• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
    • eVibali |
Shinyanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Shinyanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Yetu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
      • Afya
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Shinyanga
    • Wilaya ya Kahama
    • Wilaya ya Kishapu
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu
    • Halmashauri ya Mji wa Kahama
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu
    • Halmashauri ya Wilaya ya Msalala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
    • Bandari Kavu
  • Huduma
    • Kutoa Ushauri wa Kitaalam
    • Kutafsiri Sheria na Sera
    • Kuratibu Shughuli za Wadau
    • Ulinzi na Usalama
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Tafiti
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha

NIMERIDHISHWA NA KASI YA KILIMO CHA ZAO LA PAMBA HAPA WILAYANI KISHAPU - RC MACHA

Posted on: February 13th, 2025

Na. Paul Kasembo, KISHAPU DC.

MKUU wa Mkoa wa Shinyanga Mhe. Anamringi Macha amesema kuwa ameridhishwa na kasi inayoendelea katika kilimo cha zao la pamba huku akiwasisitiza wataalamu kuendelea kuwafikia wakulima katika maeneo yao na kuwaelimisha matumizi ya vifaa vya kisasa ikiwemo ndege ndogo zisizokuwa na rubani (drone) katika kuboresha zao hili ambapo zinatumika kunyunyizia dawa shambani, ndege ambazo zimepelekwa na Bodi ya Pamba.

Hayo ameyasema wakati akifanya ukaguzi, hamasa na ufuatiliaji wa kilimo cha zao la pamba wilayani Kishapu ambapo pamoja na mambo mengine RC Macha amesema kuwa uwepo wa vifaa hivyo vya kisasa unamuwezesha mkulima kunyunyizia dawa katika shamba lenye ukubwa wa Hekari 1 kwa dakika 6 tu, jambo ambalo linatajwa kuwa mkombozi mkubwa wa mkulima wa zao la pamba.

"Nimefuatilia na kukagua mashamba yenu ndugu zangu niseme kuwa nimeridhishwa sana na kasi ya kilimo cha zao hili la pamba hapa wilayani Kishapu, hakika sasa tunakwenda kurejesha heshima ya zao la pamba kama ilivyokuwa hapo awali na hili ndiyo kusudio la Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan la kuhakikisha kilimo hiki cha pamba kinakuwa ni chenye tija zaidi kwenu na kuchechemua uchumi wa wananchi pamoja na kuongeza pato la Taifa," amesema RC Macha.

RC Macha akiwa ameongozana na mwenyeji wake Mkuu wa Wilaya ya Kishapu Mhe. Peter Masindi, Katibu Tawala Wilaya ya Kishapu Bi. Fatma Mohamed, Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Kishapu Ndg. Emmanuel Johnson na wataalamu wengine ambapo amesisitiza kuwa, lengo la Serikali ni kuona kila mkulima wa zao la pamba anahakikisha kuwa kila Hekari moja (1) inazalisha kuanzia Kilo 1000 hadi 1200.

Kiwango hicho kinatajwa kuwahi kufikiwa hapo awali ambapo walikuwa wanafikia hadi Kilo 1800 kwa hekari 1 na hivyo kukifanya kilimo cha zao la pamba kuwa ni moja kati zao la biashara na yenye tija zaidi kwa wananchi mkoani Shinyanga na kustawisha maisha yao.

Huu ni mwendelezo wa ziara za RC Macha za kuwafikia wananchi moja kwa moja katika maeneo yao ikiwemo shambani akiwa na lengo la kuhakikisha amesikiliza na kutatua changamoto zao.


Matangazo

  • No records found
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • KIKAO CHA MAPITIO YA ROBO MWAKA KWA KIPINDI CHA OKT - DES 2024 CHA (PJT MMMAM) CHAFANYIKA MKOANI SHINYANGA.

    February 28, 2025
  • RCC SHINYANGA YARIDHIA MAPENDEKEZO NANE (8) YA MATUMIZI BORA YA ARDHI.

    February 27, 2025
  • KUKAMILISHWA KWA MIRADI YA BARABARA KUTAPUNGUZA KERO KWA WANANCHI – RC MACHA

    February 26, 2025
  • WALIMU, TOENI ELIMU INAYOENDANA NA MABADILIKO YA TEKNOLOJIA -RC MACHA

    February 24, 2025
  • Angalia zote

Video

MIFUKO BANDIA ZAIDI YA ELFU 20 YAKAMATWA SHINYANGA
Video Nyinginezo

Viunganishi vya Haraka

  • Historia
  • Dira na Dhima
  • Hotuba Mbalimbali
  • Video Mbalimbali
  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Picha za Matukio
  • Miongozo na kanuni

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Mfumo wa kutuma, kupokea na kufuatilia malalamiko, mapendekezo, maulizo na pongezi
  • Ofisi ya Rais Menejimenti ya utumishi wa Umma
  • Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Boma Street, Mwanza Road

    Anuani: P.O.Box 320, Shinyanga

    Simu: +255 28 2762222

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras@shinyanga.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2018. Mkoa wa Shinyanga. Haki zote zimehifadhiwa