• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
    • eVibali |
Shinyanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Shinyanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Yetu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
      • Afya
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Shinyanga
    • Wilaya ya Kahama
    • Wilaya ya Kishapu
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu
    • Halmashauri ya Mji wa Kahama
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu
    • Halmashauri ya Wilaya ya Msalala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
    • Bandari Kavu
  • Huduma
    • Kutoa Ushauri wa Kitaalam
    • Kutafsiri Sheria na Sera
    • Kuratibu Shughuli za Wadau
    • Ulinzi na Usalama
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Tafiti
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha

MKOA WA SHINYANGA KUNUFAIKA NA UMEME MKUBWA WA TEKNOLOJIA YA SOLAR PHOTO VOLTAIC

Posted on: May 29th, 2023

Na. Shinyanga RS.

Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) limesaini Mkataba wa kuzalisha UMEME WA JUA kwa kutumia Teknolojia ya SOLAR PHOTO VOLTAIC wenye uwezo wa kuzalisha MEGAWATI 150 ambapo itatekelezwa kwa awamu mbili, awamu ya kwanza megawati 50 na kisha megawati 100 utajengwa katika Kijiji cha Ngunga, Kata ya Talaga Wilaya ya Kishapu Mkoa wa Shinyanga mradi unaotajwa kuwa mkubwa zaidi kuwahi kutokea hapa nchini na katika Ukanda wa Afrika Mashariki.

Akizungumza mara baada ya kusaini mkataba huo, Waziri wa Nishati Mhe. January Makamba alisema kuwa kusainiwa kwa mradi huu ni sehemu ya mipango ya mapinduzi katika uzalishaji wa umeme kwa kutumia vyanzo mseto katika Sekta ya Nishati nchini ili kuweza kufikia lengo la kuwa na megawati 5000 kwenye Gridi ya Taifa ifikapo 2025.

Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Mhe. Christina Mndeme ambaye ndiye mwenyeji wa mradi huo katika Mkoa huo alimshukuru sana Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan Rais wa Jamhuri ya Munngano wa Tanzania, Wizara ya Nishati na Tanesco kwa kuwezesha utiaji saini wa mradi huo muhimu zaidi ambao utakwenda kuinufaisha Shinyanga kwa kuzalisha nishati, kuongeza ajira na kuimarisha uchumi wa wananchi kwa ujumla.

"Kwa niaba ya wananchi wa Mkoa wa Shinyanga, napenda kutoa shukurani zangu za dhati kabisa kipekee kwa Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan, Wizara ya Nishati na Tanesco kwa kuwesesha utiaji saini wa mkataba huu leo, hii ni furaha sana kwetu kwakuwa pamoja na kuzalisha umeme lakini pia mradi unakwenda kuongeza ajira na kuinua uchumi kwa wananchi wa Mkoa wa Shinyanga na pato la Taifa kwa ujumla," alisema Mhe. Mndeme.

Hafla ya utiaji saini wa mkataba wa kuzalisha umeme kwa teknolojia ya SOLAR PHOTO VOLTAIC imeongozwa na Waziri wa Nishati Mhe. January Makamba na kuhudhuriwa na viongozi mbalimbali akiwamo Mhe. Christina Mndeme ambaye ni Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, Kaimu Mwenyekiti Kamati ya Nishati na Madini ya Kudumu ya Bunge Mhe. Judith Kapinga, Mhe. Boniphace Butondo Mbunge Jimbo la Kishapu, wakandarasi kutoka Kampuni ya CHICO na wadau mbalimbali wa maendeleo.

Waziri wa Nishati Mhe. January Makamba akielezea jambo wakati wa utiaji saini wa mkataba

Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Mhe. Christina Mndeme akiongea jambo wakati wa utiaji saini

Picha ikionesha viongozi mbalimbali wakishuhudia utiaji saini wa mkataba wa uzalishaji wa umeme wa jua


Matangazo

  • No records found
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • ENDELEENI KUTOA ELIMU ZAIDI KUHUSU AFYA YA AKILI - DC. MBONI

    May 30, 2025
  • TAKUKURU SHINYANGA YAANZA KUCHUKUA HATUA DHIDI YA UBADHIRIFU WA SHILINGI MILIONI 92 ZA WAKULIMA WA TUMBAKU WA USHETU - DONASIAN.

    May 27, 2025
  • MAISHA BAADA YA KUSTAAFU YANAHITAJI UTULIVU - DC. MTATIRO

    May 26, 2025
  • MAFUNZO YA IPOSA NI MKOMBOZI KWA VIJANA WALIO WENGI WANAOKOSA FURSA YA ELIMU YA KAWAIDA - RC. MACHA

    May 23, 2025
  • Angalia zote

Video

MIFUKO BANDIA ZAIDI YA ELFU 20 YAKAMATWA SHINYANGA
Video Nyinginezo

Viunganishi vya Haraka

  • Historia
  • Dira na Dhima
  • Hotuba Mbalimbali
  • Video Mbalimbali
  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Picha za Matukio
  • Miongozo na kanuni

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Mfumo wa kutuma, kupokea na kufuatilia malalamiko, mapendekezo, maulizo na pongezi
  • Ofisi ya Rais Menejimenti ya utumishi wa Umma
  • Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Boma Street, Mwanza Road

    Anuani: P.O.Box 320, Shinyanga

    Simu: +255 28 2762222

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras@shinyanga.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2018. Mkoa wa Shinyanga. Haki zote zimehifadhiwa