• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
    • eVibali |
Shinyanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Shinyanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Yetu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
      • Afya
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Shinyanga
    • Wilaya ya Kahama
    • Wilaya ya Kishapu
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu
    • Halmashauri ya Mji wa Kahama
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu
    • Halmashauri ya Wilaya ya Msalala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
    • Bandari Kavu
  • Huduma
    • Kutoa Ushauri wa Kitaalam
    • Kutafsiri Sheria na Sera
    • Kuratibu Shughuli za Wadau
    • Ulinzi na Usalama
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Tafiti
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha

RC Shinyanga aunda Kamati ya amani

Posted on: May 10th, 2018

Serikali Mkoani Shinyanga kwa kushirikiana na viongozi wa dini wameazimia kutokomeza mauaji yaliyoshamiri Mkoani hapa kutokana na sababu mbalimbali ikiwemo wivu wa kimapenzi na imani za kishirikina kwa kuunda Kamati maalumu ya Amani kwa lengo la kutoa elimu kwa wananchi.

Uamuzi huo umefikiwa mapema jana katika kikao cha pamoja cha viongozi hao kilichoitishwa na Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Mhe. Zainab Telack kwenye ukumbi wa Mikutano wa Ofisi yake.

Kamati hiyo yenye wajumbe kumi, inayohusisha viongozi wa dini wa pande zote imepewa jukumu la kutoa elimu kwa wananchi wa Mkoa wa Shinyanga ili kuisaidia jamii kuacha kuamini ushirikina, kuacha kujichukulia sheria mkononi pamoja na kuwajengea imani ya kumcha Mungu.

Awali akifungua kikao hicho, Mkuu wa Mkoa Mhe. Telack amesema hivi sasa uhalifu hususani mauaji yameshamiri Mkoani hapa hivyo Serikali imeona kuna haja ya kushirikisha na viongozi wa Dini ili wasaidie pia kusema na wananchi kwani ndiyo waamini wao kwenye nyumba za Ibada.

Mhe. Telack amesema anaamini Kamati hiyo itafanya vizuri katika kutoa elimu kwa wananchi na pia Serikali itatoa ushirikiano katika kila hatua.

Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa, SSP Lutusyo K. Mwakyusa akitoa taarifa ya uhalifu ya Mkoa kuanzia mwezi Januari - Aprili, 2018 amesema kuwa, tathmini inaonesha, makosa ya kero kwa jamii kama wizi yamepungua japokuwa mauaji kutokana na imani za kishirikina na wivu wa mapenzi zimeongezeka. Aidha, ametaja sababu nyingine za mauaji ni pamoja na ongezeko la migogoro ya ardhi, visasi kutokana na uhasama, wananchi kujichukulia sheria mkononi, uhaba au umbali wa upatikanaji wa huduma za afya.

Lutusyo amesema mauaji ya imani za kishirikina yameongezeka kwa asilimia 14 na kutokana wivu wa mapenzi yameongezeka kwa asilimia 11.4 na pia karibu asilimia 90 ya mauaji yanatokana na imani za kishirikina.

Matangazo

  • No records found
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • WANUFAIKA WA MIKOPO YA 10% LIPENI KWA WAKATI ILI PIA VIKOPESHWE NA VIKUNDI VINGINE - RC MACHA

    February 13, 2025
  • CP. HAMDUNI AKUTANA NA KAMATI YA MICHEZO YA JWTZ

    February 13, 2025
  • WANANCHI, LIPENI KODI YA ARDHI KWA WAKATI MUEPUKE RIBA - LEO KOMBA

    February 12, 2025
  • WAJUMBE WA BODI, TUMIENI TAALUMA ZENU KUISAIDIA HOSPITALI KUKAMILISHA MIRADI YA UJENZI- RAS CP. HAMDUNI.

    February 11, 2025
  • Angalia zote

Video

MIFUKO BANDIA ZAIDI YA ELFU 20 YAKAMATWA SHINYANGA
Video Nyinginezo

Viunganishi vya Haraka

  • Historia
  • Dira na Dhima
  • Hotuba Mbalimbali
  • Video Mbalimbali
  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Picha za Matukio
  • Miongozo na kanuni

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Mfumo wa kutuma, kupokea na kufuatilia malalamiko, mapendekezo, maulizo na pongezi
  • Ofisi ya Rais Menejimenti ya utumishi wa Umma
  • Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Boma Street, Mwanza Road

    Anuani: P.O.Box 320, Shinyanga

    Simu: +255 28 2762222

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras@shinyanga.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2018. Mkoa wa Shinyanga. Haki zote zimehifadhiwa