• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
    • eVibali |
Shinyanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Shinyanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Yetu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
      • Afya
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Shinyanga
    • Wilaya ya Kahama
    • Wilaya ya Kishapu
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu
    • Halmashauri ya Mji wa Kahama
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu
    • Halmashauri ya Wilaya ya Msalala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
    • Bandari Kavu
  • Huduma
    • Kutoa Ushauri wa Kitaalam
    • Kutafsiri Sheria na Sera
    • Kuratibu Shughuli za Wadau
    • Ulinzi na Usalama
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Tafiti
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha

MHE. KUNDO ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MRADI WA MAJI YA ZIWA VICTORIA - IHELELE MWANZA

Posted on: July 28th, 2024

Na. Paul Kasembo, Ihelele Mwz.

NAIBU Waziri wa Maji Mhe. Eng. Mathew Kundo amesema kuwa ameridhishwa sana na utekelezaji wa Mradi wa Maji ya Ziwa Victoria ambao chanzo chake ni Ihelele Wilaya ya Misungwi mkoani Mwanza unaosimamiwa na Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Kahama Shinyanga (Kahama Shinyanga Water Supply and Sanitation Authority - KASHWASA) iliyopewa jukumu kuu la kuzalisha, kusambaza  na kuuza maji jumla kwa Mamlaka zingine zinazohusika na usambazaji wa maji kwa wananchi katika Mikoa 6 ikiwemo Shinyanga, Geita, Simiyu, Tabora, Mwanza na Singida.

Mhe. Kundo ameyasema haya alipotembelea na kukagua chanzo hiki cha maji ambacho kinatajwa kuwa mkombozi wa huduma ya maji ambacho kinawafikia wananchi katika maeneo mengi zaidi ya mijini na vijijini huku akimpongeza sana Mkurugenzi wa KASHWASA Mhandisi Patrick Nzamba kwa utekelezaji wake mzuri wa kazi yeye na wasaidizi wake ambao umekusudia kuhakikisha kuwa huduma ya maji inawafikia wananchi walio wengi huku akitolea mfano wa utiaji saini wa zaidi ya Bil 600 upelekaji maji Kishapu wilayani Kahama.

"Niwapongeze sana KASHWASA kwa kazi nzuri mnayoifanya ya kuwahudumia wananchi katika miji na vijiji kwa Mikoa 6, hii ni kazi nzuri sana kwa wananchi wetu na ndiyo maelekezo ya Serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ya kuhakikisha wananchi wote wanafikiwa na huduma ya maji safi na salama wakati wote. Na katika hili nitoe wito kwa wananchi wote kutunza vyanzo vyote vya maji pamoja na miundombinu yake ili iendelee kuwanufaisha na vizazi vijavyo," amesema na kusisitiza Mhe. Kundo.

Baadae Mhe. Kundo ametembelea Tangi kubwa la kuhifadhi maji lenye ujazo wa Lita Mil. 35 lililopo Mabale ambalo hutumika kupeleka maji katika maeneo yote yanayohudumiwa na KASHWASA huku Mhandisi Nzamba akisema kuwa chanzo cha Ihelele chenye uwezo wa kuzalisha maji Lita Mil. 80 kwa siku kinaouwezo wa kufanya kazi hiyo kwa ufanisi mkubwa zaidi na kukidhi mahitaji ya wananchi iwapo haitokei changamoto ya kiufundi au inayohusu nishati ya umeme.


HABARI PICHA


Matangazo

  • No records found
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • KIKAO CHA MAPITIO YA ROBO MWAKA KWA KIPINDI CHA OKT - DES 2024 CHA (PJT MMMAM) CHAFANYIKA MKOANI SHINYANGA.

    February 28, 2025
  • RCC SHINYANGA YARIDHIA MAPENDEKEZO NANE (8) YA MATUMIZI BORA YA ARDHI.

    February 27, 2025
  • KUKAMILISHWA KWA MIRADI YA BARABARA KUTAPUNGUZA KERO KWA WANANCHI – RC MACHA

    February 26, 2025
  • WALIMU, TOENI ELIMU INAYOENDANA NA MABADILIKO YA TEKNOLOJIA -RC MACHA

    February 24, 2025
  • Angalia zote

Video

MIFUKO BANDIA ZAIDI YA ELFU 20 YAKAMATWA SHINYANGA
Video Nyinginezo

Viunganishi vya Haraka

  • Historia
  • Dira na Dhima
  • Hotuba Mbalimbali
  • Video Mbalimbali
  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Picha za Matukio
  • Miongozo na kanuni

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Mfumo wa kutuma, kupokea na kufuatilia malalamiko, mapendekezo, maulizo na pongezi
  • Ofisi ya Rais Menejimenti ya utumishi wa Umma
  • Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Boma Street, Mwanza Road

    Anuani: P.O.Box 320, Shinyanga

    Simu: +255 28 2762222

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras@shinyanga.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2018. Mkoa wa Shinyanga. Haki zote zimehifadhiwa