• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
    • eVibali |
Shinyanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Shinyanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Yetu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
      • Afya
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Shinyanga
    • Wilaya ya Kahama
    • Wilaya ya Kishapu
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu
    • Halmashauri ya Mji wa Kahama
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu
    • Halmashauri ya Wilaya ya Msalala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
    • Bandari Kavu
  • Huduma
    • Kutoa Ushauri wa Kitaalam
    • Kutafsiri Sheria na Sera
    • Kuratibu Shughuli za Wadau
    • Ulinzi na Usalama
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Tafiti
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha

MHE. KUNDO AKIWA NA WATAALAM MBALIMBALI AMTEMBELEA RC MACHA

Posted on: July 29th, 2024

Na. Paul Kasembo, SHY RS.

NAIBU Waziri wa Maji Mhe. Eng. Mathew Kundo (MB) akiwa ameambatana na watalaam mbalimbali amemtembelea ofisini kwake Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Mhe. Anamringi Macha ambapo pamoja na mambo mengine pia amemueleza dhamira ya ziara yake mkoani Shinyanga ambapo ametembelea na kukagua mradi wa Maji ya Ziwa Victoria katika chanzo cha maji kilichopo Ihelele Wilaya ya Misungwi mkoani Mwanza.

Kisha baadae kukagua mradi wa maji unaotekelezwa na Wakala wa Maji na Usafi wa Mazingira Vijijini (RUWASA) wilayani Kishapu hapa Shinyanga ambapo pia alihutubia wananchi kupitia mkutano wa hadhara ambao ulihudhuriwa na Mbunge wa Jimbo la Kishapu Mhe. Boniphace Butondo na wataalam mbalimbali kutoka Wizara ya Maji na baadhi ya wakuu wa Taasisi kutoka Shinyanga.

"Nimefika hapa kukusalimu na kukueleza kuwa nimekuwa hapa tangu jana ambapo nimetembelea na kukagua miradi mbalimbali ukiwemo wa Maji ya Ziwa Victoria ambao unatekeleza shughuli zake kutoka katika chanzo cha maji cha Ihelele Mwanza na baadae nilifika Kishapu kwenye mradi wa RUWASA, kisha niliongea na wananchi kupitia mkutano wa hadhara pale Uchunga, na leo nitafanya kikao na watumishi wa Mamlaka za Maji hapo baadae," amesema Mhe. Kundo.

Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Mhe. Anamringi Macha amemueleza Mhe. Kundo kuwa, mradi wa maji ya Ziwa Victoria unaotoa huduma ya maji kwa Mamlaka nyingine za maji hapa Shinyanga unatekelezwa vema sana huku akieleza uwepi wa baadhi ya changamoto ambazo huikabili KASHWASA ikiwa ni pamoja na inapojitokeza changamoto za kiufundi na upungufu wa nishati ya umeme jambo ambalo hupelekea upungufu wa utoaji huduma ya maji kwa baadhi ya maeneo mkoani Shinyanga.

Pia RC Macha amezungumzia pia uwepo wa baadhi ya Taasisi ambazo zimekuwa zikilipa ankara kwa kusuasua jambo ambalo linakwamisha utoaji wa huduma tarajiwa kwa wananchi kwani zimekuwa na malimbikizo ya madeni ya muda mrefu huku akisema kuwa yeye mwenyewe amekwishachukua hatua kadhaa ikiwa ni pamoja na kuziita hizo taasisi na kuziagiza kulipa madeni hayo kwa wakati.

Matangazo

  • No records found
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • KIKAO CHA MAPITIO YA ROBO MWAKA KWA KIPINDI CHA OKT - DES 2024 CHA (PJT MMMAM) CHAFANYIKA MKOANI SHINYANGA.

    February 28, 2025
  • RCC SHINYANGA YARIDHIA MAPENDEKEZO NANE (8) YA MATUMIZI BORA YA ARDHI.

    February 27, 2025
  • KUKAMILISHWA KWA MIRADI YA BARABARA KUTAPUNGUZA KERO KWA WANANCHI – RC MACHA

    February 26, 2025
  • WALIMU, TOENI ELIMU INAYOENDANA NA MABADILIKO YA TEKNOLOJIA -RC MACHA

    February 24, 2025
  • Angalia zote

Video

MIFUKO BANDIA ZAIDI YA ELFU 20 YAKAMATWA SHINYANGA
Video Nyinginezo

Viunganishi vya Haraka

  • Historia
  • Dira na Dhima
  • Hotuba Mbalimbali
  • Video Mbalimbali
  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Picha za Matukio
  • Miongozo na kanuni

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Mfumo wa kutuma, kupokea na kufuatilia malalamiko, mapendekezo, maulizo na pongezi
  • Ofisi ya Rais Menejimenti ya utumishi wa Umma
  • Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Boma Street, Mwanza Road

    Anuani: P.O.Box 320, Shinyanga

    Simu: +255 28 2762222

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras@shinyanga.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2018. Mkoa wa Shinyanga. Haki zote zimehifadhiwa