• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
    • eVibali |
Shinyanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Shinyanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Yetu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
      • Afya
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Shinyanga
    • Wilaya ya Kahama
    • Wilaya ya Kishapu
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu
    • Halmashauri ya Mji wa Kahama
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu
    • Halmashauri ya Wilaya ya Msalala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
    • Bandari Kavu
  • Huduma
    • Kutoa Ushauri wa Kitaalam
    • Kutafsiri Sheria na Sera
    • Kuratibu Shughuli za Wadau
    • Ulinzi na Usalama
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Tafiti
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha

RC MACHA AKUTANA NA UONGOZI WA SHIRIKA LA STANDING VOICE LINALOTOA HUDUMA KWA WATU WENYE UALBINO

Posted on: March 25th, 2025

Na. Paul Kasembo, SHY RS.

Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Mhe. Anamringi Macha leo Machi 25, 2025 amekutana na kufanya mazungumzo na Uongozi wa Shirika la Standing Voice linalojishughulisha na utoaji wa huduma kwa watu wenye Ualbino ambao wanafanya kiliniki za uchunguzi wa ngozi na macho katika Hospitali za Wilaya mkoani Shinyanga, Shule zenye wanafunzi wenye ualbino pamoja na makao za watoto zenye watoto wenye ualbino

RC Macha pamoja na mambo mengine amewashukuru na kuwapongeza Shirika la Standing Voice kwa kuendelea kushirikiana na Serikali kupitia Maafisa Ustawi wa Jamii ili kuwatunza watoto wenye Ualbino kuwalinda dhidi ya ukatili lakini pia amewahakikishia kuwa uongozi wa Mkoa uko tayari wakati wote kushirikiana nao bega kwa bega wanapotimiza majukumu yao.

“Ninawapongeza kwa kazi nzuri mnayoifanya ya kuwatunza na kuwalinda watoto wenye ualbino dhidi ya hatari za ukatili lakini pia na huduma ya matibabu lakini niwahakikishie kuwa uongozi wa Mkoa kupitia Maafisa Ustawi wa Jamii unawakaribisha sana na upo tayari kushirikiana nanyi bega kwa bega mnapotimiza majukumu yenu” amesema RC Macha.

Kwa upande wake Mratibu wa Afya kutoka Shirika la Standing Voice Bi. Christina Silas, ameeleza kuwa wamekuwa wakifanya Kliniki ya ngozi kwa watu wenye ualbino kila baada ya miezi sita (6) kwa kushirikiana na Ofisi ya Mkuu wa Mkoa na Ofisi za Wakurugenzi wa Halmashauri kupitia Maafisa Ustawi wa Jamii pamoja na madaktari kutoka Hospitali ya Kilimanjaro Christian Medical Centre (KCMC).

Shirika la Standing Voice linajishughulisha na utoaji wa huduma za Kliniki ya ngozi kwa watu wenye ualbino ili kufanyiwa uchunguzi wa ngozi na macho, utoaji wa elimu mbalimbali pamoja na mahitaji mengine kwa watu wenye ualbino yakiwemo kutoa kofia pana za kujikinga na mionzi ya jua, mafuta maalumu pamoja na miamvuli na endapo mtu atabainika kuwa na dalili za kansa hupewa rufaa kwenda Hospitali ya Kanda ya Bugando au Hospitali ya  Ocean Road na Shirika hugharamia matibabu hayo.

Matangazo

  • No records found
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • ENDELEENI KUTOA ELIMU ZAIDI KUHUSU AFYA YA AKILI - DC. MBONI

    May 30, 2025
  • TAKUKURU SHINYANGA YAANZA KUCHUKUA HATUA DHIDI YA UBADHIRIFU WA SHILINGI MILIONI 92 ZA WAKULIMA WA TUMBAKU WA USHETU - DONASIAN.

    May 27, 2025
  • MAISHA BAADA YA KUSTAAFU YANAHITAJI UTULIVU - DC. MTATIRO

    May 26, 2025
  • MAFUNZO YA IPOSA NI MKOMBOZI KWA VIJANA WALIO WENGI WANAOKOSA FURSA YA ELIMU YA KAWAIDA - RC. MACHA

    May 23, 2025
  • Angalia zote

Video

MIFUKO BANDIA ZAIDI YA ELFU 20 YAKAMATWA SHINYANGA
Video Nyinginezo

Viunganishi vya Haraka

  • Historia
  • Dira na Dhima
  • Hotuba Mbalimbali
  • Video Mbalimbali
  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Picha za Matukio
  • Miongozo na kanuni

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Mfumo wa kutuma, kupokea na kufuatilia malalamiko, mapendekezo, maulizo na pongezi
  • Ofisi ya Rais Menejimenti ya utumishi wa Umma
  • Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Boma Street, Mwanza Road

    Anuani: P.O.Box 320, Shinyanga

    Simu: +255 28 2762222

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras@shinyanga.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2018. Mkoa wa Shinyanga. Haki zote zimehifadhiwa