Kiswahili
  • English
  • Kiswahili
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
    • eVibali |
Shinyanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Shinyanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Yetu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
      • Afya
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Shinyanga
    • Wilaya ya Kahama
    • Wilaya ya Kishapu
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu
    • Halmashauri ya Mji wa Kahama
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu
    • Halmashauri ya Wilaya ya Msalala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
    • Bandari Kavu
  • Huduma
    • Kutoa Ushauri wa Kitaalam
    • Kutafsiri Sheria na Sera
    • Kuratibu Shughuli za Wadau
    • Ulinzi na Usalama
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Tafiti
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha

MKOA WA SHINYANGA WAPOKEA MRADI WA KUONGEZA UPATIKANAJI NA MATUMIZI YA VYAKULA VILOVYOONGEZWA VIRUTUBISHI SHULENI

Posted on: May 19th, 2023

Na. Shinyanga RS.

Mkoa wa Shinyanga umepokea rasmi na kuanza kwa Mradi wa Kuongeza Upatikanaji wa Matumizi ya

Vyakula Vilivyoongezwa Virutubishi katika Shule na jamii kwa ujumla unaosimamiwa na kutekelezwa

kwa ushirikiano baina ya Serikali na Shirika lisilo la Kiserikali la GLOBAL ALLIANCE FOR IMPROVED

NUTRITION - GAIN, pamoja na Kampuni ya SANKU Project Healthy Children Ltd.

Akizungumza wakati wa kupokea mradi huo Katibu Tawala Wilaya ya Shinyanga Ndg. Boniphace Chambi

ambaye alimuwakilisha Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Mhe. Christina Mndeme alisema kwamba, Lishe ni

suala mtambuka sana.

Utapiamlo katika jamii ni matokeo ya mkusanyiko wa matatizo mengi sana ambayo yaweza

kusababishwa na Ulaji duni na mtindo wa maisha usiofaa, maradhi mbalimbali, kutokuwa na uhakika wa

chakula, matunzo duni ya mama na mtoto, mazingira machafu, rasilimali haba na mgawanyo wa

rasilimali usiokuwa na uwiano sahihi kijinsia, umasikini wa kipato, machafuko ya kisiasa na hata sera

zisizitambua umuhimu wa loshe kwa maendeleo ya mwanadamu na Taifa kqa ujumla.

"Ukifuatilia maelezo yangu hapo awali na ukatazma takwimu za afya kitaifa za hivi karibuni ambazo

zimebaini kuwa Mkoa wa Shinyanga unaasilimia 27.5 ya watoto walio Dumaa, na ndiyo sababu

kubwa ya kuwatafuta wenzetu GAIN na SANKU ilii kwa pamoja tuweze kushirikiana katika kutatua

mpja ya visababishi na kiwanho hiki cha udumavu katika Mkoa wetu ambapo itasaidia kupatikana

chakula kilichoongezwa virutubisho ambavyo ni Iron kwa ajili ya damu, madini ya Zinki kwa kinga ya

mwili na j8shipa ya damu, vitamini A na Foliki Asidi kwa ajili kusaidia uumbaji wa mtoto," alisema

Chambi.

Chambi kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa alitumia fulsa hiyo kuwaelekeza Wakuu wa Elimu kuwa 1.Vyakula

vyote vinavyotolewa mashuleni viwe na virutunisho tajwa, 2. Wazabuni wote kuzingatia maelekezo hayo

ya virutubisho, 3. Kamati/Bodi za shule ziteue wazabuni wenye vigezo kwa muibu wa sheria na

miongozo iliyopo, 4. Taasisi zote za Udhibiti Ubora zihakikishe usalama wa chakula na kufuatilia kwa

karibu kuepuka mafhara ambayo yaweza kutokea na kwa Mamlaka za Serikali za Mitaa na Wadau

kuendelea kuyoa elimu kwa jamii juu ya umuhimu wa virutubisho.

Kwa pande wake Ndg. Peter Kaja muwakilishi Wizara ya Afya Idara ya Kinga àlisema kuwa wapo hapa

Mkoa wa Shinyanga kwa ajili ya KUKABIDHI MRADI ikiwa ni moja wapo ya afua kama Wizara na

watekelezaji ambao ni TAMISEMI kwa kushirikiana na wadau ambao ni SANKU na GAIN baada ya

uzinduzi uliofanyika Wilaya ya Kahama mwezi Aprili, 2023 na leo unakabidhiwa rasmi hapa kwa niaba ya

Mikoa 6 ya Kanda ya Ziwa ambayo inashiriki na lengo ni kunufaisha wanafunzi 120,000 ikiwa ni shuke 40

kwa kila Mkoa.


Picha ya pamoja kwa washiriki wa mradi

Matangazo

  • No records found
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • KIKAO CHA MAPITIO YA ROBO MWAKA KWA KIPINDI CHA OKT - DES 2024 CHA (PJT MMMAM) CHAFANYIKA MKOANI SHINYANGA.

    February 28, 2025
  • RCC SHINYANGA YARIDHIA MAPENDEKEZO NANE (8) YA MATUMIZI BORA YA ARDHI.

    February 27, 2025
  • KUKAMILISHWA KWA MIRADI YA BARABARA KUTAPUNGUZA KERO KWA WANANCHI – RC MACHA

    February 26, 2025
  • WALIMU, TOENI ELIMU INAYOENDANA NA MABADILIKO YA TEKNOLOJIA -RC MACHA

    February 24, 2025
  • Angalia zote

Video

MIFUKO BANDIA ZAIDI YA ELFU 20 YAKAMATWA SHINYANGA
Video Nyinginezo

Viunganishi vya Haraka

  • Historia
  • Dira na Dhima
  • Hotuba Mbalimbali
  • Video Mbalimbali
  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Picha za Matukio
  • Miongozo na kanuni

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Mfumo wa kutuma, kupokea na kufuatilia malalamiko, mapendekezo, maulizo na pongezi
  • Ofisi ya Rais Menejimenti ya utumishi wa Umma
  • Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Boma Street, Mwanza Road

    Anuani: P.O.Box 320, Shinyanga

    Simu: +255 28 2762222

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras@shinyanga.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2018. Mkoa wa Shinyanga. Haki zote zimehifadhiwa