• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
    • eVibali |
Shinyanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Shinyanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Yetu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
      • Afya
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Shinyanga
    • Wilaya ya Kahama
    • Wilaya ya Kishapu
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu
    • Halmashauri ya Mji wa Kahama
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu
    • Halmashauri ya Wilaya ya Msalala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
    • Bandari Kavu
  • Huduma
    • Kutoa Ushauri wa Kitaalam
    • Kutafsiri Sheria na Sera
    • Kuratibu Shughuli za Wadau
    • Ulinzi na Usalama
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Tafiti
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha

RC MACHA AFUNGUA MAONESHO YA NANENANE KANDA YA ZIWA MASHARIKI

Posted on: August 3rd, 2024

Na. Paul Kasembo, SHY RS.

MKUU wa Mkoa wa Shinyanga Mhe. Anamringi Macha amefungua maonesho ya nanenane Kanda ya Ziwa Masharikii yanayofanyika viwanja vya Nyakabindi Bariadi mkoani Simiyu huku akiwataka wananchi kutembelea maonesho haya ili wapate elimu, ushauri na maarifa mapya juu ya kuendesha kilimo na ufugaji wa kisasa kwani katika viwanja hivi kuna wataalam wengi mbalimbali kutoka mikoa ya Shinyanga, Simiyu, Mara na pia  Wizara zimeshiriki.

RC Macha ameyasema haya leo tarehe 3 Agosti, 2024 alipokuwa alipokuwa akihutubia mkutano mkubwa wa hadhara ambao umehudhuriwa na viongozi mbalimbali akiwemo Mkuu wa Mkoa wa Simiyu Mhe. Kenan Kihongosi ambaye ndiye mwenyeji wa maonesho haya, alikuwepo pia Mkuu wa Mkoa wa Mara Mhe.Kanali Evans Mtambi, Makatibu Tawala wa Mikoa yote mitatu, Wakuu wa Wilaya, Wakuu wa Taasisi na wananchi ambao kimsingi ndiyo walengwa huku akipongeza kwa ujumla namna ambavyo maandalizi yamefanyika kufanikisha maonesho haya.

"Pamoja na pongezi kwa wandaaji wa maonesho haya, lakini niwaombe wananchi wajitokeze kwa wingi hapa kwa siku hizi za maonesho ili wapate elimu, ushauri na utaalam kutoka kwa wabobezi wetu kuhusu namna bora ya kulima, kufuga na kufanya biashara kilimo, na uzuri wake ni kwamba vyote hivi vinafanyika bure bila gharama yoyote,"amesema RC Macha.

Awali akimkaribisha kuhutubia wananchi, RC Kihongosi alisema kuwa uwepo wa maonesho haya Nyakabindi ni fursa kubwa sana kwa wananchi wetu wa Mikoa hii mitatu ya Shinyangq, Mara na Simiyu kwani imekutanisha wataalam wa Serikali, Taasisi na Sekta binafsi 

Maonesho haya ya nanenane yanatarajiwa kuhitimishwa ifikapo tarehe 8 Agosti, 2024 ikiwa ni kilele chake kwa nchi nzima huku yakitajwa kuwa na tija zaidi kwa wananchi hususan wakulima ambao watapata fursa ya kukutana na wataalam, taasisi mbalimabali zikiwemo za kifedha na kilimo zenye kutoa elimu, mikopo ya vifaa vya kilimo na namna bora ya kufanya kilimo na ufugaji kuwa wenye tija zaidi kwa rasilimali chache.



Matangazo

  • No records found
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • ENDELEENI KUTOA ELIMU ZAIDI KUHUSU AFYA YA AKILI - DC. MBONI

    May 30, 2025
  • TAKUKURU SHINYANGA YAANZA KUCHUKUA HATUA DHIDI YA UBADHIRIFU WA SHILINGI MILIONI 92 ZA WAKULIMA WA TUMBAKU WA USHETU - DONASIAN.

    May 27, 2025
  • MAISHA BAADA YA KUSTAAFU YANAHITAJI UTULIVU - DC. MTATIRO

    May 26, 2025
  • MAFUNZO YA IPOSA NI MKOMBOZI KWA VIJANA WALIO WENGI WANAOKOSA FURSA YA ELIMU YA KAWAIDA - RC. MACHA

    May 23, 2025
  • Angalia zote

Video

MIFUKO BANDIA ZAIDI YA ELFU 20 YAKAMATWA SHINYANGA
Video Nyinginezo

Viunganishi vya Haraka

  • Historia
  • Dira na Dhima
  • Hotuba Mbalimbali
  • Video Mbalimbali
  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Picha za Matukio
  • Miongozo na kanuni

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Mfumo wa kutuma, kupokea na kufuatilia malalamiko, mapendekezo, maulizo na pongezi
  • Ofisi ya Rais Menejimenti ya utumishi wa Umma
  • Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Boma Street, Mwanza Road

    Anuani: P.O.Box 320, Shinyanga

    Simu: +255 28 2762222

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras@shinyanga.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2018. Mkoa wa Shinyanga. Haki zote zimehifadhiwa