• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
    • eVibali |
Shinyanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Shinyanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Yetu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
      • Afya
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Shinyanga
    • Wilaya ya Kahama
    • Wilaya ya Kishapu
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu
    • Halmashauri ya Mji wa Kahama
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu
    • Halmashauri ya Wilaya ya Msalala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
    • Bandari Kavu
  • Huduma
    • Kutoa Ushauri wa Kitaalam
    • Kutafsiri Sheria na Sera
    • Kuratibu Shughuli za Wadau
    • Ulinzi na Usalama
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Tafiti
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha

MHE. MNDEME AITAKA HALMASHAURI YA WILAYA YA SHINYANGA KUFIKISHA LENGO LA MAKUSANYO YA MAPATO KABLA YA MWAKA WA FEDHA KUISHA NA KUIMARISHA VYANZO VYA MAPATO

Posted on: June 23rd, 2023

Na.Shinyanga RS.

Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Mhe. Christina Solomon Mndeme ameshiriki Kikao Maalumu cha Baraza la Madiwani katika Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu ambacho kilihusisha ajenda ya taarifa ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG).

 

Baada ya kupokea taarifa na kumsikiliza (CAG) ilikabainika kuwa pamoja na kazi nzuri wanazofanya ikiwamo ya kujibu hoja lakini hawajafikisha asilimia 100 za lengo la makusanyo kwa mwaka unaoishia tarehe 30 Juni, 2023 hivyo akawaagiza kuhakikisha wanafikisha asilimia 100 kabla ya tarehe hiyo kwani Kishapu imefikisha 85% na Shinyanga DC ina 75% ya lengo la 100% ya mwaka 2022/2023.

“Sikubaliani kabisa na suala la kutofikishwa kwa lengo la makusanyo kwa mwaka 2022/2023, kwakuwa bado tumebakiwa na siku chache niwatake sasa kuhakikisha kuwa mnafikisha ili kuondokana na aibu ya kusomwa mbele ya Halmashauri nyingine ambazo zimefikisha. Aidha niwatake sasa muimarishe vyanzo vya mapato na kubuni vyanzo vingine sambamba na kudhibiti mianya ya upotevu wa fedha za umma ili tuweze kuwahudumia wananchi wetu,” alisema Mhe. Mndeme..

Kando na hayo, aliwapongeza sana wakurugenzi wa Halmashauri hizo, Ndg. Emmanuel Johnson wa Kishapu kwa kuendelea kuaminiwa na Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ili amsaidie kazi na pia kwa kuweza kujibu hoja 22 kati ya 54, na Ndg. Simon Berege kwa kuendelea kuaminiwa na Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ili amsaidie kazi katika Halmashauri ya Shinyanga na kwa kujibu hoja 90 kati ya 149 na nyingine zinazobakia zikiwa katika hatua mbalimbali za utekelezaji ili zifungwe.

Aidha aliwapongeza sana Wakuu wa Wilaya ya Kishapu Mhe. Joseph Mkude na Mhe. Johari Samizi wa Wilaya ya Shinyanga pamoja na Waheshimiwa Wenyeviti na Madiwani wa Halmashauri hizo kwa usimamizi mzuri na ushirikiano wao wakati wote na watumishi katika kutekeleza majukumu yao na hiyo ndiyo misingi mizuri ya kuwahudumia wananchi wetu.

Picha ikionesha sehemu ya Waheshimiwa Madiwani Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga wakiwa katika kika maalumu cha CAG

Sehemu ya picha ikionesha waheshimiwa madiwani wa Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu katika kikao cha CAG


Matangazo

  • No records found
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • KIKAO CHA MAPITIO YA ROBO MWAKA KWA KIPINDI CHA OKT - DES 2024 CHA (PJT MMMAM) CHAFANYIKA MKOANI SHINYANGA.

    February 28, 2025
  • RCC SHINYANGA YARIDHIA MAPENDEKEZO NANE (8) YA MATUMIZI BORA YA ARDHI.

    February 27, 2025
  • KUKAMILISHWA KWA MIRADI YA BARABARA KUTAPUNGUZA KERO KWA WANANCHI – RC MACHA

    February 26, 2025
  • WALIMU, TOENI ELIMU INAYOENDANA NA MABADILIKO YA TEKNOLOJIA -RC MACHA

    February 24, 2025
  • Angalia zote

Video

MIFUKO BANDIA ZAIDI YA ELFU 20 YAKAMATWA SHINYANGA
Video Nyinginezo

Viunganishi vya Haraka

  • Historia
  • Dira na Dhima
  • Hotuba Mbalimbali
  • Video Mbalimbali
  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Picha za Matukio
  • Miongozo na kanuni

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Mfumo wa kutuma, kupokea na kufuatilia malalamiko, mapendekezo, maulizo na pongezi
  • Ofisi ya Rais Menejimenti ya utumishi wa Umma
  • Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Boma Street, Mwanza Road

    Anuani: P.O.Box 320, Shinyanga

    Simu: +255 28 2762222

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras@shinyanga.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2018. Mkoa wa Shinyanga. Haki zote zimehifadhiwa