• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
    • eVibali |
Shinyanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Shinyanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Yetu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
      • Afya
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Shinyanga
    • Wilaya ya Kahama
    • Wilaya ya Kishapu
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu
    • Halmashauri ya Mji wa Kahama
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu
    • Halmashauri ya Wilaya ya Msalala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
    • Bandari Kavu
  • Huduma
    • Kutoa Ushauri wa Kitaalam
    • Kutafsiri Sheria na Sera
    • Kuratibu Shughuli za Wadau
    • Ulinzi na Usalama
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Tafiti
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha

RC MACHA ATOA WITO KWA WAZAZI NA WALEZI - SHINYANGA

Posted on: April 22nd, 2024

Na. Paul Kasembo, SHY RS.

MKUU wa Mkoa wa Shinyanga Mhe. Anamringi Macha ametoa wito wa kuwataka wazazi na walezi wote Mkoani Shinyanga kuhakikisha wanashiriki kikamilifu katika kuhamasisha, kuwaruhusu au kuwapeleka wasichan wenye umri wa kati ya miaka 9 hadi 14 katika shule zilizokaribu nao kwa ajili ya kupatiwa chanjo muhimu dhidi ya Saratani ya mlango wa kizazi huku akisisitiza kuwa chanjo hii haina madhara yoyote wa watoto wa kike.

Haya yamesemwa leo tarehe 22 Aprili, 2024 kwenye hafla yenye sura ya Kimkoa katika viwanja vya Shule ya Msingi Ndala A iliyopo Kata ya Masekelo, Manispaa ya Shinyanga ambapo RC Macha alikuwa akizindua Kampeni ya Wiki ya Chanjo ambayo imeanza leo na itadumu hadi tarehe 28, Aprili 2024 na kuhudhuriwa na viongozi mbalimbali wa Kiserikali, Kisiasa, wananchi na walengwa wenyewe ambao ni wanafunzi.

"Natoa wito huu kwenu wazazi na walezi wote Mkoa wa Shinyanga mhakikishe kuwa mnahamasisha na kuwapeleka watoto wenu wenye umri wa kati ya miaka 9 hadi 14 wakapate chanjo ukizingatia kuwa chanjo hii haina madhara yoyote," amesema RC Macha.

RC Macha amewakumbusha wananchi wote kuwa, kujuwa afya zao ni muhimu sana, hivyo kila mwananchi ajiwekee utaratibu wa kuwa anapima mara kwa mara hata kama haugui ili kuweza kujuwa mwenendo wa mwili wake badala ya kusubiria tukio muhimu kama hili.

Kando na hayo RC Macha pia ametoa angalizo kwa yeyote atakayejaribu kutumia mitandao ya kijamii kundika au kuripoti taarifa zinazohusu chanjo hii kwa lengo la kupotosha umma kwamba atachukuliwa hatua kali za kisheria ikiwa ni pamoja na kupelekwa mahakamani, kama hajaelewa ni vema akaja kupata ufafanuzi kwa wataalam wetu ambao watakuwa wakipatikana katika shule zote.

Chanjo hii iliyoanza kutolewa rasmi hapa Shinyanga, inatarajia kuwanufaisha wasichana 198,865 katika shule 887 ambapo kutakuwa na vituo vya kutolea huduma 238 na jumla ya Timu ya watoa huduma itakayohusika ni  242 na lengo litafikiwa kwa asilimia 100.


HABARI PICHA

RC Macha (kushoto) akimpatia zawadi mtoto wa kwanza kupata chanjo

Mkuu wa Wilaya ya Kishapu Mhe. Joseph Mkude ambaye anakaimu Wilaya ya Shinyanga akielezea jambo wakati wa uzinduzi


Mganga Mkuu Mkoa wa Shinyanga Daktari Yudas Ndungile 



Matangazo

  • No records found
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • KIKAO CHA MAPITIO YA ROBO MWAKA KWA KIPINDI CHA OKT - DES 2024 CHA (PJT MMMAM) CHAFANYIKA MKOANI SHINYANGA.

    February 28, 2025
  • RCC SHINYANGA YARIDHIA MAPENDEKEZO NANE (8) YA MATUMIZI BORA YA ARDHI.

    February 27, 2025
  • KUKAMILISHWA KWA MIRADI YA BARABARA KUTAPUNGUZA KERO KWA WANANCHI – RC MACHA

    February 26, 2025
  • WALIMU, TOENI ELIMU INAYOENDANA NA MABADILIKO YA TEKNOLOJIA -RC MACHA

    February 24, 2025
  • Angalia zote

Video

MIFUKO BANDIA ZAIDI YA ELFU 20 YAKAMATWA SHINYANGA
Video Nyinginezo

Viunganishi vya Haraka

  • Historia
  • Dira na Dhima
  • Hotuba Mbalimbali
  • Video Mbalimbali
  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Picha za Matukio
  • Miongozo na kanuni

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Mfumo wa kutuma, kupokea na kufuatilia malalamiko, mapendekezo, maulizo na pongezi
  • Ofisi ya Rais Menejimenti ya utumishi wa Umma
  • Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Boma Street, Mwanza Road

    Anuani: P.O.Box 320, Shinyanga

    Simu: +255 28 2762222

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras@shinyanga.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2018. Mkoa wa Shinyanga. Haki zote zimehifadhiwa