• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
    • eVibali |
Shinyanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Shinyanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Yetu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
      • Afya
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Shinyanga
    • Wilaya ya Kahama
    • Wilaya ya Kishapu
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu
    • Halmashauri ya Mji wa Kahama
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu
    • Halmashauri ya Wilaya ya Msalala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
    • Bandari Kavu
  • Huduma
    • Kutoa Ushauri wa Kitaalam
    • Kutafsiri Sheria na Sera
    • Kuratibu Shughuli za Wadau
    • Ulinzi na Usalama
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Tafiti
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha

RAS SHINYANGA AFUNGUA KIKAO CHA VYAMA VIKUU VYA USHIRIKA NA WARAJIS WASAIDIZI WA MIKOA - KANDA YA ZIWA

Posted on: November 10th, 2023

Na. Shinyanga RS.

KATIBU Tawala Mkoa wa Shinyanga Prof. Siza D. Tumbo amefungua kikao cha vyama vya ushirika na warajis wasaidizi wa mikoa ya kanda ya ziwa na baadhi ya mikoa ya singida na Tabora kilichofanyika leo 10 Nov, 2023 katika ukumbi wa mikutano ofisi ya mkuu wa mkoa lengo ni kuhabarishana juu ya kuanza kwa matumizi ya Mfumo wa Stakabadhi Ghalani huku akiwasisitiza kwenda kuwa wazalendo katika utekelezaji huu ili ulete tija kama serikali ilivyokusudia.

Prof. Tumbo amesema serikali hii ya awamu ya sita inayoongozwa na Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, yeye mwenyewe Mhe. Rais ameamua kurejesha mfumo huu kwetu ili unufaishe vema pande zote, na kwamba kinachotakiwa kwa viomgozi hawa sasa ni kwenda kuutndea haki katika maeneo yao.

"Niwaagize viongozi wote wa Muungano wa Vyama vya Msingi vya Ushirika kwenda kutanguliza uzalendo, weledi na umakini zaidi katika kutekeleza mfumo huu wa stakabadhi ghalani ili ulete tija kwa pande zote kama ambavyo serikali ilivyo na nia njema na wananchi wake kupitia ninyi," alisema Prof. Tumbo.

Kwa upande wake Mrajis Msaidizi Mkoa wa Shinyanga Bi. Hilda Boniphace ambaye pia katika kikao hiki alikuwa Mwenyekiti aliwakumbusha washiriki kwenda kuanza maandalizi hivi sasa ya utumiaji wa mfumo huu, huku akiwasisitiza katika kushirikisha makundi yote muhimu katika kuwapatia elimu na taarifa ili wakati utakapofika iwe rahisi katika utekelezaji.

Nao washiriki wa kikao hiki kwa kauli moja wameazimia kwenda kusimamia yale yote waliyokubaliana ili kuleta tija kwao na kwa nyingine za wadau kama ambavyo serikali imekusudia.

Pamoja na RAS Shinyanga, pia kikao kimehudhuriwa na Augustino Mbulumi, Mkurugenzi wa Uendeshaji Soko la Bidhaa Tanzania (TMX), Witness Temba Afisa Udhibiyi Ubora kutoka Bodi ya Usimamizi wa Stakabadhi za Ghala Tanzania na Robert Nsunza kutoka Masoko na Uwekezaji Tume ya Maendeleo ya Ushirika Tanzania.

Stakabadhi ghalani ina lengo la kumsaidia mkulima kuuza zao lake kwa bei ya soko, uhakika wa soko, uhakika wa kuhifadhi zao lake na ushindani kulingana na hali ya soko, kujuwa hali ya soko nk.


HABARI PICHA

Prof. Siza D. Tumbo, Katibu Tawala Mkoa wa Shinyanga akielezea jambo wakati wa kikao cha viongozi wa vyama vikuu vya ushirika wa mikoa ya kanda ya ziwa na baadhi ya mikoa ya Tabora na Singida.

Bi. Hilda Boniphace, Mrajis Msaidizi Mkoa wa Shinyanga

Sehemu ya viongozi wa vyama vya ushirika wakiwa ukumbi wa mikutano uliopo ofisi ya mkuu wa mkoa wa shinyanga wakati wa kikao

Matangazo

  • No records found
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • WANUFAIKA WA MIKOPO YA 10% LIPENI KWA WAKATI ILI PIA VIKOPESHWE NA VIKUNDI VINGINE - RC MACHA

    February 13, 2025
  • CP. HAMDUNI AKUTANA NA KAMATI YA MICHEZO YA JWTZ

    February 13, 2025
  • WANANCHI, LIPENI KODI YA ARDHI KWA WAKATI MUEPUKE RIBA - LEO KOMBA

    February 12, 2025
  • WAJUMBE WA BODI, TUMIENI TAALUMA ZENU KUISAIDIA HOSPITALI KUKAMILISHA MIRADI YA UJENZI- RAS CP. HAMDUNI.

    February 11, 2025
  • Angalia zote

Video

MIFUKO BANDIA ZAIDI YA ELFU 20 YAKAMATWA SHINYANGA
Video Nyinginezo

Viunganishi vya Haraka

  • Historia
  • Dira na Dhima
  • Hotuba Mbalimbali
  • Video Mbalimbali
  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Picha za Matukio
  • Miongozo na kanuni

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Mfumo wa kutuma, kupokea na kufuatilia malalamiko, mapendekezo, maulizo na pongezi
  • Ofisi ya Rais Menejimenti ya utumishi wa Umma
  • Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Boma Street, Mwanza Road

    Anuani: P.O.Box 320, Shinyanga

    Simu: +255 28 2762222

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras@shinyanga.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2018. Mkoa wa Shinyanga. Haki zote zimehifadhiwa