• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
    • eVibali |
Shinyanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Shinyanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Yetu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
      • Afya
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Shinyanga
    • Wilaya ya Kahama
    • Wilaya ya Kishapu
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu
    • Halmashauri ya Mji wa Kahama
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu
    • Halmashauri ya Wilaya ya Msalala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
    • Bandari Kavu
  • Huduma
    • Kutoa Ushauri wa Kitaalam
    • Kutafsiri Sheria na Sera
    • Kuratibu Shughuli za Wadau
    • Ulinzi na Usalama
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Tafiti
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha

RC MACHA APOKEA DARASA NA MADAWATI KUTOKA CRDB - SHINYANGA

Posted on: April 10th, 2024

Na. Paul Kasembo - KISHAPU.

MKUU wa Mkoa wa Shinyanga Mhe. Anamringi Macha amepokea mchango wa Darasa 1 na Madawati 20 kutoka CRDB BANK - Shinyanga ikiwa ni sehemu ya mrejesho utokanao na faida baada ya makato ya TRA yaani CSR iliyogharimi Tzs. Mil. 20 ambapo pamoja na kuwashukuru, kuwapongeza na kuwaomba tena CRDB lakini pia aliwataka wananchi kuvitunza ili viwanufaishe na wengine.

RC MACHA ameyasema haya tarehe 9 Aprili, 2024 alialikwa katika hafla ya kukabidhiwa mchango huu katika Kijiji cha Kiloleli Kata ya Kiloleli katika Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu ambapo pamoja na mambo mengine RC Macha ameahidi kupeleka tofali elfu 4 kwa ajili ya umaliziaji wa ujenzi wa vyumba vya madarasa 2 na ofisi moja ujenzi ambao umefikia hatua ya msingi.

"Tunawashukuru sana CRDB BANK Tawi la Shinyanga kwa mchango wenu wa darasa 1 na madawati 20, mchango ambao umehamasishwa na Ndg. Madaha Chaba ambaye ni mzaliwa wa kijiji hiki na mtumishi wa CRDB BANK Makao Makuu, hakika mmeacha alama kwa jamii yetu, nasi Serikali tutaendelea kushirikiana nanyi wakati wote," RC MACHA.

Kwa upande wake Meneja wa CRDB BANK Kanda ya Magharibi Mchumi Jumanne Wagana amesema kuwa Benki yao Tawi la Shinyanga iliamua kutekeleza hili baada ya kupokea wazo kutoka kwa mtumishi mwenzao na huu ni utaratibu wa kawaida kabisa wa Benki yao kurejesha sehemu ya faida kwa jamii ili kuweka miradi yenye kunufaisha wananchi katika eneo husika huku akiwasisitiza wananchi kutunza rasilimali hizi.

Shule ya Msingi Kiloleli kilianzishwa rasmi mwaka 1956 ina jumla ya wanafunzi 1949, walimu 9 na ilianza rasmi ujenzi wa darasa hili Mei, 2023 lenye madawati 20. Kukamilika kwa darasa hili kunatajwa kupunguza msongamano kwa wanafunzi katika shule hii.


HABARI PICHA



Matangazo

  • No records found
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • NATOA WITO KWA VIJANA HAPA SHINYANGA KUREJEA NA KUTATHIMINI UPYA NJIA ZA KUJIPATIA KIPATO - RC. MACHA

    May 20, 2025
  • SERIKALI YATHIBITISHA VIFO VYA WATU SITA NA MAJERUHI 11 KATIKA AJALI YA MGODI WA MWAKITOLYO.

    May 18, 2025
  • WAZAZI NA WALEZI, NENDENI MKAWE MABALOZI SAHIHI WA KAZI ZA MHE. RAIS DKT. SAMIA SULUHU HASSAN – RC. MACHA

    May 16, 2025
  • WAZAZI NA WALEZI WEKEZENI ZAIDI KATIKA MALEZI NA MAKUZI YA WATOTO – LYAMONGI

    May 15, 2025
  • Angalia zote

Video

MIFUKO BANDIA ZAIDI YA ELFU 20 YAKAMATWA SHINYANGA
Video Nyinginezo

Viunganishi vya Haraka

  • Historia
  • Dira na Dhima
  • Hotuba Mbalimbali
  • Video Mbalimbali
  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Picha za Matukio
  • Miongozo na kanuni

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Mfumo wa kutuma, kupokea na kufuatilia malalamiko, mapendekezo, maulizo na pongezi
  • Ofisi ya Rais Menejimenti ya utumishi wa Umma
  • Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Boma Street, Mwanza Road

    Anuani: P.O.Box 320, Shinyanga

    Simu: +255 28 2762222

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras@shinyanga.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2018. Mkoa wa Shinyanga. Haki zote zimehifadhiwa