• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
    • eVibali |
Shinyanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Shinyanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Yetu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
      • Afya
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Shinyanga
    • Wilaya ya Kahama
    • Wilaya ya Kishapu
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu
    • Halmashauri ya Mji wa Kahama
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu
    • Halmashauri ya Wilaya ya Msalala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
    • Bandari Kavu
  • Huduma
    • Kutoa Ushauri wa Kitaalam
    • Kutafsiri Sheria na Sera
    • Kuratibu Shughuli za Wadau
    • Ulinzi na Usalama
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Tafiti
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha

RC MACHA APONGEZA UJENZI WA HOSPITALI YA WILAYA YA MSALALA

Posted on: May 20th, 2024

RC MACHA APONGEZA UJENZI WA HOSPITALI YA WILAYA YA MSALALA


Na. Paul Kasembo, Msalala.

MKUU wa Mkoa wa Shinyanga Mhe. Anamringi Macha amepongeza ujenzi wa Hospitali ya Wilaya ya Msalala yenye majengo 15 ambayo imeanza kutoa huduma za afya mwezi Oktoba, 2022 huku akiwataka kuanzisha utaratibu wa kufanya vipimo kwa wananchi ambao siyo wagonjwa hasa wazee ili waweze kujuwa afya zao ikiwemo kipiko cha Figo.


RC Macha amemshukuru sana Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kuwezesha fedha za ujenzi wa Hospitali hii na kuwataka watumishi wa afya kuwa na lugha nzuri, uzalendo na uchapakazi ili kuunga mkono juhudi za Mhe. Rais.

Macha ameyasema haya leo tarehe 20 Mei, 2024 mara baada ya kukagua majengo, kuongea na wagonjwa pamoja na kupokea taarifa ya ujenzi huu ambao umejumuisha na nyumba za wahudumu wa Hospitali wakiwemo Madaktari ili kuwa karibu na utoaji huduma.

"Nimeridhishwa na ujenzi wa Hospitali ya Wilaya ya Msalala, hakika nawapongeza sana kwa mradi huu na kwakweli mmenifariji sana na kunifurahisha kulinganisha na baadhi ya eneo niliyopita kukagua Sekta hii ya afya, Msalala nawapongeza sana hongereni sana na pia tuendelee kumshukuru sana Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuwezesha ujenzi huu," amesema RC Macha.

Pamoja na mambo mengine, pia ameitaka TARURA Wilaya ya Kahama kuangalia namna ya kutengeneza barabara inayoingia Hospitalini hapo ili iweze kupitika wakati wote na bila kuwa shida ukizingatia inapeleka na kutoa wagonjwa wetu.

Akisoma taarifa ya Hospitali, Daktari Samweli Mapula ambaye ni Mganga Mfawidhi Hospitali ya Wilaya ya Msalala amesema kuwa mpaka sasa zaidi ya Bil. 2 zimekwisha kutumika katika ujenzi huu ulioanza mwaka 2019 na inahudumia wananchi katika Kata 18 za Halmashauri ya Wilaya ya Msalala pamoja na Halmashauri jirani za Mkoa wa Geita (Mbogwe).

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Msalala Ndg. Khamis Katimba amemueleza RC Macha kuwa yale yote aliyoelekeza na kushauri wameyapokea na kwamba watayafanyia kazi kwa haraka na kwa weledi zaidi ili kuboresha huduma kwa wananchi.


HABARI PICHA



Matangazo

  • No records found
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • KIKAO CHA MAPITIO YA ROBO MWAKA KWA KIPINDI CHA OKT - DES 2024 CHA (PJT MMMAM) CHAFANYIKA MKOANI SHINYANGA.

    February 28, 2025
  • RCC SHINYANGA YARIDHIA MAPENDEKEZO NANE (8) YA MATUMIZI BORA YA ARDHI.

    February 27, 2025
  • KUKAMILISHWA KWA MIRADI YA BARABARA KUTAPUNGUZA KERO KWA WANANCHI – RC MACHA

    February 26, 2025
  • WALIMU, TOENI ELIMU INAYOENDANA NA MABADILIKO YA TEKNOLOJIA -RC MACHA

    February 24, 2025
  • Angalia zote

Video

MIFUKO BANDIA ZAIDI YA ELFU 20 YAKAMATWA SHINYANGA
Video Nyinginezo

Viunganishi vya Haraka

  • Historia
  • Dira na Dhima
  • Hotuba Mbalimbali
  • Video Mbalimbali
  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Picha za Matukio
  • Miongozo na kanuni

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Mfumo wa kutuma, kupokea na kufuatilia malalamiko, mapendekezo, maulizo na pongezi
  • Ofisi ya Rais Menejimenti ya utumishi wa Umma
  • Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Boma Street, Mwanza Road

    Anuani: P.O.Box 320, Shinyanga

    Simu: +255 28 2762222

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras@shinyanga.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2018. Mkoa wa Shinyanga. Haki zote zimehifadhiwa