• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
    • eVibali |
Shinyanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Shinyanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Yetu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
      • Afya
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Shinyanga
    • Wilaya ya Kahama
    • Wilaya ya Kishapu
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu
    • Halmashauri ya Mji wa Kahama
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu
    • Halmashauri ya Wilaya ya Msalala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
    • Bandari Kavu
  • Huduma
    • Kutoa Ushauri wa Kitaalam
    • Kutafsiri Sheria na Sera
    • Kuratibu Shughuli za Wadau
    • Ulinzi na Usalama
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Tafiti
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha

RC MHITA AAGIZA MKANDARASI KUKATWA MILIONI 2 KILA SIKU KWA KUCHELEWESHA BARABARA KAHAMA

Posted on: September 30th, 2025

Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Mhe. Mboni Mhita  ameonyesha kutoridhishwa na kasi ya ujenzi wa barabara za ndani katika Manispaa ya Kahama na kuagiza hatua kali zichukuliwe dhidi ya mkandarasi anayetekeleza mradi huo, Kampuni ya Sichuan Road and Bridge Group (SRBG).

Akiwa kwenye ziara ya kukagua maendeleo ya ujenzi huo unaotekelezwa kupitia Mradi wa TACTIC iliyofanyika Septemba 30,2025 RC Mhita amemuagiza Mkurugenzi wa Manispaa ya Kahama Masoud Kibetu kuandika barua rasmi kwa mkandarasi huyo, ikiambatana na adhabu ya kukatwa milioni 2 kwa kila siku kuanzia Oktoba 1, 2025, baada ya mkataba wake kufikia ukomo tarehe 30 Septemba 2025, bila kazi kukamilika.

“Mkandarasi huyu amelipwa zaidi ya shilingi bilioni 5, lakini kasi ya utekelezaji ni ya kusuasua licha ya kuongezewa muda mara mbili. Serikali haina tena sababu ya kumuongezea mkataba,” alisema Mhita kwa msisitizo.

Amesema Serikali ya Mkoa haitavumilia kuona fedha za umma zinatumika bila matokeo halisi, akisisitiza kuwa kila mkandarasi anapaswa kuzingatia muda wa utekelezaji na thamani ya fedha inayotolewa kwa miradi ya maendeleo.

Katika maagizo yake, Mhita amesisitiza kuwa adhabu hiyo ya kisheria inalenga kulinda maslahi ya wananchi ambao wanasubiri huduma bora za miundombinu na kuonya kuwa hatua zaidi za kisheria zitachukuliwa endapo mkandarasi atashindwa kumaliza kazi hiyo kwa haraka.

Ziara hiyo imekuwa sehemu ya msukumo wa kuhakikisha utekelezaji wa miradi ya maendeleo unakwenda kwa kasi inayostahili, huku RC Mhita akisisitiza uwajibikaji kwa watendaji wote na wadau wa ujenzi katika Mkoa wa Shinyanga


Nao baadhi ya wananchi waliokuwepo kwenye mradi huo walimpongeza RC Mhita kwa hatua alizochukua na kumuomba kumsimamia kwa ukaribu mkandarasi huyo katika kipindi ambacho Mvua zinatarajia kunyesha ili wasipate madhara yakiwemo mafuriko kutokana na kutokamilika kwa miundombinu katika manispaa ya Kahama.

Matangazo

  • No records found
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • RC MHITA AWAHAMASISHA WAFANYABIASHARA NA WAWEKEZAJI KUCHANGAMKIA FURSA ZA KIUCHUMI MKOANI SHINYANGA

    November 13, 2025
  • RC MHITA AKUTANA NA MSANII BANDO MC, APONGEZA JUHUDI ZA KUSAIDIA VIJANA SHINYANGA

    November 11, 2025
  • RC MHITA APONGEZA UONGOZI MPYA WA KANISA LA WASABATO NGBF MKOANI SHINYANGA.

    November 07, 2025
  • WANAFUNZI 29,193 KUFANYA MTIHANI WA UPIMAJI KIDATO CHA PILI SHINYANGA.

    November 07, 2025
  • Angalia zote

Video

RC MHITA AWAHAMASISHA WAFANYABIASHARA NA WAWEKEZAJI KUCHANGAMKIA FURSA ZA KIUCHUMI MKOANI SHINYANGA
Video Nyinginezo

Viunganishi vya Haraka

  • Historia
  • Dira na Dhima
  • Hotuba Mbalimbali
  • Video Mbalimbali
  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Picha za Matukio
  • Miongozo na kanuni

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Mfumo wa kutuma, kupokea na kufuatilia malalamiko, mapendekezo, maulizo na pongezi
  • Ofisi ya Rais Menejimenti ya utumishi wa Umma
  • Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    OFISI YA MKUU WA MKOA, MKOA WA SHINYANGA, 04 MTAA WA BOMA

    Anuani: P.O.Box 320, 37180,SHINYANGA, TANZANIA

    Simu: +255 28 2762222

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras@shinyanga.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2018. Mkoa wa Shinyanga. Haki zote zimehifadhiwa