• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
    • eVibali |
Shinyanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Shinyanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Yetu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
      • Afya
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Shinyanga
    • Wilaya ya Kahama
    • Wilaya ya Kishapu
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu
    • Halmashauri ya Mji wa Kahama
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu
    • Halmashauri ya Wilaya ya Msalala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
    • Bandari Kavu
  • Huduma
    • Kutoa Ushauri wa Kitaalam
    • Kutafsiri Sheria na Sera
    • Kuratibu Shughuli za Wadau
    • Ulinzi na Usalama
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Tafiti
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha

RC MBONI MHITA ATETA NA MANAIBU WAZIRI KUHUSU AJALI YA MGODI WA NYANDOLWA – ATANGAZA MAENDELEO YA ZOEZI LA UOKOAJI

Posted on: August 19th, 2025

Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, Mhe. Mboni Mhita, leo Agosti 19,2025 amekutana na Naibu Waziri wa Madini Mhe. Dkt. Steven Kiruswa pamoja na Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi Mhe. Daniel Sillo, katika kikao kazi kilichofanyika ofisini kwake kwa lengo la kujadili mwenendo wa shughuli za uokoaji kufuatia ajali ya kuporomoka kwa Mgodi wa Nyandolwa uliopo katika Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga.

Katika mazungumzo hayo, RC Mhita ameeleza kuwa Serikali ya Mkoa kwa kushirikiana na vyombo vya ulinzi na usalama, taasisi za uokoaji pamoja na wadau mbalimbali, inaendelea na jitihada za kuwaokoa wachimbaji waliokwama mgodini tangu kutokea kwa ajali hiyo.

Mhe. Mhita amethibitisha kuwa hadi sasa jumla ya watu wanane (8) wameopolewa kutoka mgodini, ambapo kwa masikitiko makubwa mwili wa fundi mwingine umepatikana akiwa amefariki dunia, na hivyo kufanya idadi ya waliofariki kufikia watano. Aidha, mafundi 17 bado hawajafikiwa, na juhudi za kuwatafuta zinaendelea kwa kasi na umakini mkubwa.

 “Tunafanya kazi usiku na mchana kuhakikisha tunawafikia wote waliokwama. Serikali imeweka nguvu kubwa katika eneo hili la uokoaji, na tunashukuru kwa ushirikiano kutoka kwa vyombo vyote husika,” alisema Mhita.

RC Mhita pia amepongeza ujio wa Manaibu Waziri hao kwa kuonesha mshikamano na uzito wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika kushughulikia maafa ya aina hii, huku akiendelea kuwapa pole ndugu na familia za waathirika wa tukio hilo.

Serikali ya Mkoa imeendelea pia kutoa msaada wa chakula kwa familia zilizoathirika, na kuimarisha huduma muhimu katika eneo la tukio ili kuleta faraja kwa ndugu wanaosubiri hatima ya wapendwa wao.

Matangazo

  • No records found
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • KIKAO KAZI CHA MMMAM CHAFANYIKA SHINYANGA, KUWEKA MIKAKATI MADHUBUTI YA MALEZI NA MAKUZI BORA KWA MTOTO

    August 20, 2025
  • WAMILIKI WA VITUO VYA KULELEA WATOTO MCHANA SHINYANGA WAASWA KUSAJILI VITUO VYAO ILI KUTOA HUDUMA SALAMA KWA WATOTO

    August 20, 2025
  • RC MBONI MHITA ATETA NA MANAIBU WAZIRI KUHUSU AJALI YA MGODI WA NYANDOLWA – ATANGAZA MAENDELEO YA ZOEZI LA UOKOAJI

    August 19, 2025
  • RC MBONI MHITA APONGEZA TUME YA UTUMISHI WA MAHAKAMA KWA KUIMARISHA MAADILI NA UWAJIBIKAJI KWA WATUMISHI.

    August 19, 2025
  • Angalia zote

Video

MIFUKO BANDIA ZAIDI YA ELFU 20 YAKAMATWA SHINYANGA
Video Nyinginezo

Viunganishi vya Haraka

  • Historia
  • Dira na Dhima
  • Hotuba Mbalimbali
  • Video Mbalimbali
  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Picha za Matukio
  • Miongozo na kanuni

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Mfumo wa kutuma, kupokea na kufuatilia malalamiko, mapendekezo, maulizo na pongezi
  • Ofisi ya Rais Menejimenti ya utumishi wa Umma
  • Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Boma Street, Mwanza Road

    Anuani: P.O.Box 320, Shinyanga

    Simu: +255 28 2762222

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras@shinyanga.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2018. Mkoa wa Shinyanga. Haki zote zimehifadhiwa