• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
    • eVibali |
Shinyanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Shinyanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Yetu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
      • Afya
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Shinyanga
    • Wilaya ya Kahama
    • Wilaya ya Kishapu
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu
    • Halmashauri ya Mji wa Kahama
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu
    • Halmashauri ya Wilaya ya Msalala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
    • Bandari Kavu
  • Huduma
    • Kutoa Ushauri wa Kitaalam
    • Kutafsiri Sheria na Sera
    • Kuratibu Shughuli za Wadau
    • Ulinzi na Usalama
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Tafiti
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha

NATOA WITO KWA VIJANA HAPA SHINYANGA KUREJEA NA KUTATHIMINI UPYA NJIA ZA KUJIPATIA KIPATO - RC. MACHA

Posted on: May 20th, 2025

Na: Paul Kasembo.

MKUU wa Mkoa wa Shinyanga Mhe. Anamringi Macha, ametoa wito kwa vijana mkoani hapa kutathmini upya mbinu wanazotumia katika kujipatia kipato, kwa kuzingatia usalama wao, uhalali wa shughuli hizo pamoja na mustakabali wa maisha yao ya sasa na baadae.

Akizungumza na vyombo vya habari kufuatia tukio la ajali ya mgodi wa dhahabu namba nane (8) katika Kata ya Mwakitolyo, Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga, Mhe. Macha alisema kuwa ofisi yake iko wazi kupokea na kufanyia kazi ushauri wowote kutoka kwa wadau mbalimbali kuhusu tukio hilo. Alisisitiza kuwa hadi sasa Serikali imethibitisha vifo vya watu sita (6) na majeruhi kumi na mmoja (11), ambapo wanne kati yao tayari wameruhusiwa kutoka hospitali, mmoja amehamishiwa Hospitali ya Rufaa ya Bugando, wawili wanaendelea kupatiwa matibabu katika wodi na wengine watatu walipokelewa na kuhudumiwa katika Zahanati ya Mwakitolyo.

“Nitumie nafasi hii kutoa wito kwa vijana wote hapa Shinyanga kutathmini kwa kina njia wanazotumia kujipatia kipato. Kuna mifano mizuri ya vijana wanaojihusisha na kilimo cha kisasa na kufanikiwa. Mathalani, vijana wa Kikundi cha Jipange kilichopo Kata ya Kishapu wanajishughulisha na kilimo cha matunda kama tikiti maji na Kata ya Songwa wanaojishughulisha na kilimo cha nyanya na mpunga. Hawa ni baadhi tu ya vijana na vikundi vya kuigwa kwani wameweza kuinua maisha yao kiuchumi kwa kutumia njia salama na halali,” alisema Mhe. Macha.

Aidha, RC. Macha alisisitiza kuwa taarifa rasmi kuhusu ajali ya mgodi huo alizitoa akiwa eneo la tukio husika (ndani ya mgodi) na leo tena alirejea mbele ya wanahabari na pia alikanusha uvumi ulioenea kupitia baadhi ya vyombo vya habari kuhusu idadi tofauti ya waliofukiwa mgodini na kwamba hofu ilitanda eneo hilo kuwa siyo za kweli kabisa.

Ajali hiyo iliripotiwa kutokea mnamo Mei 17, 2025 majira ya saa 5 asubuhi katika mgodi huo wa dhahabu uliopo Mwakitolyo, ambapo hatua mbalimbali zimechukuliwa kuhakikisha wahanga wanapata huduma stahiki na kuchunguzwa kwa kina ili tukio kama hilo lisijirudie tena.


Matangazo

  • No records found
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • NATOA WITO KWA VIJANA HAPA SHINYANGA KUREJEA NA KUTATHIMINI UPYA NJIA ZA KUJIPATIA KIPATO - RC. MACHA

    May 20, 2025
  • SERIKALI YATHIBITISHA VIFO VYA WATU SITA NA MAJERUHI 11 KATIKA AJALI YA MGODI WA MWAKITOLYO.

    May 18, 2025
  • WAZAZI NA WALEZI, NENDENI MKAWE MABALOZI SAHIHI WA KAZI ZA MHE. RAIS DKT. SAMIA SULUHU HASSAN – RC. MACHA

    May 16, 2025
  • WAZAZI NA WALEZI WEKEZENI ZAIDI KATIKA MALEZI NA MAKUZI YA WATOTO – LYAMONGI

    May 15, 2025
  • Angalia zote

Video

MIFUKO BANDIA ZAIDI YA ELFU 20 YAKAMATWA SHINYANGA
Video Nyinginezo

Viunganishi vya Haraka

  • Historia
  • Dira na Dhima
  • Hotuba Mbalimbali
  • Video Mbalimbali
  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Picha za Matukio
  • Miongozo na kanuni

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Mfumo wa kutuma, kupokea na kufuatilia malalamiko, mapendekezo, maulizo na pongezi
  • Ofisi ya Rais Menejimenti ya utumishi wa Umma
  • Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Boma Street, Mwanza Road

    Anuani: P.O.Box 320, Shinyanga

    Simu: +255 28 2762222

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras@shinyanga.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2018. Mkoa wa Shinyanga. Haki zote zimehifadhiwa