• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
    • eVibali |
Shinyanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Shinyanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Yetu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
      • Afya
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Shinyanga
    • Wilaya ya Kahama
    • Wilaya ya Kishapu
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu
    • Halmashauri ya Mji wa Kahama
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu
    • Halmashauri ya Wilaya ya Msalala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
    • Bandari Kavu
  • Huduma
    • Kutoa Ushauri wa Kitaalam
    • Kutafsiri Sheria na Sera
    • Kuratibu Shughuli za Wadau
    • Ulinzi na Usalama
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Tafiti
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha

RAIS AENDELEA KUTIMIZA AHADI YAKE KWA MAAFISA TARAFA MKOA WA SHINYANGA

Posted on: May 29th, 2020

Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Bi. Zainab Telack amekabidhi Pikipiki 14 kwa Maafisa Tarafa wa Mkoa wa Shinyanga kwa lengo la kurahisisha utendaji kazi wao na kuonya kuwa hatarajii kuona pikipiki hizo zikitumika nje ya shughuli za Serikali.

Kiongozi huyo wa Mkoa wa Shinyanga amekabidhi pikipiki hizo kwa niaba ya Rais John Pombe Magufuli na kuwataka maafisa tarafa hao kuhakikisha pikipiki hizo zinatunzwa vizuri ili wengine waweze kuzitumia na kuwaonya watendaji hao kutotumia pikipiki hizo kubeba abiria kama ilivyo kwa madereva bodaboda.

Aidha Bi. Telack amewataka Maafisa Tarafa hao pamoja na kupewa pikipiki mpya pia wahakikishe wanatunza Ofisi walizojengewa pamoja na vifaa walivyopewa kwa lengo kuwezesha mazingira mazuri ya utendaji kazi zinatunzwa vizuri akionya kuwa baadhi yao tayari washaanza matumizi mabaya ya vifaa hivyo.

‘’Wapo watu wanafanya vizuri na tumeanza kuona mnavyofanya kazi vizuri, yapo matatizo mengine mmeanza kuyashughulikia endeleeni lakini niwahusie kuwa zile kompyuta ni kwa ajili ya matumizi ya kazi za Serikali zisitoke kwenda sehemu yoyote fanyeni kazi kwani nasi tunafarijika kuona mnafanya kazi na kutupunguzia mzigo.’’Aliendelea kusema Bi. Zainab Telack Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga.

Mkuu wa Mkoa pia aliwataka Maafisa Tarafa hao kuwasimamia watendaji wa kata ili waeze kutatua migogoro inayowakabili wananchi akiongeza kuwa lengo la Serikali ni kuona wananchi wa Shinyanga wakiishi kwa furaha na amani na kutambua uwepo wa viongozi wao.

Bi. Telack amewataka Maafisa Tarafa kutunza pikipiki hizo kutokana na uwepo wa mahitaji makubwa ya pikipiki katika jamii nakuwazuia wasisimame nazo katika mabaa na kuonya kuwa Afisa yoyote atakayesema kuwa Pikipiki yake imeibiwa hataeleweka.

Wakati huo huo Afisa Tarafa Bw. Cleophasi Mdui amempongeza Rais John Pombe Magufuli kwa kutekeleza ahadi yake ya kuwapatia vitendea kazi maafisa hao baada ya kuwaita Ikulu Juni 4, mwaka jana na kuhaidi kuendelea kufanya kazi kwa bidii na kulipa fadhila kwa kiongozi Mkuu wa Nchi.

Naye Afisa Tarafa kutoka Old Shinyanga Bi. Neema Mkandala amesema usafiri huo utawawezesha Mafisa Tarafa hao kutatua kero za wananch kwa haraka ikiwemo kufika maeneo yenye shida na kutoa maelekezo kwa wananchi kwa lengo la kuboresha ufanisi.

Pikipiki hizo zimetolewa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Rais John Pombe Magufuli kama kutimiza ahadi yake kwa Maafisa hao aliyoitoa tarehe 4 Juni mwaka jana Ikulu jijini Dar es Salaam.  

Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Bi. Zainab Telack akiongea na vyombo vya habari pamoja na  Maafisa Tarafa

 wa Mkoa wa Shinyanga mapema leo Ofisini kwake Mjini Shinyanga wakati wakuwakabidhi pikipiki 14 maafisa 

hao zilizotolewa na Rais John Pombe Magufuli kwa lengo la kuboresha utendaji wao.


Matangazo

  • No records found
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • WANUFAIKA WA MIKOPO YA 10% LIPENI KWA WAKATI ILI PIA VIKOPESHWE NA VIKUNDI VINGINE - RC MACHA

    February 13, 2025
  • CP. HAMDUNI AKUTANA NA KAMATI YA MICHEZO YA JWTZ

    February 13, 2025
  • WANANCHI, LIPENI KODI YA ARDHI KWA WAKATI MUEPUKE RIBA - LEO KOMBA

    February 12, 2025
  • WAJUMBE WA BODI, TUMIENI TAALUMA ZENU KUISAIDIA HOSPITALI KUKAMILISHA MIRADI YA UJENZI- RAS CP. HAMDUNI.

    February 11, 2025
  • Angalia zote

Video

MIFUKO BANDIA ZAIDI YA ELFU 20 YAKAMATWA SHINYANGA
Video Nyinginezo

Viunganishi vya Haraka

  • Historia
  • Dira na Dhima
  • Hotuba Mbalimbali
  • Video Mbalimbali
  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Picha za Matukio
  • Miongozo na kanuni

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Mfumo wa kutuma, kupokea na kufuatilia malalamiko, mapendekezo, maulizo na pongezi
  • Ofisi ya Rais Menejimenti ya utumishi wa Umma
  • Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Boma Street, Mwanza Road

    Anuani: P.O.Box 320, Shinyanga

    Simu: +255 28 2762222

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras@shinyanga.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2018. Mkoa wa Shinyanga. Haki zote zimehifadhiwa