• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
    • eVibali |
Shinyanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Shinyanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Yetu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
      • Afya
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Shinyanga
    • Wilaya ya Kahama
    • Wilaya ya Kishapu
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu
    • Halmashauri ya Mji wa Kahama
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu
    • Halmashauri ya Wilaya ya Msalala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
    • Bandari Kavu
  • Huduma
    • Kutoa Ushauri wa Kitaalam
    • Kutafsiri Sheria na Sera
    • Kuratibu Shughuli za Wadau
    • Ulinzi na Usalama
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Tafiti
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha

MWAITEBELE AWATAKA WATUMISHI WA TRA MKOA WA SHINYANGA KUYAISHI MAADILI

Posted on: November 4th, 2023

Na. Shinyanga RC.

KATIBU Msaidizi, Ofisi ya Rais, Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma Kanda ya Magharibi Ndg Gerald Mwaitebele ametoa mafunzo haya kwa watumishi wa Mamlaka ya Mapato Tanzania-TRA Mkoa wa Shinyanga huku akiwataka kuanzia sasa kuyaishi maadili haya kwakuwa wao ni watumishi wa umma na kwamba ni kioo kwa umma wanaoutumikia.

Maelekezo haya yanetolewa leo na Mwaitebele katika ukumbi wa mikutano uliopo ofisi za mamlaka hii mbele ya watumishi wote huku akiwasisitiza kubadilisha tabia, matumizi mabaya ya lugha kwa wanaowahudumia, kuacha kuomba rushwa, kukopa bila kuoipa, kutoa siri za ofisi ili kuihujumu na badala yake wawe waadilifu ndani na nje ya ofisi kwakuwa wao ni viongozi wa umma.

"Kuanzia sasa tubadilishe mwenendo wetu, tubadili tabia zetu, matumizi ya lugha kwa tunaowahudumia ambao ndiyo umma, tuanze kuyaishi maadili kuanzia leo na tukumbuke kuwa sisi ni viongozi tunaotumikia umma hivyo tunatakiwa kuwa kioo mbele ya umma", alisema Mwaitebele.

Kando na hayo Mwaitebele alitaja miongoni mwa sifa na utambulisho wa mtumishi mwadilifu kwa umma ikiwemo na kujali wengine, kujitolea kusaidia wenye uhitaji, kuwa msikivu, mwaminifu nyakati zote na anayeheshimu kila mtu bila ubaguzi. Sifa nyingine ni pamoja na kuwa mnyenyekevu, kufanya kazi kwa bidii, kutenda haki, anapaswa kufikiria kwa makini kabla ya kutenda, kujizuia na tamaa ya aina yoyote na kuwa tayari na kukubali kukoselewa na kubadilika.

Misingi ya maadili katika Sekta ya umma ni muhimu sana ili kulinda maslahi ya umma na kukuza uwajibikaji kwa umma, sheria ya maadili ya viongozi wa umma, sheria ya utumishi wa umma pamoja na kanuni zake zimeanisha misinhi kadhaa ikiwemo Uadilifu, Haki ya kutopendelea, Kuheshimu sheria, kutopokea zawadi au fadhila kutoka kwa unayemuhudumia.

Awali akimkaribisha muwezeshaji, Meneja TRA Mkoa wa Shinyanga Ndg. Faustine C. Mdessa alisema kuwa wao kama watumishi na viongozi wa umma wapo tayari kupokea mafunzo ya maadili ya viongozi wa umma, wapo tayari kupokea maelekezo, miongozo na ushauri wote watakaopewa na kwamba kuanzia sasa wamebadilika na watayaishi.

Picha juu ikimuonesha Ndg. Gerald Mwaitebele, Katibu Msaidizi, Ofisi ya Rais, Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma, Kanda ya Magharibi akielezea jambo wakati wa mafunzo.

Picha juu ikimuonesha Ndg. Faustine Mdessa Meneja TRA Mkoa wa Shinyanga


Matangazo

  • No records found
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • WANUFAIKA WA MIKOPO YA 10% LIPENI KWA WAKATI ILI PIA VIKOPESHWE NA VIKUNDI VINGINE - RC MACHA

    February 13, 2025
  • CP. HAMDUNI AKUTANA NA KAMATI YA MICHEZO YA JWTZ

    February 13, 2025
  • WANANCHI, LIPENI KODI YA ARDHI KWA WAKATI MUEPUKE RIBA - LEO KOMBA

    February 12, 2025
  • WAJUMBE WA BODI, TUMIENI TAALUMA ZENU KUISAIDIA HOSPITALI KUKAMILISHA MIRADI YA UJENZI- RAS CP. HAMDUNI.

    February 11, 2025
  • Angalia zote

Video

MIFUKO BANDIA ZAIDI YA ELFU 20 YAKAMATWA SHINYANGA
Video Nyinginezo

Viunganishi vya Haraka

  • Historia
  • Dira na Dhima
  • Hotuba Mbalimbali
  • Video Mbalimbali
  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Picha za Matukio
  • Miongozo na kanuni

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Mfumo wa kutuma, kupokea na kufuatilia malalamiko, mapendekezo, maulizo na pongezi
  • Ofisi ya Rais Menejimenti ya utumishi wa Umma
  • Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Boma Street, Mwanza Road

    Anuani: P.O.Box 320, Shinyanga

    Simu: +255 28 2762222

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras@shinyanga.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2018. Mkoa wa Shinyanga. Haki zote zimehifadhiwa