• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
    • eVibali |
Shinyanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Shinyanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Yetu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
      • Afya
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Shinyanga
    • Wilaya ya Kahama
    • Wilaya ya Kishapu
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu
    • Halmashauri ya Mji wa Kahama
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu
    • Halmashauri ya Wilaya ya Msalala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
    • Bandari Kavu
  • Huduma
    • Kutoa Ushauri wa Kitaalam
    • Kutafsiri Sheria na Sera
    • Kuratibu Shughuli za Wadau
    • Ulinzi na Usalama
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Tafiti
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha

MHE. SILAA APONGEZA UTEKELEZAJI WA BARAZA LA MAWAZIRI MKOA WA SHINYANGA

Posted on: December 4th, 2023

Na. Shinyanga RS

WAZIRI wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. Jerry Silaa (MB) leo tarehe 4 Desemba, 2023 amefika Mkoani Shinyanga na kufanya kikao na watumishi wa Sekta ya Ardhi ambapo pia alipewa taarifa ya Utekelezaji wa Maamuzi ya Baraza la Mawaziri Mkoa wa Shinyanga kuhusu utatuzi wa Migogoro ya matumizi ya ardhi katika vijiji 975, na kupongeza sana  namna ambavyo imetekelezwa.

Hayo yamesemwa leo na Mhe. Silaa katika ukumbi wa mikutano uliopo ofisi ya mkuu wa mkoa wa shinyanga na kuhudhuriwa na viongozi mbalimbali akiwemo mkuu wa mkoa wa shinyanga Mhe. Christina Mndeme, Katibu Tawala Mkoa wa Shinyanga Prof. Siza Tumbo, mkuu wa wilaya ya Kahama Mhe. Mboni Mhita.

Pia aliambatana na mwenyeviti wa Halmashauri ya wilaya ya shinyanga, viongozi wa Chama Cha Mapinduzi, Kamishna Msaidizi wa Ardhi Mkoa wa Shinyanga Ndg. Leo Komba, wakurugenzi wa Halmashauri zote na watumishi mbalimbali wa sekta ya ardhi huku akiwataka watumishi wote wa ardhi kubadilika katika utendaji kazi wao wa kila siku.

"Niwapongeze sana Mkoa wa Shinyanga kwa utekelezaji huu mzuri wa maelekezo ya Baraza la Mawaziri, mmefanya kazi nzuri sana hivyo ni wajibu wa sasa wa kila mtumishi wa sekta ya ardhi kubadilika katika utendaji kazi wa kila siku ili kusiwepo na kero za ardhi tena", alisema Mhe. Silaa.

Awali akimkaribisha Mhe. Silaa, Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Mhe. Christina Mndeme alisema kuwa ifike wakati sasa ardhi iwe ni baraka na siyo laana kwetu. Mhe. Mndeme aliendelea kumueleza Mhe. Silaa kuwa, mkoa wa shinyanga unaendeleaza utatuzi wa migogoro ya ardhi, kusimamia matumizi bora ya ardhi na kwenye ile migogoro mikubwa mkoa utaomba msaada kwake waziri mwenye dhamana ili aweze kusaidia.

Akitoa salamu za Halmashauri ya wilaya ya Shinyanga Mhe. Ngassa Mboje ambaye ni Mwenyekiti wa Halmashauri hiyo alisema, kumekuwa na baadhi ya migogoro sugu katika eneo la Nyanhwale na Halmashauri ya Wilaya ya Geita kupitia kijiji cha Chang'ombe ambapo Halmashauri ya Wilaya Geita wamekuwa wakidai ni eneo lao. Kufuatia malalamiko hayo Mhe. Silaa alimuelekeza Katibu Mkuu na Msajili wa Mabaraza kufika Shinyanga kutatua kero hizo.


HABARI PICHA


Matangazo

  • No records found
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • KIKAO CHA MAPITIO YA ROBO MWAKA KWA KIPINDI CHA OKT - DES 2024 CHA (PJT MMMAM) CHAFANYIKA MKOANI SHINYANGA.

    February 28, 2025
  • RCC SHINYANGA YARIDHIA MAPENDEKEZO NANE (8) YA MATUMIZI BORA YA ARDHI.

    February 27, 2025
  • KUKAMILISHWA KWA MIRADI YA BARABARA KUTAPUNGUZA KERO KWA WANANCHI – RC MACHA

    February 26, 2025
  • WALIMU, TOENI ELIMU INAYOENDANA NA MABADILIKO YA TEKNOLOJIA -RC MACHA

    February 24, 2025
  • Angalia zote

Video

MIFUKO BANDIA ZAIDI YA ELFU 20 YAKAMATWA SHINYANGA
Video Nyinginezo

Viunganishi vya Haraka

  • Historia
  • Dira na Dhima
  • Hotuba Mbalimbali
  • Video Mbalimbali
  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Picha za Matukio
  • Miongozo na kanuni

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Mfumo wa kutuma, kupokea na kufuatilia malalamiko, mapendekezo, maulizo na pongezi
  • Ofisi ya Rais Menejimenti ya utumishi wa Umma
  • Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Boma Street, Mwanza Road

    Anuani: P.O.Box 320, Shinyanga

    Simu: +255 28 2762222

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras@shinyanga.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2018. Mkoa wa Shinyanga. Haki zote zimehifadhiwa