• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
    • eVibali |
Shinyanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Shinyanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Yetu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
      • Afya
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Shinyanga
    • Wilaya ya Kahama
    • Wilaya ya Kishapu
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu
    • Halmashauri ya Mji wa Kahama
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu
    • Halmashauri ya Wilaya ya Msalala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
    • Bandari Kavu
  • Huduma
    • Kutoa Ushauri wa Kitaalam
    • Kutafsiri Sheria na Sera
    • Kuratibu Shughuli za Wadau
    • Ulinzi na Usalama
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Tafiti
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha

MWENGE WA UHURU WAWEKA JIWE LA MSINGI OFISI YA MACHINGA - NYAMILANGANO

Posted on: August 14th, 2024

Na. Paul Kasembo, USHETU.

MWENGE wa Uhuru umeweka Jiwe la Msingi mradi wa ujenzi wa Ofisi ya Machinga iliyopo Nyamilangano katika Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu huku kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa ndg. Eliakim Mnzava akimpongeza Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Ushetu Bi. Hadija Kabojela kwa utekelezaji wa mradi huu mzuri wenye lengo la kuwawezesha Machinga kuwa na ofisi yao ukizingatia kuwa hili ni kundi kubwa sana linalojumuisha na bodaboda.

Haya yamesemwa leo tarehe 14 Agosti, 2024 na Mnzava wakati wa ukaguzi na kutembelea jumla ya miradi 7 ya Halmashauri ya Ushetu mradi ambao umegharimu zaidi ya Tzs. 47 ambapo pamoja na mambo mengine lakini pia kulifanyika zoezi la uteketezaji wa madawa ya kulevya aina ga bangi yenye uzito wa Kg. 34 huku ndg. Mnzava akitoa wito kwa wananchi kuwa na malezi mema zaidi kwa vijana wetu kundi ambalo limetajwa kuwa wahanga wakubwa wa madawa ya kjlevya

"Nawapongeza sana Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu kwa kazi nzuri ya utekelezaji wa mradi huu wa ujenzi wa ofisi ya machinga pamoja na bodaboda, ni mradi mzuri sana wenye tija kubwa ukizingatia kuwa hili kundi kubwa sana amnalo limejiajiri na kupata uungaji mkono mkubwa wa Serikali, hivyo kukamilika kwa ofisi hii kunakwenda kuwaongezea hadhi zaidi," amesema Mnzava.

Mwenge wa Uhuru ukiwa katika Halmashauri ya Wilaya Ushetu umekimbizwa kilomita 123, umeifikia miradi ya maendeleo 7 yenye jumla ya zaidi ya Tzs. Bilioni 2.8 huku miradi yote ikipitishwa bila kukwama baada ya Mwenge wa Uhuru kuridhishwa na utekelezaji wake na hivo kuifanya Halmashauri iliyo chini ya Wilaya ya Kahama na ambayo inaongozwa na Mkuu wa Wilaya ya Kahama Mhe. Mboni Mhita na Mkurugenzi wake Bi. Hadija Kabojela kung'ara zaidi.

Miradi iliyofikiwa ni pamoja na Ujenzi wa vyumba vya madarasa 5 Shule ya Msingi Ukune ambapo ilikuwa ni kuzindua, Mradi wa barabara km 1.05 kiwango cha lami na kuwekewa Jiwe la msingi Nyamilangano, ujenzi wa ofisi ya machinga na bodaboda na kuwekewa Jiwe la Msingi Nyamilangano, ujenzi wa bweni la wanafunzi wenye mahitaji maalum na kuwekewa jiwe la msningi,mradi wa mazingira, CTC na RUWASA.


Matangazo

  • No records found
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • KIKAO CHA MAPITIO YA ROBO MWAKA KWA KIPINDI CHA OKT - DES 2024 CHA (PJT MMMAM) CHAFANYIKA MKOANI SHINYANGA.

    February 28, 2025
  • RCC SHINYANGA YARIDHIA MAPENDEKEZO NANE (8) YA MATUMIZI BORA YA ARDHI.

    February 27, 2025
  • KUKAMILISHWA KWA MIRADI YA BARABARA KUTAPUNGUZA KERO KWA WANANCHI – RC MACHA

    February 26, 2025
  • WALIMU, TOENI ELIMU INAYOENDANA NA MABADILIKO YA TEKNOLOJIA -RC MACHA

    February 24, 2025
  • Angalia zote

Video

MIFUKO BANDIA ZAIDI YA ELFU 20 YAKAMATWA SHINYANGA
Video Nyinginezo

Viunganishi vya Haraka

  • Historia
  • Dira na Dhima
  • Hotuba Mbalimbali
  • Video Mbalimbali
  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Picha za Matukio
  • Miongozo na kanuni

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Mfumo wa kutuma, kupokea na kufuatilia malalamiko, mapendekezo, maulizo na pongezi
  • Ofisi ya Rais Menejimenti ya utumishi wa Umma
  • Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Boma Street, Mwanza Road

    Anuani: P.O.Box 320, Shinyanga

    Simu: +255 28 2762222

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras@shinyanga.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2018. Mkoa wa Shinyanga. Haki zote zimehifadhiwa