Kiswahili
  • English
  • Kiswahili
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
    • eVibali |
Shinyanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Shinyanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Yetu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
      • Afya
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Shinyanga
    • Wilaya ya Kahama
    • Wilaya ya Kishapu
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu
    • Halmashauri ya Mji wa Kahama
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu
    • Halmashauri ya Wilaya ya Msalala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
    • Bandari Kavu
  • Huduma
    • Kutoa Ushauri wa Kitaalam
    • Kutafsiri Sheria na Sera
    • Kuratibu Shughuli za Wadau
    • Ulinzi na Usalama
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Tafiti
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha

NASHAURI, ELIMU YA MLIPA KODI IANZE KUFUNDISHWA KATIKA SHULE ZETU NA IRASIMISHWE - DC MTATIRO.

Posted on: January 17th, 2025

Na. Paul Kasembo, SHY RS.

Mwakilishi wa Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga ambaye pia ni Mkuu wa Wilaya ya Shinyanga Mhe. Julius Mtatiro (Wakili) ameshauri kuwepo na mpango wa muda mrefu katika utoaji wa elimu ya mlipa kodi huku akisisitiza juu ya umuhimu wa kuanzisha utaratibu wa kuanza kufundishwa katika shule zetu na kuirasimisha lengo ni kuwajengea uelewa kuhusu elimu ya mlipa kodi huku njia hii ikitajwa kuleta mapinduzi ya uzalendo na uelewa kwa jamii na hasa walipa kodi wa Taifa letu.

Mhe. Mtatiro ameyasema haya leo tarehe 17 Januari, 2025 wakati akifungua mkutano wa Tume ya Rais ya Kukusanya Maoni ya Maboresho ya Kodi ambayo kwa Mkoa wa Shinyanga uliongozwa na CPA. Leonard Mususa ambaye alimwakilisha Mwenyekiti wa Bodi Balozi. Ombeni Sefue ambapo pamoja na mambo mengine amewaongoza wadau katika zoezi la ukusanyaji maoni hayo, mkutano huu umehudhuriwa na viongozi mbalimbali akiwemo Davil Lyamongi aliyemwakilisha Katibu Tawala Mkoa wa Shinyanga CP. Salum Hamduni.

"Pamoja na pongezi kwa kazi nzuri, naomba nitoe ushauri wangu, kuanzishwe utaratibu wa kufundisha somo la kodi katika shule zetu na lirasimishwe kwenye mitaala yetu ili watakapohitimu watakuwa wamejengeka katika uzalendo na uelewa mkubwa juu ya ulipaji kodi jambo ambalo litapelekea ongezeko kubwa la pato, na hili liwe ni sehemu ya utekelezaji wa mpango wa utoaji elimu wa muda mrefu," amesema Wakili Mhe. Mtatiro.

Akitoa salamu za Tume, CPA. Leonard alisema kuwa dhumuni la kuundwa kwa Tume ni kufanya tathmini ya mifumo ya kodi, mapato na tozo nyingine ili kuiwezesha Serikali kuchukua hatua stahiki za kuondoa kero/malalamiko, kuimarisha ukusanyaji wa mapato, kuboresha mazingira ya biashara na uwekezaji na kuvutia mitaji ya ndani na nje ya nchi.

Mdau wa masuala ya kodi, unaombwa kutoa maoni yako kuhusu changamoto zilizopo kwenye masuala ya kodi, upendekeze njia za kutatua changamoto hizo. Pamoja na mambo mengine, Tume imewaomba wadau kuendelea kutoa maoni na mapendekezo ya kuboresha kwa kutuma ujumbe mfupi (sms) na Whatsapp kwa namba 0748 755677, 0738 588813, 0682 288784.


Matangazo

  • No records found
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • SHINYANGA KUNUFAIKA NA MIRADI YA REA, WAUZIWA KWA RUZUKU MITUNGI 13000

    June 02, 2025
  • ENDELEENI KUTOA ELIMU ZAIDI KUHUSU AFYA YA AKILI - DC. MBONI

    May 30, 2025
  • TAKUKURU SHINYANGA YAANZA KUCHUKUA HATUA DHIDI YA UBADHIRIFU WA SHILINGI MILIONI 92 ZA WAKULIMA WA TUMBAKU WA USHETU - DONASIAN.

    May 27, 2025
  • MAISHA BAADA YA KUSTAAFU YANAHITAJI UTULIVU - DC. MTATIRO

    May 26, 2025
  • Angalia zote

Video

MIFUKO BANDIA ZAIDI YA ELFU 20 YAKAMATWA SHINYANGA
Video Nyinginezo

Viunganishi vya Haraka

  • Historia
  • Dira na Dhima
  • Hotuba Mbalimbali
  • Video Mbalimbali
  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Picha za Matukio
  • Miongozo na kanuni

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Mfumo wa kutuma, kupokea na kufuatilia malalamiko, mapendekezo, maulizo na pongezi
  • Ofisi ya Rais Menejimenti ya utumishi wa Umma
  • Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Boma Street, Mwanza Road

    Anuani: P.O.Box 320, Shinyanga

    Simu: +255 28 2762222

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras@shinyanga.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2018. Mkoa wa Shinyanga. Haki zote zimehifadhiwa