• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
    • eVibali |
Shinyanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Shinyanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Yetu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
      • Afya
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Shinyanga
    • Wilaya ya Kahama
    • Wilaya ya Kishapu
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu
    • Halmashauri ya Mji wa Kahama
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu
    • Halmashauri ya Wilaya ya Msalala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
    • Bandari Kavu
  • Huduma
    • Kutoa Ushauri wa Kitaalam
    • Kutafsiri Sheria na Sera
    • Kuratibu Shughuli za Wadau
    • Ulinzi na Usalama
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Tafiti
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha

WAZIRI LUKUVI ATEMBELEA MGODI WA NYANDOLWA, AFIKISHA MAELEKEZO YA RAIS SAMIA

Posted on: August 22nd, 2025

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu – Sera, Bunge na Uratibu, Mhe. William Lukuvi ametembelea Mgodi wa Nyandolwa uliopo katika Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga kufuatia ajali ya kutitia kwa mgodi huo, na kueleza kuridhishwa kwake na kasi ya jitihada za uokoaji zinazoendelea kufanywa na vyombo vya ulinzi na usalama kwa kushirikiana na wadau mbalimbali.

Kabla ya Waziri huyo kuzungumza na vyombo vya habari na wananchi waliokusanyika katika eneo la tukio, Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, Mhe. Mboni Mhita, alitoa taarifa fupi kuhusu hatua mbalimbali ambazo zimechukuliwa tangu kutokea kwa ajali hiyo. Alieleza kuwa kazi ya uokoaji inaendelea bila kuchoka na Serikali imehakikisha wahusika wote wa usalama na msaada wapo kazini muda wote kuhakikisha maisha yanaokolewa.

Katika ziara hiyo, Mhe. Lukuvi alieleza kuwa Serikali inafuatilia kwa karibu hali ya uokoaji na itaendelea kutoa misaada muhimu kwa familia za waathirika. Ametoa pole kwa familia zilizopoteza ndugu na kusema kuwa serikali imejipanga kugharamia mazishi, pamoja na kutoa usafiri kwa miili ya wale watakaopatikana wakiwa wamefariki dunia.

 Aidha, Mhe. Lukuvi amesema kuwa ziara yake ni sehemu ya utekelezaji wa maelekezo ya Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, aliyetoa agizo kuwa Serikali isimamie kwa karibu shughuli zote za uokoaji na kuhakikisha waathirika wanapatiwa msaada wa haraka, wa kutosha na wa kuwafariji.

"Serikali iko pamoja na wananchi katika kipindi hiki kigumu, na tutaendelea kuhakikisha kila juhudi inafanyika kuwaokoa mafundi waliokwama chini ya kifusi, sambamba na kuwapa faraja wahanga na familia zao," amesema Lukuvi.

Amewapongeza pia viongozi wa Mkoa wa Shinyanga wakiongozwa na RC Mhita kwa kusimamia kwa karibu shughuli za uokoaji, na kuhakikisha usalama na utulivu vinatawala katika eneo hilo la tukio.

Mpaka sasa jumla ya mafundi 11 wameopolewa, ambapo kati yao 8 wamepoteza maisha na 3 wakiwa hai, huku mafundi wengine 14 wakiendelea kutafutwa chini ya kifusi kufuatia ajali hiyo iliyotokea wakati wa shughuli za ukarabati wa mgodi huo zikiendelea.

Matangazo

  • No records found
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • AFISA UTAMADUNI MKUU AHITIMISHA SIKU YA NNE YA TAMASHA LA UTAMADUNI UKUNE, APONGEZA JUHUDI ZA KUHIFADHI MILA NA DESTURI ZA KISUKUMA.

    August 23, 2025
  • WAZIRI LUKUVI ATEMBELEA MGODI WA NYANDOLWA, AFIKISHA MAELEKEZO YA RAIS SAMIA

    August 22, 2025
  • MSANII MBOSSO AMTEMBELEA MKUU WA MKOA WA SHINYANGA OFISINI KWAKE.

    August 22, 2025
  • RC MHITA ATAKA KASI KUONGEZWA KWA UTOAJI VITAMBULISHO VYA WAFANYA BIASHARA,ARUHUSU SOKO LA IBINZAMATA KUTUMIKA KAMA GULIO.

    August 22, 2025
  • Angalia zote

Video

RC MHITA ALIVYOTOA KIBALI CHA KUTUMIKA KWA SOKO LA IBINZAMATA KUWA GULIO.... ASISITIZA ...
Video Nyinginezo

Viunganishi vya Haraka

  • Historia
  • Dira na Dhima
  • Hotuba Mbalimbali
  • Video Mbalimbali
  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Picha za Matukio
  • Miongozo na kanuni

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Mfumo wa kutuma, kupokea na kufuatilia malalamiko, mapendekezo, maulizo na pongezi
  • Ofisi ya Rais Menejimenti ya utumishi wa Umma
  • Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Boma Street, Mwanza Road

    Anuani: P.O.Box 320, Shinyanga

    Simu: +255 28 2762222

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras@shinyanga.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2018. Mkoa wa Shinyanga. Haki zote zimehifadhiwa