• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
    • eVibali |
Shinyanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Shinyanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Yetu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
      • Afya
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Shinyanga
    • Wilaya ya Kahama
    • Wilaya ya Kishapu
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu
    • Halmashauri ya Mji wa Kahama
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu
    • Halmashauri ya Wilaya ya Msalala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
    • Bandari Kavu
  • Huduma
    • Kutoa Ushauri wa Kitaalam
    • Kutafsiri Sheria na Sera
    • Kuratibu Shughuli za Wadau
    • Ulinzi na Usalama
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Tafiti
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha

"Mwaka huu tunaingia mikataba ya kazi na Walimu" - RC Telack

Posted on: January 31st, 2020

Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Mhe. Zainab Telack amesema mwaka huu 2020 ataingia mkataba wa kazi na Waratibu wa Elimu kata ili kuweka mikakati ya kuhakikisha ufaulu mzuri katika mitihani ya Taifa ya darasa la saba na kidato cha nne.

Akizungumza katika kikao cha pamoja na Watendaji wa kata, Waratibu Elimu kata na Wakuu wa shule za msingi na sekondari wa Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu, Wilaya ya Kahama mapema leo tarehe 31/01/2020, Mhe. Telack amesema lengo la mikataba ni kuhakikisha kuwa kila mmoja anasimamia Elimu kikamilifu kwenye eneo lake ili kuongeza ufaulu.

"Mimi mwenyewe nitasaini Mikataba moja kwa moja na Waratibu Elimu kata nao watasaini na Wakuu wa shule pamoja na walimu, nataka kuona watoto wanatoka darasa la kwanza wanajua kusoma na kuandika, mjipangie mikakati ya kuondoa sifuri" amesema Telack.

Ili kufanikisha mkakati huo, Mhe. Telack amewataka Waratibu wa Elimu kata kuwasilisha kila mwezi taarifa ya maendeleo ya taaluma kwenye kila shule.

Aidha, amesema kuwa kuanzia mwezi Machi mwaka huu kila baada ya miezi miwili ifanyike mitihani ya kuwapima wanafunzi ili kubaini changamoto na kuzifanyia kazi.

Amesisitiza pia ni lazima kuhakikisha mitaala inakamilishwa ili wanafunzi wapate nafasi ya kufanya marudio kabla ya mtihani.

Telack amekemea tabia ya baadhi ya walimu kuwaachia wanafunzi kujisimamia ikiwemo kufuatlia mahudhurio yao wakati walimu wa madarasa wapo. "Walimu tumefikia pabaya, walimu wa madarasa hawafanyi kazi yao, sitaki kusikia"

Katibu Tawala Msaidizi sehemu ya Elimu ambaye ni Afisa Elimu Mkoa, Bw. Mohamed Kahundi amewataka wasimamizi wote Elimu Mkoani hapa kufuata miongozo na maelekezo ya Wizara ya Elimu katika kuandaa ratiba za vipindi ili kukamilisha mitaala.

"Tusibadilishe miongozo na melekezo ya Wizara katika kuandaa vipindi" amesema Kahundi.

Wakati huo huo, Mkuu wa Mkoa amewapa siku tatu Wakuu wote wa shule za msingi na sekondari Mkoani hapa kukarabati madawati, viti na meza kwa fedha ya ukarabati inayoletwa na Serikali kila mwezi.

Katibu Tawala Mkoa wa Shinyanga Bw. Albert Msovela akizungumza na watendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu kabla ya kumkaribisha Mkuu wa Mkoa Mhe. Zainab Telack, kushoto ni Mkuu wa Wilaya ya Kahama Annamringi Macha na kulia ni Afisa Elimu Sekondari wa Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu

Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Mhe. Zainab Telack akizungumza na Maafisa Elimu kata, Watendaji wa kata na Wakuu wa shule za msingi na sekondari(hawapo pichani) wa Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu

Katibu Tawala Msaidizi Sehemu ya Elimu, ambaye ni Afisa Elimu Mkoa wa Shinyanga Bw. Mohamed Kahundi akitoa mwongozo wa Wizara ya Elimu kuhusu upangaji wa vipindi shuleni katika kikao hicho

Baadhi ya washiriki wa kikao hicho wakimsikiliza Mkuu wa Mkoa katika kikao hicho

Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Mhe. Zainab Telack akiwa darasani katika shule ya msingi Ukune, Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu akifuatilia ufundishaji na ujifunzaji wa wanafunzi, kulia ni Katibu Tawala Mkoa Bw. Albert Msovela

Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Mhe. Zainab Telack akiagiza kukarabatiwa kwa viti na meza katika shule ya sekondari Ukune, Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu 


Matangazo

  • No records found
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • WANUFAIKA WA MIKOPO YA 10% LIPENI KWA WAKATI ILI PIA VIKOPESHWE NA VIKUNDI VINGINE - RC MACHA

    February 13, 2025
  • CP. HAMDUNI AKUTANA NA KAMATI YA MICHEZO YA JWTZ

    February 13, 2025
  • WANANCHI, LIPENI KODI YA ARDHI KWA WAKATI MUEPUKE RIBA - LEO KOMBA

    February 12, 2025
  • WAJUMBE WA BODI, TUMIENI TAALUMA ZENU KUISAIDIA HOSPITALI KUKAMILISHA MIRADI YA UJENZI- RAS CP. HAMDUNI.

    February 11, 2025
  • Angalia zote

Video

MIFUKO BANDIA ZAIDI YA ELFU 20 YAKAMATWA SHINYANGA
Video Nyinginezo

Viunganishi vya Haraka

  • Historia
  • Dira na Dhima
  • Hotuba Mbalimbali
  • Video Mbalimbali
  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Picha za Matukio
  • Miongozo na kanuni

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Mfumo wa kutuma, kupokea na kufuatilia malalamiko, mapendekezo, maulizo na pongezi
  • Ofisi ya Rais Menejimenti ya utumishi wa Umma
  • Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Boma Street, Mwanza Road

    Anuani: P.O.Box 320, Shinyanga

    Simu: +255 28 2762222

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras@shinyanga.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2018. Mkoa wa Shinyanga. Haki zote zimehifadhiwa