• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
    • eVibali |
Shinyanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Shinyanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Yetu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
      • Afya
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Shinyanga
    • Wilaya ya Kahama
    • Wilaya ya Kishapu
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu
    • Halmashauri ya Mji wa Kahama
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu
    • Halmashauri ya Wilaya ya Msalala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
    • Bandari Kavu
  • Huduma
    • Kutoa Ushauri wa Kitaalam
    • Kutafsiri Sheria na Sera
    • Kuratibu Shughuli za Wadau
    • Ulinzi na Usalama
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Tafiti
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha

POLISI MKOANI SHINYANGA YABAINI MAKOSA 6320

Posted on: May 27th, 2024

Na. Paul Kasembo, SHY RS.

KAMANDA wa Polisi Mkoa wa Shinyanga SACP Janeth S. Magomi amesema kuwa Jeshi la Polisi Mkoa wa Shinyanga Kikosi cha Usalama Barabarani limekagua, kubaini na kukamata jumla ya makosa 6320 ya Usalama Barabarani ambapo makosa 4847 ni ya magari, 1473 ya pikipiki na bajaji huku wahusika wakiwajibishwa kwa kulipa.

RPC Janeth ameyasema haya leo tarehe 27 Mei, 2024 alipokuwa akitoa Taarifa kwa Umma ambayo inaonesha kuwa makosa haya yamepatikana kati ya Aprili 17, 2024 na Mei 27, 2024 huku akisisitiza kuwa Jeshi la Polisi Mkoa wa Shinyanga litaendelea kuimarisha ulinzi na usalama kwa kushirikiana na Jamii katika kubaini na kutanzua uhalifu kwa kufanya doria, misako pamoja na oparesheni mbalimbali katika kufanikisha kazi zake.

"Jeshi la Polisi Mkoa wa Shinyanga kupitia Kikosi cha Usalama Barabarani limefanya ukaguzi mbalimbali na kubaini jumla ya makosa 6320 ikiwa 4847 ni kutoka katika magari na 1473 ni kwenye pikipiki na bajaji ambapo wahusika wamewajibishwa kwa kulipa faini za papo kwa hapo," amesema RPC Janeth.

Wito umetolewa na Jeshi la Polisi Mkoa wa Shinyanga kwa wananchi wote kuendelea kushirikiana na Polisi katika kubaini na kutanzua uhalifu wa kijinai ikiwemo usafirishaji, uuzaji na utunzaji wa dawa za kulevya na kwamba,  Polisi haitasita kuchukua hatua kali kwa mujibu wa sheria kwa yeyote yule atakayekiuka sheria za nchi.

Matangazo

  • No records found
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • VIJANA NA WASOMI MKOANI SHINYANGA, IGENI MFANO WA BBT KISHAPU - RC MACHA

    February 18, 2025
  • MKANDARASI CHICO, FUNGA TAA UWANJANI HARAKA ILI UTUMIKE MASAA 24 - MHE. MAJALIWA.

    February 16, 2025
  • RC MACHA AMKARIBISHA SHINYANGA WAZIRI MKUU MHE. KASSIM MAJALIWA

    February 15, 2025
  • WAFANYABIASHARA NDOGONDOGO, HAMISHIENI NGUVU KWENYE UONGEZAJI THAMANI WA MAZAO - RC MACHA.

    February 14, 2025
  • Angalia zote

Video

MIFUKO BANDIA ZAIDI YA ELFU 20 YAKAMATWA SHINYANGA
Video Nyinginezo

Viunganishi vya Haraka

  • Historia
  • Dira na Dhima
  • Hotuba Mbalimbali
  • Video Mbalimbali
  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Picha za Matukio
  • Miongozo na kanuni

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Mfumo wa kutuma, kupokea na kufuatilia malalamiko, mapendekezo, maulizo na pongezi
  • Ofisi ya Rais Menejimenti ya utumishi wa Umma
  • Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Boma Street, Mwanza Road

    Anuani: P.O.Box 320, Shinyanga

    Simu: +255 28 2762222

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras@shinyanga.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2018. Mkoa wa Shinyanga. Haki zote zimehifadhiwa