• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
    • eVibali |
Shinyanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Shinyanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Yetu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
      • Afya
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Shinyanga
    • Wilaya ya Kahama
    • Wilaya ya Kishapu
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu
    • Halmashauri ya Mji wa Kahama
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu
    • Halmashauri ya Wilaya ya Msalala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
    • Bandari Kavu
  • Huduma
    • Kutoa Ushauri wa Kitaalam
    • Kutafsiri Sheria na Sera
    • Kuratibu Shughuli za Wadau
    • Ulinzi na Usalama
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Tafiti
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha

RC MACHA AWAOMBA VIONGOZI WA DINI KUTOA MAFUNDISHO SAHIHI

Posted on: May 26th, 2024

Na. Paul Kasembo, SHY RS.

MKUU wa Mkoa wa Shonyanga Mhe. Anamringi Macha amewaomba viongozi wa dini zote kuendelea kutoa mafundisho yaliyo sahihi kwa waumini ambao ndiyo wananchi kwa upande wa Serikali ili kuweza kuleta maslahi mapana kwa pande zote mbili pamoja na  kusaidia utoaji wa elimu katika nyanja mbalimbali kwa umma huku akisisitiza kuwa Serikali itaendelea kushirikiana na Madhehebu yote ya dini katika kufikia lengo na maono ya Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ya kuwawezesha wananchi kuishi kwa amani na kuinua maisha yao kiuchumi, kijamii na kiutamaduni katika maeneo yao.

RC Macha ameyamesema haya  leo tarehe 26 Mei, 2024 alipokuwa akihutubia waumini wa Jumuiya ya Kikristo Tanzania (CCT) yenye wanachama 14 kutoka Madhehebu ya Kiprotestanti yenye mwelekeo wa Kikanisa kutoka Tanzania Bara na Visiwani ambayo ilianzoshwa tarehe 23 Jan, 1934 ambapo leo inatimiza miaka 90 ya uwepo wake ikiwa leo ni MAADHIMISHO YA SIKU YA CCT huku maadhimisho yakianisha baadhi ya lengo kuwa ni Kuimarisha Uinjilisti kikamilifu unaozingatia mafundisho yenye msingi wa YESU KRISTO.

"Niwaombe sana Viongozi wote wa Dini kuendelea kutoa mafundisho yaliyo sahihi kwa waumini ambao ndiyo wananchi kwa upande wa Serikali kuweza kuleta maslahi mapana kwa pande zote mbili pamoja sanjari na kutoa elimu kwa umma lengo ni kufikia kusudio kwa wananchi," amesema RC Macha.

Kando na wito huo, pia amewataka viongozi wa dini Mkoani Shinyanga kuendelea kutoa elimu ya utunzaji wa mazingira, kuimarisha usafi na kuelekeza jitihada katika kuelimisha waumini na wananchi juu ya matumizi ya Nishati Safi huku akisisitiza kwamba Serikali itaendelea kuweka miundombinu ya mazingira rafiki na wezeshi ili kuimarisha matumizi haya ya nishati safi ukizingatia Mkoa wa Shinyanga moja ya kazi kuu ni uchimbaji wa madini.

Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Shinyanga Mhe. Julius Mtatiro ametumia nafasi hii kuwakumbusha waumini wa CCT dhima ya Uumbaji na kwa nini tupo hapa duniani huku akisisitiza kupendana na kusaidiana wakati wote na huu ndiyo wito wake kwa waumini wote.

Matangazo

  • No records found
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • VIJANA, NJOONI SHAMBA MTAFANIKIWA ZAIDI - RC MACHA

    February 13, 2025
  • NIMERIDHISHWA NA KASI YA KILIMO CHA ZAO LA PAMBA HAPA WILAYANI KISHAPU - RC MACHA

    February 13, 2025
  • WANUFAIKA WA MIKOPO YA 10% LIPENI KWA WAKATI ILI PIA VIKOPESHWE NA VIKUNDI VINGINE - RC MACHA

    February 13, 2025
  • CP. HAMDUNI AKUTANA NA KAMATI YA MICHEZO YA JWTZ

    February 13, 2025
  • Angalia zote

Video

MIFUKO BANDIA ZAIDI YA ELFU 20 YAKAMATWA SHINYANGA
Video Nyinginezo

Viunganishi vya Haraka

  • Historia
  • Dira na Dhima
  • Hotuba Mbalimbali
  • Video Mbalimbali
  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Picha za Matukio
  • Miongozo na kanuni

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Mfumo wa kutuma, kupokea na kufuatilia malalamiko, mapendekezo, maulizo na pongezi
  • Ofisi ya Rais Menejimenti ya utumishi wa Umma
  • Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Boma Street, Mwanza Road

    Anuani: P.O.Box 320, Shinyanga

    Simu: +255 28 2762222

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras@shinyanga.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2018. Mkoa wa Shinyanga. Haki zote zimehifadhiwa