• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
    • eVibali |
Shinyanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Shinyanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Yetu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
      • Afya
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Shinyanga
    • Wilaya ya Kahama
    • Wilaya ya Kishapu
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu
    • Halmashauri ya Mji wa Kahama
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu
    • Halmashauri ya Wilaya ya Msalala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
    • Bandari Kavu
  • Huduma
    • Kutoa Ushauri wa Kitaalam
    • Kutafsiri Sheria na Sera
    • Kuratibu Shughuli za Wadau
    • Ulinzi na Usalama
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Tafiti
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha

RAS HAMDUNI AKARIBISHA TIMU YA MAMA SAMIA LEGAL SHINYANGA

Posted on: October 2nd, 2025

Katibu Tawala wa Mkoa wa Shinyanga, CP Salum Hamduni, leo Oktoba 2, 2025, amepokea rasmi timu ya Mama Samia Legal kikosi maalum cha wataalamu wa sheria kilichofika mkoani Shinyanga kwa ajili ya kutoa msaada wa kisheria katika magereza, hususan kwa wahitaji wasiokuwa na uwezo wa kupata uwakilishi wa kisheria.

Akizungumza wakati wa kuwapokea, CP Hamduni aliipongeza timu hiyo kwa kazi kubwa wanayoifanya ya kuwafikia wananchi walioko magerezani, akisisitiza kuwa serikali ya mkoa iko tayari kutoa ushirikiano wa karibu kuhakikisha huduma hiyo inatolewa kikamilifu na kwa ufanisi.

“Niwakaribishe katika Mkoa wa Shinyanga. Hii ni kazi ya huruma na haki. Tunawapongeza kwa uamuzi wa kuwatumikia wale ambao mara nyingi sauti zao hazisikiki. Serikali ya mkoa ipo pamoja nanyi,” alisema CP Hamduni.

Kwa upande wake, Mratibu wa Mama Samia Legal, Bw. Haruna Matata, alisema kuwa timu hiyo inajumuisha wataalamu kutoka taasisi mbalimbali za serikali ikiwemo Wizara ya Katiba na Sheria, Wizara ya Mambo ya Ndani, Ofisi ya Taifa ya Mashtaka, Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora, pamoja na Makao Makuu ya Magereza.

Bwana Matata alieleza kuwa lengo kuu la programu hiyo ni kusogeza huduma za kisheria karibu na wananchi walio magerezani, hasa wale waliokosa msaada wa uwakilishi wakati wa mashauri yao. Alibainisha kuwa Shinyanga ni mkoa wa pili kutembelewa baada ya Mwanza, katika kampeni ya kitaifa inayolenga kufikia magereza yote 128 nchini.

“Wapo wafungwa wengi waliokosa wanasheria wakati wa kesi zao, na huenda waliadhibiwa bila msaada sahihi wa kisheria. Sisi kama timu ya Mama Samia Legal, tumejipanga kuwapa msaada huo kwa weledi na huruma,” alisema

Huduma hii ni sehemu ya dhamira ya Serikali ya Awamu ya Sita chini ya Rais Samia Suluhu Hassan ya kuhakikisha haki inatolewa kwa wote, bila kujali uwezo wa mtu. Zoezi hilo litakuwa endelevu na linaweka historia mpya ya usawa mbele ya sheria kwa watanzania wote.

Matangazo

  • No records found
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • RC MHITA AWAHAMASISHA WAFANYABIASHARA NA WAWEKEZAJI KUCHANGAMKIA FURSA ZA KIUCHUMI MKOANI SHINYANGA

    November 13, 2025
  • RC MHITA AKUTANA NA MSANII BANDO MC, APONGEZA JUHUDI ZA KUSAIDIA VIJANA SHINYANGA

    November 11, 2025
  • RC MHITA APONGEZA UONGOZI MPYA WA KANISA LA WASABATO NGBF MKOANI SHINYANGA.

    November 07, 2025
  • WANAFUNZI 29,193 KUFANYA MTIHANI WA UPIMAJI KIDATO CHA PILI SHINYANGA.

    November 07, 2025
  • Angalia zote

Video

RC MHITA AWAHAMASISHA WAFANYABIASHARA NA WAWEKEZAJI KUCHANGAMKIA FURSA ZA KIUCHUMI MKOANI SHINYANGA
Video Nyinginezo

Viunganishi vya Haraka

  • Historia
  • Dira na Dhima
  • Hotuba Mbalimbali
  • Video Mbalimbali
  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Picha za Matukio
  • Miongozo na kanuni

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Mfumo wa kutuma, kupokea na kufuatilia malalamiko, mapendekezo, maulizo na pongezi
  • Ofisi ya Rais Menejimenti ya utumishi wa Umma
  • Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    OFISI YA MKUU WA MKOA, MKOA WA SHINYANGA, 04 MTAA WA BOMA

    Anuani: P.O.Box 320, 37180,SHINYANGA, TANZANIA

    Simu: +255 28 2762222

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras@shinyanga.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2018. Mkoa wa Shinyanga. Haki zote zimehifadhiwa