• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
    • eVibali |
Shinyanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Shinyanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Yetu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
      • Afya
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Shinyanga
    • Wilaya ya Kahama
    • Wilaya ya Kishapu
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu
    • Halmashauri ya Mji wa Kahama
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu
    • Halmashauri ya Wilaya ya Msalala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
    • Bandari Kavu
  • Huduma
    • Kutoa Ushauri wa Kitaalam
    • Kutafsiri Sheria na Sera
    • Kuratibu Shughuli za Wadau
    • Ulinzi na Usalama
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Tafiti
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha

Prof. Ndalichako aridhishwa na ubora wa majengo ya Elimu Shinyanga

Posted on: November 10th, 2019

Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Mhe. Prof. Joyce Ndalichako amesema ameridhishwa na ubora wa majengo pamoja na usimamizi mzuri wa fedha za Serikali kwa kufuatilia kwa karibu kuhakikisha ujenzi wa majengo hayo unalingana na thamani ya fedha.

Akizungumza kwa nyakati tofauti wakati wa ziara yake jana tarehe 09/11/2019 Mkoani hapa, ambapo amekagua madarasa yaliyojengwa kwa mpango wa lipa kwa matokeo katika shule ya msingi Viwandani na kuweka jiwe la msingi kwenye Ofisi ya Mdhibiti ubora wa shule kwenye Manispaa ya Shinyanga, pamoja na kufungua Ofisi ya mdhibiti ubora katika Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga Mhe. Ndalichako amesema usimamizi mzuri ndiyo kitu cha muhimu katika kusababisha ubora wa majengo.

Serikali ilitoa kiasi cha sh. milioni 152 kwa ujenzi wa kila Ofisi ya mdhibiti ubora lakini katika Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga, imekamilisha Ofisi hiyo ndani ya muda wa miezi miwili na nusu na kutumia kiasi cha sh. 107 na Halmashauri Manispaa ya Shinyanga ambayo ipo kwenye hatua ya ukamilishaji hadi sasa imetumia kiasi cha sh. milioni 91.

"Hiyo inaonesha kwamba, uaminifu na usimamizi mzuri unapata matokeo mazuri kwa gharama nafuu" amesema Mhe. Ndalichako akiupongeza uongozi wa Mkoa na Wilaya kwa kushirikiana kusimamia vema majengo hayo.

Ameongeza pia, dhamira ya Serikali ni kuhakikisha Watanzania wote wanapata elimu bora ambapo Wadhibiti ubora ndiyo jicho kuhakikisha elimu hiyo inatolewa, lakini kwa muda mrefu walikuwa wamesahaulika hivyo Serikali imetoa shilingi milioni 15. 2 kwa Halmashauri zote nchini kujenga Ofisi za Wadhibiti ubora pamoja na magari 54 yameshanunuliwa ili kuwawezesha kufanya kazi yao kama ilivyo lengo la Serikali.

Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Mhe. Zainab Telack akimshukuru Waziri Ndalichako kwa Wizara yake kufanya kazi kubwa ya kujenga Ofisi za Wadhibiti ubora amemuomba kuangalia namna ya kuwawezesha wadhibiti ubora kupata fungu la kutosha ili waweze kukagua shule zote hasa za pembezoni, 

"Kwa sababu tumesema kipaumbele chetu ni elimu ningependa kuona shule zetu zote zinakaguliwa" amesema Mhe. Telack

Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Mhe. Zainab Telack akisisitiza jambo wakati akimkaribisha Waziri Ndalichako katika Mkoa wa Shinyanga mapema jana tarehe 09/11/2019 Ofisini kwake

Muonekano wa jengo la Ofisi ya Mdhibiti Ubora katika Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga 

Matangazo

  • No records found
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • ENDELEENI KUTOA ELIMU ZAIDI KUHUSU AFYA YA AKILI - DC. MBONI

    May 30, 2025
  • TAKUKURU SHINYANGA YAANZA KUCHUKUA HATUA DHIDI YA UBADHIRIFU WA SHILINGI MILIONI 92 ZA WAKULIMA WA TUMBAKU WA USHETU - DONASIAN.

    May 27, 2025
  • MAISHA BAADA YA KUSTAAFU YANAHITAJI UTULIVU - DC. MTATIRO

    May 26, 2025
  • MAFUNZO YA IPOSA NI MKOMBOZI KWA VIJANA WALIO WENGI WANAOKOSA FURSA YA ELIMU YA KAWAIDA - RC. MACHA

    May 23, 2025
  • Angalia zote

Video

MIFUKO BANDIA ZAIDI YA ELFU 20 YAKAMATWA SHINYANGA
Video Nyinginezo

Viunganishi vya Haraka

  • Historia
  • Dira na Dhima
  • Hotuba Mbalimbali
  • Video Mbalimbali
  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Picha za Matukio
  • Miongozo na kanuni

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Mfumo wa kutuma, kupokea na kufuatilia malalamiko, mapendekezo, maulizo na pongezi
  • Ofisi ya Rais Menejimenti ya utumishi wa Umma
  • Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Boma Street, Mwanza Road

    Anuani: P.O.Box 320, Shinyanga

    Simu: +255 28 2762222

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras@shinyanga.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2018. Mkoa wa Shinyanga. Haki zote zimehifadhiwa