• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
    • eVibali |
Shinyanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Shinyanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Yetu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
      • Afya
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Shinyanga
    • Wilaya ya Kahama
    • Wilaya ya Kishapu
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu
    • Halmashauri ya Mji wa Kahama
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu
    • Halmashauri ya Wilaya ya Msalala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
    • Bandari Kavu
  • Huduma
    • Kutoa Ushauri wa Kitaalam
    • Kutafsiri Sheria na Sera
    • Kuratibu Shughuli za Wadau
    • Ulinzi na Usalama
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Tafiti
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha

RAS CP. HAMDUNI AJITAMBULISHA MBELE YA BARAZA LA MADIWANI SHINYANGA MC

Posted on: October 31st, 2024

Na. Paul Kasembo, SHY MC.

KATIBU Tawala Mkoa wa Shinyanga CP. Salum Hamduni amejitambulisha mbele ya Baraza la Waheshimiwa Madiwani wa Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga huku akiwaomba ushirikiano wao katika kuhakikisha anatekeleza vema wajibu na majukumu yake ya kila siku hapa Mkoa wa Shinyanga.

CP. Hamduni ameyasema haya leo tarehe 31 Oktoba, 2024 katika ukumbi wa mkutano uliopo Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga ambapo pia ametumia nafasi hii kuwakumbusha Waheshimiwa Madiwani kwenda kuwa sehemu ya utoaji hamasa na elimu juu ya ushiriki wa wananchi katika Uchaguzi wa Serikali za Mitaa na kwamba watumie fursa zote za vikao na mikutano yao kutoe ujumbe huu ili wakati utakapofika wananchi waweze kujitokeza na kushiriki kikamilifu zaidi.

"Waheshimiwa Madiwani Manispaa ya Shinyanga pamoja na watumishi wenzangu, baada ya kujitambulisha rasmi kwenu sasa niwaombe ushirikiano wenu ili nami niweze kutekeleza vema wajibu na majukumu yangu na pia twende tukasaidie kutoa elimu na hamasa kwa wanachama na wananchi wetu ili waweze kushiriki Uchaguzi wa Serikali za Mitaa tarehe 27 Novemba, 2024," amesema CP. Hamduni.

Kando na hili, pia amewataka Waheshimiwa Madiwani kwenda kushirikiana na Kamati za Usalama katika maeneo yao ukizingatia tunaelekea kwenye Uchaguzi hivyo wananchi wawe na amani na utulivu zaidi kusiwepo na hali yoyote itayopelekea viashiria vya uvunjifu wa amani wakati wote. 

Kwa upande wake Naibu Meya Manispaa ya Shinyanga Mhe. Zamda Shabani kwa niaba ya Mstahiki Meya Mhe. Elias Masumbuko na Waheshimiwa Madiwani amemkaribisha kwa mikono miwili CP. Hamduni na kwamba amemhakikishia ushirikiano wa haki na mali wakati wote kutoka kwao na wananchi wa Manispaa kwa ujumla.

Matangazo

  • No records found
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • KIKAO CHA MAPITIO YA ROBO MWAKA KWA KIPINDI CHA OKT - DES 2024 CHA (PJT MMMAM) CHAFANYIKA MKOANI SHINYANGA.

    February 28, 2025
  • RCC SHINYANGA YARIDHIA MAPENDEKEZO NANE (8) YA MATUMIZI BORA YA ARDHI.

    February 27, 2025
  • KUKAMILISHWA KWA MIRADI YA BARABARA KUTAPUNGUZA KERO KWA WANANCHI – RC MACHA

    February 26, 2025
  • WALIMU, TOENI ELIMU INAYOENDANA NA MABADILIKO YA TEKNOLOJIA -RC MACHA

    February 24, 2025
  • Angalia zote

Video

MIFUKO BANDIA ZAIDI YA ELFU 20 YAKAMATWA SHINYANGA
Video Nyinginezo

Viunganishi vya Haraka

  • Historia
  • Dira na Dhima
  • Hotuba Mbalimbali
  • Video Mbalimbali
  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Picha za Matukio
  • Miongozo na kanuni

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Mfumo wa kutuma, kupokea na kufuatilia malalamiko, mapendekezo, maulizo na pongezi
  • Ofisi ya Rais Menejimenti ya utumishi wa Umma
  • Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Boma Street, Mwanza Road

    Anuani: P.O.Box 320, Shinyanga

    Simu: +255 28 2762222

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras@shinyanga.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2018. Mkoa wa Shinyanga. Haki zote zimehifadhiwa