisitiza kuwa ubunifu wa walimu ni nyenzo muhimu katika kuongeza umahiri wa wanafunzi na kuinua matokeo ya kielimu.

Uzinduzi huo umefanyika Septemba 30, 2025 katika Shule ya Sekondari ya Wavulana Shinyanga iliyoko Wilayani Kishapu, ambapo Hango amempongeza Mwalimu David Ipamba, Mratibu na Mbunifu wa maabara ya Jiografia shuleni hapo, pamoja na wanafunzi walioshiriki katika ubunifu huo.

Ameeleza kuwa ushirikiano baina ya walimu na wanafunzi ni msingi wa mafanikio ya kitaaluma, akitaja kuwa shule hiyo inapaswa kuwa mfano wa kuigwa kwa shule zote za Mkoa wa Shinyanga.

Mwl. David Ipamba ameeleza kuwa mfumo wa AICBL umeundwa kwa lengo la kutumia sauti, modeli, na mbinu za vitendo ili kujenga mazingira shirikishi ya ujifunzaji. Mfumo huo unawajengea wanafunzi uwezo wa kufikiri kwa kina, kubuni, na kujenga stadi za karne ya 21 kama vile ubunifu, mawasiliano na ushirikiano. AICBL pia inalenga kuwafikia wanafunzi wote, wakiwemo wenye mahitaji maalum, kupitia matumizi ya redio, simu, na vifaa vya TEHAMA.

Mwakilishi wa Afisa Elimu Sekondari Wilaya ya Kishapu, Moshi Moshi, amepongeza jitihada hizo na kutoa wito wa kuendelea kuboresha vifaa vya kufundishia na kujifunzia. Kwa upande wake, Mkuu wa Shule hiyo, Mwl. Bernard Ishengoma, amesema shule yao imejipanga kuongeza ubunifu, kusimamia nidhamu, na kuhakikisha kila mwanafunzi anashiriki kikamilifu katika masomo na shughuli za kuendeleza ujuzi.

Shule ya Sekondari ya Wavulana Shinyanga, iliyoanzishwa mwaka 1966, kwa sasa ina jumla ya wanafunzi 930 wakiwemo 118 wenye mahitaji maalum. Kupitia mfumo wa AICBL, shule hiyo inalenga kuwa kitovu cha ubunifu na ubora wa elimu si tu kwa Mkoa wa Shinyanga bali kwa Tanzania nzima.

Matangazo

  • No records found
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • RC MHITA AWAHAMASISHA WAFANYABIASHARA NA WAWEKEZAJI KUCHANGAMKIA FURSA ZA KIUCHUMI MKOANI SHINYANGA

    November 13, 2025
  • RC MHITA AKUTANA NA MSANII BANDO MC, APONGEZA JUHUDI ZA KUSAIDIA VIJANA SHINYANGA

    November 11, 2025
  • RC MHITA APONGEZA UONGOZI MPYA WA KANISA LA WASABATO NGBF MKOANI SHINYANGA.

    November 07, 2025
  • WANAFUNZI 29,193 KUFANYA MTIHANI WA UPIMAJI KIDATO CHA PILI SHINYANGA.

    November 07, 2025
  • Angalia zote

Video

RC MHITA AWAHAMASISHA WAFANYABIASHARA NA WAWEKEZAJI KUCHANGAMKIA FURSA ZA KIUCHUMI MKOANI SHINYANGA
Video Nyinginezo

Viunganishi vya Haraka

  • Historia
  • Dira na Dhima
  • Hotuba Mbalimbali
  • Video Mbalimbali
  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Picha za Matukio
  • Miongozo na kanuni

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Mfumo wa kutuma, kupokea na kufuatilia malalamiko, mapendekezo, maulizo na pongezi
  • Ofisi ya Rais Menejimenti ya utumishi wa Umma
  • Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    OFISI YA MKUU WA MKOA, MKOA WA SHINYANGA, 04 MTAA WA BOMA

    Anuani: P.O.Box 320, 37180,SHINYANGA, TANZANIA

    Simu: +255 28 2762222

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras@shinyanga.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2018. Mkoa wa Shinyanga. Haki zote zimehifadhiwa